Live updates: Kilele cha mbio za Mwenge mkoani Iringa

Wadau,

Kweli Mwenge umechosha watu. Nilikuwa najaribu kuangalia sherehe hizi kupitia TBC. Maajabu karibu uwanja mzima hauna watu pamoja na taarifa ya kukusanya idadi kubwa ya wanafunzi wa shule za msingi na sekondari hapo Iringa.

Nimetambua kuwa, hasira zinaweza kwenda kirahisi kwa Kamanda Msigwa.

"Tofauti zetu ndio raha zenyewe" by JK.
 
Wabunge washinikize bungeni huo mwenge ufutwe na upelekwe makumbusho mara moja, mwenge umekaa kichama zaidi badala ya kitaifa, tunaomba utujuze viongozi gani waliopo?
 
Namuona Mkuu wa Kaya anaelezea juu ya Ukimwi, simuelewi vizuri vile anamaanisha nini , najiuluza mwenge unamausiano yapi na huu Ukimwi?
 
Kwa nini wawalazimishe hao walimu na wanafunzi kwenda kujaza uwanja?kwa nini wasiwaache huru ili wapime kama huo mwenge unakubalika kwa asilimia ngapi?

na kwanini kila siku iwe ni walimu tu? Na sio wafanyakazi wengine kama mapolisi nk?
 
ondoa kwanza matangazo yote ya kupiga vita vita ukimwi , maana kama unaogopa ukimwi huwezi kuhudhuria tamasha la mwenge !
 
Nilishuhudia jana magari 30 yakija kuzindua msingi wa jengo la kituo cha polisi mtaani kwetu, kazi ambayo hata mkuu wa wilaya angeweza kuifanya peke yake. Baadae bila aibu wataanza tena kutuchangisha hela mtaani kwa ajili ya kumalizia kituo hicho
 
Jamani tuwe waungwana mbona naangalia live kupitia Tbc 1 na naona jinsi watu walivosheheni na Mc anasema huko nje nako watu kibao wanaendelea kuingia uwanjani,!!! Kusema sherehe zimedorora ni unafiki. Mwenge Oyeeeeeeeeeeee!!
huku kwetu Mwenge shughuli za mwenge ziligharimu zaid ya Tsh.180,000,000/=, na ulitembelea vijiji 3 na Kuzindua nyumba 3 vijijini vyenye jumla ya Tsh,22,000,000/= jamani tueleweni mwenge ni kudhalilishana.
 
Back
Top Bottom