Bhikalamba
JF-Expert Member
- Dec 6, 2015
- 2,340
- 3,361
Katika kipindi Cha hivi karibuni Chadema wamezindua kampeni ya 'No reform -No election' (NRNE).
Lissu kama mwenyekiti na icon ya chama amejikita zaidi kuelezea ubovu wa katiba na Sheria mbovu za uchaguzi, zinazopekelea kutokuwa na chaguzi zilizo Huru na Haki (free and fair elections). Hili ni sawa kabisa, na yeyote mwenye uelewa, kuangazia mbele na kulitakia mwema TAIFA hili huku akiweka uchawa na maslahi binafsi pembeni, atakubali kuwa Kuna haja kubwa ya kufanya reforms kwenye tume na namna ya uendeshaji wa chaguzi zetu.
Ili kupata uungwaji mkono wa umma wa watanzania, na kuishinikiza serikali kufanya reforms, Lissu na Chadema Kwa ujumla wakaja na kampeni hii. Aidha, Chadema hawana jeshi, wanategemea nguvu ya umma kushinikiza hili.
Hivyo ili wapate kuungwa mkono na majority ya watanzania (siyo wanachadema tu), Lissu apanue Wigo kutoka katika kuwa gwiji wa sheria na kujipambanua zaidi Kwa wananchi Kwa kuangazia masuala ya uchumi, huduma za jamii na maendeleo ya wananchi. Ajikite kujenga hoja kwa kuwaeleza wananchi mambo yanayo wagusa Moja Kwa Moja kama ajira, huduma za jamii, kilimo, uchumi, rushwa na marekebisho ya Sheria ya mifuko ya jamii hususani NSSF Kwa kurejeshwa fao la kujitoa au kuruhusu mtu kulipwa fedha zake zote anapopoteza ajira ndani ya kipindi Cha miezi Sita, marekebisho juu ya kikotoo n.k.
Yeye kama icon ya chama anapaswa kuwaeleza wananchi jinsi CCM ilivyo shindwa kutatua kero za wananchi, nini CHADEMA itafanya na kwanini wananchi wanapaswa kuiamini CHADEMA na kuikataa CCM, halafu ndo aingize habari za madhaifu ya katiba na chaguzi zetu na mwisho apigilie msumari wa 'No reform -No election'.
Aidha napendezwa na jinsi Heche anavyojenga hoja; anaongelea masuala yanayowagusa wananchi kwa kutoa mifano ya nchi mbali mbali. Na ni Kwa namna gani sera mbovu za CCM na usimamizi duni wa raslimali za TAIFA, unazorotesha maendeleo ya nchi, huku akijenga matumaini ya wananchi juu ya Chadema.
Nakutanabahisha Lissu, usifanye hotuba zako zikatawaliwa na maudhui Moja tu ya uchaguzi. Wananchi wataona huna unachowaletea au kuwatetea zaidi ya kupigania tume huru ili kupata madaraka Kwa manufaa yako ya kisiasa na Chama chako. Pia ukweli mchungu ni kuwa epuka kumtaja taja Magufuli, pamoja na madhaifu na madhila yote ya Magufuli bado Kwa watanzania walio wengi ikichagizwa na Madhaifu ya awamu hii ya mama, Magufuli amekuwa branded au kuonekana kama mtetezi wa wanyonge na shujaa wa watanzania. (Though he was fickle, dictator, impassive and sadist. But you can not ignore public sentiments in regard to him).
