Makoye Matale
JF-Expert Member
- May 2, 2011
- 6,490
- 2,104
- Thread starter
- #221
Tisha-TOTO
Mkuu, ni ukweli usiopingika (na mchungu kumeza kwa wana Simba) kuwa Yanga ndiyo timu iliyosheheni vipaji bora kuliko timu yo yote hapa Tanzania kwa sasa ukilinganisha one vs one. Hilo halina ubishi.
Ni kwa vile tu Yanga wamejichanganya siku za hivi karibuni kwa kitendo cha kubadili benchi la ufundi ambalo lilikuwa linafanya kazi vizuri bado (ubingwa msimu uliopita na kuiweka timu kileleni mwa ligi msimu huu). Hii ni moja ya oversight kubwa sana ya uongozi na ndicho kitu kimeifanya timu ianze kwa kusuasua round hii ya pili.
Hata hivyo, pamoja na yote haya, nina uhakika wa 110% Yanga ataibuka bingwa come end of the season. Hii ni kwa sababu ya uzoefu wa kikosi ambao unaowawezesha kuhimili pressure ambayo huwapo kwenye run-in stage ya ligi yoyote and the fact kuwa hata historia inawa-back Yanga kuwa huwa ni wazuri sana kwenye run-in stage. Azam bado sana uwezo wa ku-handle aina hii ya pressure. Simba ni jina kubwa lakini wachezaji wake bado wachanga ku-handle pressure kubwa. Mbeya City ni kama Simba.
Haya mambo maamuzi yenye utata wa marefa ni jambo lisilokwepeka (inevitable) kwenye ligi yoyote duniani. Nadhani mmesikia jana Mourinho akilalamika kuwa ManCity huwa wanabebwa, lakini anasahau kuwa Chelsea alikuwa apoteze mechi pale darajani msimu huu dhidi ya West Brom kama si maamuzi tata ya refa yaliyowaokoa.
Yanga mwenyewe ni victim mara kadhaa wa maamuzi tata ya marefa, ingawa ni ukweli usiopingika kuwa kuna mengine amenufaika nayo pia. Hii hutokea si kwa Yanga tu bali pia kwa Simba, Azam, Coastal, nk. At the end of the season, things tend to even themselves out!
Yaani weekend hii imekuwa tamu sana kwangu mimi mwenzenu.....
Liverpool 5 Arsenal 1
Yanga 7 Wakomoro 0
Mgambo 1 Simba 0.
It can't get better than this, can it?
Mliofurahi kama mimi kwa matokeo hayo yote matatu tuungane kufurahi pamoja!!
Msimbaziiiiiii
Msimbaziiiiiii
Tuko identical twins katika hili!
Panadol haisaidii mpwa...@Katavi pole sana meza panadol
Sisi wa arsenal na msimbazi wikendi hii imekuwa mbaya.Kitufe cha "like" hakipo active.....otherwise nimeku-LIKE sana!
Asante sana @Mtoboasiri.Pole jamaa yangu Katavi!
Sisi wa arsenal na msimbazi wikendi hii imekuwa mbaya.
Inategemea na timu, Mgambo inashika mkia halafu ndani ya dakika 90 mnakubali kipigo, wachezaji wetu wana matatizo hawajui maumivu wanayotusababishia, jiulize kuna watu wanatumia hela zao kusafiri kwenda kuwashangilia halafu wanaishia kupata maumivu hiyo ni haki kweli.
Inategemea na timu, Mgambo inashika mkia halafu ndani ya dakika 90 mnakubali kipigo, wachezaji wetu wana matatizo hawajui maumivu wanayotusababishia, jiulize kuna watu wanatumia hela zao kusafiri kwenda kuwashangilia halafu wanaishia kupata maumivu hiyo ni haki kweli.
Mkuu ushabiki wa mpira ni kama kabila huwezi kubadilisha sana sana utaacha baadhi ya mila za kabila lenu lakini huwezi kufanya total change ya kabila na mpira ni hivyo hivyo, ushabiki utafifia tu kushabikia timu yako kutokana na uzembe wanaofanya lakini huwezi kuihama kabisa.Kuna watu tulikuwa tiGO tukahamia Airtel kwa sababu ya mauzauza mengi, kwa nini wewe usihamie Yanga, Azam au hata Mbeya City; timu zinazofanya vizuri? Kwa nini uendelee kuumia kila siku. Ukiwa mbishi utaendelea kupata dhoruba. Kuna kipigo kingine cha nguvu kinawasubiri pale Mbeya, jifunge kiume usije ukaanguka.
Wasukuma tunasema 'kwibata' yaani unajifunga nguo (normally khanga) na kuipitisha katika mapaja yote ili kuhakikisha kuwa sehemu nyeti ziko salama, huku ukiwa kifua wazi ndipo uingie vitani. Mkuu Masuke mnatakiwa 'kwibata' kabla ya kukipiga na Mbeya City, vinginevyo MCC watagonga sehemu nyeti mapema na ndipo mtakapolegea na kutandikwa goli nyingi tu.
Mkuu ushabiki wa mpira ni kama kabila huwezi kubadilisha sana sana utaacha baadhi ya mila za kabila lenu lakini huwezi kufanya total change ya kabila na mpira ni hivyo hivyo, ushabiki utafifia tu kushabikia timu yako kutokana na uzembe wanaofanya lakini huwezi kuihama kabisa.
Mbeya City hawataamini kitakachowatokea hiyo jmosi.Sasa mjiandae 'kwibata' mnapokutana na Mbeya City.
Mshayamaliza yaliyowafanya mkose ushindi kwa mgambo?Mbeya City hawataamini kitakachowatokea hiyo jmosi.
tichaa said:Many teacher have to work not only for many hrs but also for a very small salary.
By TIE (english bk2 pg8)
What is ua commen?
Mshayamaliza yaliyowafanya mkose ushindi kwa mgambo?