Mwandishi aliyeshinda Tuzo ya CNN ahoji nini kimemtokea Lissu?Aliwatukana Acacia/Barrick kwa miaka 20, leo anawatetea? Ataka uchunguzi wa kina.
@ Lissu, aliwatukana kwa miaka 20, baada ya magufuri kuingia madarakani na kukata mirija ya makinikia, Lissu akaanza kuwatetea, hapo ndo shida ilipoanzia kupelekea kutaka kumalizwa kabisa kidogo. Kwa nini hakuwatetea kipindi cha kikwete cha Shamba la Bibi, kitu gani alipewa na hao wazungu, pia kwenye share za Acacia 36.1% ambazo kampuni mama Barrick ilitaka kununua, Acacia walikataa katakata kuziuza kwa Barrick, wenye hizo share ni akina nani, pia kipindi cha mwanzo kabisa cha timbwili la makinikia, kuna viongozi wa juu kabisa awamu ya nne walipanda ndege hadi Toronto Canada kuweka mambo sawa yasije bumbuluka. Je Lissu alitumwa na nani awatetee Acacia pamoja na kuwaponda zaidi ya miaka 20. Ukifumbua hiki kitendawili utajuwa ni kwa nini Lissu alitaka kumalizwa kabisa. Je ni kwa upande aliokuwa anatetea au upande wa pili. Ndo maana hata akipiga kelele kiasi gani wazungu wanaojua kwa undani jambo hili watakuwa wanampa mkono Lissu kwa mbele wakimpa mgongo wanasema idiot guy.
Pia nyoka waliyoko ubarozi wetu Canada, je ndo walimtoa barozi kidatu kutaka kuingizwa kwenye pay slip ya hao jamaa wanaomiliki hizo asilimia 36.1% za Acacia.