Katika ulingo ya siasa unapaswa kuangazia mambo yafuatayo:
1. Tambua na kuzungumzia changamoto au matatizo yanayoikabili jamii ya eneo husika na TAIFA Kwa ujumla. (Addressing social problems)
1. Taja Madhaifu ya mpinzani wako, Kwa Chadema Mpinzani wao ni CCM . (Disreputation of your opponent)
2. Toa hoja au sera mbadala kushughulikia changamoto zinazoikabili jamii. (Suggest alternatives or solutions)
3. Jenga matumaini ya wananchi juu yako au Chama chako.(Instill hopes)
**********************************
Nakala Kwa: Erythrocyte , Pascal Mayalla , Bams , Yericko Nyerere , Yoda , johnthebaptist 'et al'
Lissu kama mwenyekiti na icon ya chama amejikita zaidi kuelezea ubovu wa katiba na Sheria mbovu za uchaguzi, zinazopekelea kutokuwa na chaguzi zilizo Huru na Haki (free and fair elections). Hili ni sawa kabisa, na yeyote mwenye uelewa, kuangazia mbele na kulitakia mwema TAIFA hili huku akiweka uchawa na maslahi binafsi pembeni, atakubali kuwa Kuna haja kubwa ya kufanya reforms kwenye tume na namna ya uendeshaji wa chaguzi zetu.
Ili kupata uungwaji mkono wa umma wa watanzania, na kuishinikiza serikali kufanya reforms, Lissu na Chadema Kwa ujumla wakaja na kampeni hii. Aidha, Chadema hawana jeshi, wanategemea nguvu ya umma kushinikiza hili.
Hivyo ili wapate kuungwa mkono na majority ya watanzania (siyo wanachadema tu), Lissu apanue Wigo kutoka katika kuwa gwiji wa sheria na kujipambanua zaidi Kwa wananchi Kwa kuangazia masuala ya uchumi, huduma za jamii na maendeleo ya wananchi. Ajikite kujenga hoja kwa kuwaeleza wananchi mambo yanayo wagusa Moja Kwa Moja kama ajira, huduma za jamii, kilimo, uchumi, rushwa na marekebisho ya Sheria ya mifuko ya jamii hususani NSSF Kwa kurejeshwa fao la kujitoa au kuruhusu mtu kulipwa fedha zake zote anapopoteza ajira ndani ya kipindi Cha miezi Sita, marekebisho juu ya kikotoo n.k.
Yeye kama icon ya chama anapaswa kuwaeleza wananchi jinsi CCM ilivyo shindwa kutatua kero za wananchi, nini CHADEMA itafanya na kwanini wananchi wanapaswa kuiamini CHADEMA na kuikataa CCM, halafu ndo aingize habari za madhaifu ya katiba na chaguzi zetu na mwisho apigilie msumari wa 'No reform -No election'.
Aidha napendezwa na jinsi Heche anavyojenga hoja; anaongelea masuala yanayowagusa wananchi kwa kutoa mifano ya nchi mbali mbali. Na ni Kwa namna gani sera mbovu za CCM na usimamizi duni wa raslimali za TAIFA, unazorotesha maendeleo ya nchi, huku akijenga matumaini ya wananchi juu ya Chadema.
Nakutanabahisha Lissu, usifanye hotuba zako zikatawaliwa na maudhui Moja tu ya uchaguzi. Wananchi wataona huna unachowaletea au kuwatetea zaidi ya kupigania tume huru ili kupata madaraka Kwa manufaa yako ya kisiasa na Chama chako. Pia ukweli mchungu ni kuwa epuka kumtaja taja Magufuli, pamoja na madhaifu na madhila yote ya Magufuli bado Kwa watanzania walio wengi ikichagizwa na Madhaifu ya awamu hii ya mama, Magufuli amekuwa branded au kuonekana kama mtetezi wa wanyonge na shujaa wa watanzania. (Though he was fickle, dictator, impassive and sadist. But you can not ignore public sentiments in regard to him).
Katika ulingo ya siasa unapaswa kuangazia mambo yafuatayo:
1. Tambua na kuzungumzia changamoto au matatizo yanayoikabili jamii ya eneo husika na TAIFA Kwa ujumla. (Addressing social problems)
1. Taja Madhaifu ya mpinzani wako, Kwa Chadema Mpinzani wao ni CCM . (Disreputation of your opponent)
2. Toa hoja au sera mbadala kushughulikia changamoto zinazoikabili jamii. (Suggest alternatives or solutions)
3. Jenga matumaini ya wananchi juu yako au Chama chako.(Instill hopes)
**********************************
Nakala Kwa: Erythrocyte , Pascal Mayalla , Bams , Yericko Nyerere , Yoda , johnthebaptist 'et al'