Lissu: Makinikia yameshaondoka, Hatujalipwa kitu, Acacia bado wanasafirisha dhahabu, Bombardier siyo mpya, Dreamliner haina kibali cha kuruka nje

Ndege kuharibika haimaanishi kuwa ndege hiyo ni chakavu.
Kuna ajali za kugonga ndege wanyama huko angani kunakopelekea uharibifu wa propeler.
main-qimg-9c7719d9bd1360e43488b1662482d198-c.jpg
PAY-Flybe-plane-which-was-disabled-by-a-birdstrike.jpg
1415700279403_wps_17_The_propeller_on_a_Flybe_.jpg
 
Mngekuwa mnaweka ushahidi kuongea kama walevi mnataka mjibiwe nini? No evidence talking like parrits.Enzi za Slaa chadema wakituhumu kitu mtu kubisha ngumu wanakuwa wamesheheni ushahidi wa uhakika hii ya akina Lisu mmmmmm
It is very simple my dear, prove him wrong,

September rusha dreamliner to Bombay,
Semeni Mwanza airport hakuna bombardier iliyokwama,
Makontena ya makinikia yapo,
Trillion 425 na $300 zimeshalipwa,
Tuambieni Acacia hawachimbi au wameshapata leseni mpya.

Mkiendelea kuimba tu Lissu muongo pasipo kuusema ukweli mnaoujua watu wataendelea kuamini maneno ya Lissu.
 
Lissu anapewa habari za uongo kama yule dada,naye kwa kukurupuka anazirusha ili ajipatie political mileage.
Lissu ni wa kupuuzwa hakuna jipya hapo yote ameshawahi kutolea mapovu,akafeli sasa amepaka rangi tu,maneno ni yale yale
Uongo wake ni UPI
Je T400 au B300 tumelipwa?
Je Makinikia bado hapo au yamendoka?
Je kamati iliundwa au la?
Je kibali cha IATA kipo?
Je Ndege iliharibika au la?
 
Lissu acha uongo.. Mainjinia ndio wanarusha ndege? Ndege inarushwa na Pilots na Pilots wengi wameshaenda Simulator course ya Dreamliner na wanaruka wazawa.. Kwnn unakuwa muongo hivi?

Kuhusu mainjinia (AME) wameenda type rating course na wamefaulu na wana rating endorsed in their AME licences..!! Kwnini Lissu muongo hivi? Na ni wazawa..!! Alafu sheria ya IATA kuhusu kuruka International flight ni kuwa na ndege zaidi ya moja ya kufanya safari za International flights.. Na sio eti tumekosa IOSA-IATA certificate.. So once tukipata ndege ya pili ya masafa marefu next year, IATA itatoa certificate ya kufanya International flights, so huo ni utaratibu wa kawaida kabisa.. Ila sio hizo sbb Lissu alizosema.. Lissu muongo sana sana.. Hivi vitu ni very scientific & technical sio kama political barking Lissu anayofanya..!!:mad::mad::oops: And no one ana ubavu wa kupinga mambo ya kisayansi haya sio siasa hii..!!:mad::oops:

Na lissu alitaka mje mkiri hamjapata kibali cha kuruka nje?? Na mmekiri mazima mazima hamna kibali till 2020 ......aliyeturoga na afufuke basi....
 
Jiwe kabana makinikia kwa mbwembwe nyiiingi, then kaja kayaachia kimyakimya!
Kweli jiwe kazi yake kuvuruga tu, kila anachogusa anavuruga tu!
Labda ndiyo maana Propesa Kalamaganda Kabugi kapotea kwenye limelight ili wafukunyuku wasimuulize makinikia yako wapi na Trilion zetu 424 zitakuja lini!
Kuna official alisema sasa hivi tukilipwa hatutangazi kwa sababu wamaotudai watatukuja.

Makinikia tumelipwa!
 
Waalimu wanapanda daladala bure ?
Wale kahaba pale Kona bar wameisha ?
Wale bongo movies wamezuia movie za nje?
Wale waliotelekeza watoto wameishia wapi ?
Gesi ya Ntwara ipo bado ? Inazalisha umeme ?
Mil 50 Kila Kijiji
Tukimaliza kuondoa wafanyakazi hewa tunapandisha mishahara.
Oh sorry nadhani ntakuwa nimelewa.
Waalimu wanapanda bure na wanavitambulisho vya kupanda bure!! Mkuu labda haupo TZ au hujafuatilia mpaka kitu kiripotiwe JF ndo ufuatilie
 
Siamini kama Makinikia yameondoka hadi niende mwenyewe bandarini nikaangalie pale yalipokuwepo. Hatari sana
 
Uongo wake ni UPI
Je T400 au B300 tumelipwa?
Je Makinikia bado hapo au yamendoka?
Je kamati iliundwa au la?
Je kibali cha IATA kipo?
Je Ndege iliharibika au la?
Tatizo lenu mnataka kila kazi inayofanyika muambiwe,mna mkiambiwa mnasema utawala wa kiki
ndege sio sawa na gari ukitakata kwenda kenya unajiendea tu,kibali kipo kwenye mchakato soon dege litaanza safari,hata atangazo ya Dar to Entebbe,bujumbura,comoro mumbai,hujayaona?
 
