ndenga
JF-Expert Member
- Dec 20, 2010
- 1,895
- 1,578
JK ndie sio tuu anaongoza umati wa Watanzania katika heshima za mwisho za Bob Makani, pali pia ni JK ndiye aliyetoa PA inayotumika hapa!.
Kitendo cha heshima za mwisho za Kiongozi na muasisi wa Chadema kuagwa kwa kutumia PA ya Mwenyekiti wa CCM ni kitendo cha uthibitisho wa baadhi ya mazuri ya Kikwete!. Nilisema JK ni mtu wa watu!.
Matumizi haya ya PA ya JK pia ni uthibitisho wa political tolerance kuwa upinzani wa vyama sio uadui, Watanzani ni wamoja kwenye shida na raha.
Nawaombeni wapenzi wa Chadema wenye nia njema, lazima mtamshukuru JK hata kimoyomoyo tuu!.
RIP Bob Makani!.
Saa hii Freeman Mbowe anaongea atafuatiwa na JK!.
Hiyo ni flash ya camera, siyo lebo.
Bodygurd wa Mbowe siku zote anapenda kusimama nyuma ya Mbowe pamoja kuwa ana kitambi lakini ni mwepesi kama Chadema wenyewe wanavyosema.
Mkuu Pasco, sikutegemea kama utaandika hivyo. Mimi hapa mtaani suala la ufuasi wa wa mtu wa chama fulani cha siasa huwa nalijua kipindi cha uchaguzi tu, na mtu akifiwa huwa hatuna hata chembe ya mawazo kwamba yeye ni chama gani. Nimeshtuka kuona ukiandika kwamba Public Addressing System (PA) inayotumika kwenye msiba huo (wa CDM) ni mali ya mwenyekiti wa CCM! Kuna ajabu gani hapo hadi uandike? Mbona mimi huwa natoa maturubai yangu au umeme wangu kwenye misiba ya wasio na vitu hivyo bila kujali vyama vyao vya siasa? Sijawahi kufikiria kama kuna mtu atakuja kutokea na hoja ya kisiasa kwenye msiba wa jirani! Pole sana Pasco, maybe JK alikushinda tender mliyo.bid wote katika kutoa huduma ya PA, lakini naona kama vile unamchafua JK hapa!
Kaka wachaga wamekukosea nini? Mbona unaonekana unawachukia sana. Au ni siasa za maji taka zinakusababisha uongee haya. Pole mkuu ila badilika,
Thubutu hawezi kuitoa hiyo lebo wanakodi hizo suti 10,
000 kwa saa halafu ni marufuku hata kukaa.
episodes, humu jf tuna tatizo na watu wenye kambi zao, hivyo mnataka kila mtu humu ama awe ni CCM au Chadema!.mkuu pasco kati ya watu niliowaona hawana misimamo ni wewe,mara kikwete hamtaki lowassa,mara kiwete hafai kuongoza,mara kikwete ni mtu wa watu,sasa unasimamia wapi mbona hueleweki????au ulisharudi kambi ya mkweree????ukipewa uongozi nchi hii utatusumbuwa sana wee jamaa
Siyo kwa hapa tu yatupasa watanzania kuelewa ya kuwa JK ni muungwana na tena siyo dikiteta kwani anayo nafasi kubwa sana ya kuukandamiza upinzani kama angependa lakini amewaacha tu waendeshe siasa bila kuwawekee mizengwe kama wafanyiwavyo wenzetu ktk nchi zinazotuzunguka,hata zinapofanyika chaguzi mbalimbali pale ccm inaposhindwa hatumii mabavu kulazimisha ushindi na hata kwenye mazishi ya kiongozi wa chama cha upinzani anashiriki kwa dhati,na hii ni ishara nyingine anatuonyesha ya kuwa hata ktk uchaguzi mkuu wa urais upinzani ukishinda hawezi kulazimisha ushindi kwa chama anachokiongoza atakubaliana na matokeo japo kibinadamu atakuwa anaumiaJK ndie sio tuu anaongoza umati wa Watanzania katika heshima za mwisho za Bob Makani, pali pia ni JK ndiye aliyetoa PA inayotumika hapa!.
Kitendo cha heshima za mwisho za Kiongozi na muasisi wa Chadema kuagwa kwa kutumia PA ya Mwenyekiti wa CCM ni kitendo cha uthibitisho wa baadhi ya mazuri ya Kikwete!. Nilisema JK ni mtu wa watu!.
Matumizi haya ya PA ya JK pia ni uthibitisho wa political tolerance kuwa upinzani wa vyama sio uadui, Watanzani ni wamoja kwenye shida na raha.
Nawaombeni wapenzi wa Chadema wenye nia njema, lazima mtamshukuru JK hata kimoyomoyo tuu!.
RIP Bob Makani!.
Saa hii Freeman Mbowe anaongea atafuatiwa na JK!.