Nipo katika mitaa ya mji kasoro bahari kama kawaida naona jezi za CCM zimetapakaa maeneo mengi ya mji huku maroli na mabasi ya abiria yakisombawanachama toka pande zote za mkoa ili kuhudhuria mkutano wao.
Bodaboda zinaanza kuadimika mara baada ya CCM kuwakodisha kwenda katika maandamano
Kama kawaida yao Katibu wa Zanzibar aanza na mipasho kwa kukashifu CUF kuwa toka kinaanzishwa baba na mama na kitanda kilivyoanzishwa na mimba ilivyoingia anajua.
Ila kwa ufupi watu ni wachache mnoo sio kama ilivyotarajiwa na raia wengi wamekaa kwenye viti.
Updates.
Mbunge wa morogoro anaongea ila kama JK lazima asome.
Nape anaona watu wanaondoka anawambia Diamond anatudi stejini kuburudisha
Nipo katika mitaa ya mji kasoro bahari kama kawaida naona jezi za ccm zimetapakaa maeneo mengi ya mji huku maroli na mabasi ya abiria yakisombawanachama toka pande zote za mkoa ili kuhudhuria mkutano wao.
Bodaboda zinaanza kuadimika mara baada ya ccm kuwakodisha kwenda katika maandamano
Mimi huwa ninajiuliza, hivi CCM wanapoitisha mikutano kama hiyo wanawaambia nini wananchi? Maana tangu watuahidi maisha bora kwa kila mtanzania mwaka 2005, hali yetu ya maisha imekuwa mbaya kuliko ya awali, sasa wakija kwa wananchi wanasema nini?
Wanawapa sababu za maisha kuwa magumu zaidi, wanawaambia wavumilie hali inarekebishwa au wanawaambia CHADEMA wamekwamisha utekelezaji wa sera za CCM? Na wananchi tuna nini cha kutufanya tuwaamini hawa watu ambao ndiyo chanzo cha umaskini wetu?
Umaskini unaletwa na wananchi wenyewe. Hapa nawaona wazee hasa naweza waita mabibi kusema ukweli wamechoka jamani na kwa kuwatazama ni dhahiri njaa huko watokako ila baada ya kupewa vilemba na khanga wamesahau shida zote kwa ufupi wameweka shida chini
sidhani kama wana kipya zaidi ya kutumia muda wao wote kuwaponda chadema
na kujitakasa kuwa wao ni chama makini
nani asiejua ni chama cha wezi wa rasilimali zetu,tembo, kuhonga,mafisadi,kulindana na chama
kinachotumia bunge kwa maslalhi yao?
wana moro vaeni nguo za kijani kapokeeni mshiko lakini mtawaumbua ktik sanduku la kura 2015.
wajinga ndio waliwaoooo.
morogoro bado ni mkoa mgumu ki mageuzi, hasa morogoro mjini na kilosa, angalau kidogo ifakara, ruaha, na mvomero hasa turiani, huko wattu wameamka makala anaomba 2015 ifike aondoke maana hapati ushirikiano wowote huko mvomero hasa mtibwa tuliani
Naona watu wanaingia kikakundi kuonesha wamekuja kutoka sehemu moja kuna kosta kinaingia watoto wa mjini wanalizome ukiuliza watu wanasema wamekuja fiesta sababu P.A wamesema atakuepo lina chege temba na diamond
kwa sasa naona Chege yupo anatumbuiza,jamani hii ndio nini tena,watu sio wengi ukilinganisha na nguvu iliyotumika kuutangaza. updates: Diamond naye amepanda juktwaani,anatumbuisa pia.