JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,308
- 5,462
Liverpool ikiwa nyumbani kwenye Uwanja wa Anfield imelazimishwa matokeo ya 0-0 dhidi ya Manchester United katika mchezo wa Premier League ambapo Liverpool ilipewa nafasi kubwa ya kushinda kutokana na kuonesha ubora katika michezo ya hivi karibuni tofauti na wapinzani wao.
Matokeo hayo yanaifanya Liverpool “Jogoo wa Anfield” ibaki nafasi ya pili ikiwa na pointi 38 nyuma ya Arsenal yenye 39 katika msimamo wa ligi, Man. United “Mashetani Wekundu” imebaki nafasi ya 7 ikiwa na alama 28, timu zote zikiwa zimecheza mechi 17.
Matokeo hayo yanaifanya Liverpool “Jogoo wa Anfield” ibaki nafasi ya pili ikiwa na pointi 38 nyuma ya Arsenal yenye 39 katika msimamo wa ligi, Man. United “Mashetani Wekundu” imebaki nafasi ya 7 ikiwa na alama 28, timu zote zikiwa zimecheza mechi 17.