*Anaandika Hon TunduLissu*

Further thoughts apropos makinikia na Bombardier za Magufuli:

Je, makinikia yaliyokuwa yamezuiliwa bandarini bado yapo??? Mimi nimeambiwa na a highly placed source kwamba yameachiliwa kimya kimya na kusafirishwa nje.

Kwa hiyo hatujalipwa shilingi trilioni 495 alizozisema Jiwe na professorial rubbish yake.

Hatujalipwa dola milioni 300 walizodai Wazungu wa makinikia wamekubali kulipa ex gratia.

Acacia Mining, tulioambiwa hawana hata leseni za uchimbaji, wanaendelea na uchimbaji Nyamongo wilayani Tarime, na wanasafirisha dhahabu yote nje ya Tanzania kama ilivyokuwa zamani.

Na Acacia Mining wameshafunga Mgodi wa Buzwagi baada ya kumaliza dhahabu yote, na wamesimamisha uzalishaji Bulyanhulu kusubiri uamuzi wa kesi ya arbitration, waliyoitolea notisi mara baada ya Magufuli kukamata makinikia.

Wahenga walisema 'wajinga ndio waliwao.' Tumeliwa!!!!

Kuhusu Bombardier za Magufuli:

Nimeambiwa kuwa mojawapo kati ya zile Bombardier mbili za mwanzo imeharibikia Mwanza kitambo sasa. Apparently, zote mbili hazikuwa mpya.

Na kati ya mbili zilizobaki, ile iliyokuwa imekamatwa Canada kwa sababu ya Magufuli kuvunja mkataba nayo ni mbovu. Ilikwenda Mwanza ikashindwa kurudi kwa sababu engine haikuwa na nguvu na kulikuwa na crack kwenye mojawapo ya rotor blades zake.

Naambiwa aliyekuwa Waziri wa Uchukuzi Profesa Makame Mbarawa aliunda Tume ya wataalamu wa Wizara yake kuchunguza masuala haya.

Tume ilikabidhi Taarifa yake na, naambiwa, imethibitisha kuwa tuliuziwa ndege kuukuu. Taarifa hiyo imekaliwa mahali.

Kuhusu Dreamliner:

Bila shaka mnafahamu kwamba safari pekee iliyofanya nje ya Tanzania ni ile ya kutoka Seattle, Marekani, kuja Tanzania. Tangu ifike inafanya safari za Dar, KIA na Mwanza tu.

Sababu ni hii: Air Tanzania haina certificate ya Ukaguzi wa Usalama wa Uendeshaji wa shirika la ndege (IOSA - IATA Operational Safety Audit) inayotolewa na Shirika la Kimataifa la Usafiri wa Anga (IATA) kwa kila shirika la ndege mwanachama.

Kwa taarifa nilizopewa, mainjinia wote waliopelekwa Marekani kwa ajili ya mafunzo ya kuendesha Dreamliner ile wamefeli mitihani yao mara mbili. Hawawezi kuruhusiwa kuirusha.

Kwa hiyo, hadi sasa, Dreamliner inaendeshwa bado na mainjinia wa Boeing Corporation walioileta Tanzania. Na hadi hapo ATCL itakapopata IOSA certification, haitaruka popote nje ya Tanzania.

Sio tu ATCL haikuwa na, na bado haina, business plan, inaelekea hakukuwa hata na maandalizi ya kuwa na shirika la ndege lenye kutimiz masharti ya kusafirisha abiria nje ya Tanzania.

Narudia tena: wajinga ndio waliwao!!!!!
 
*Anaandika Hon TunduLissu*

Further thoughts apropos makinikia na Bombardier za Magufuli:

Je, makinikia yaliyokuwa yamezuiliwa bandarini bado yapo??? Mimi nimeambiwa na a highly placed source kwamba yameachiliwa kimya kimya na kusafirishwa nje.

Kwa hiyo hatujalipwa shilingi trilioni 495 alizozisema Jiwe na professorial rubbish yake.

Hatujalipwa dola milioni 300 walizodai Wazungu wa makinikia wamekubali kulipa ex gratia.

Acacia Mining, tulioambiwa hawana hata leseni za uchimbaji, wanaendelea na uchimbaji Nyamongo wilayani Tarime, na wanasafirisha dhahabu yote nje ya Tanzania kama ilivyokuwa zamani.

Na Acacia Mining wameshafunga Mgodi wa Buzwagi baada ya kumaliza dhahabu yote, na wamesimamisha uzalishaji Bulyanhulu kusubiri uamuzi wa kesi ya arbitration, waliyoitolea notisi mara baada ya Magufuli kukamata makinikia.

Wahenga walisema 'wajinga ndio waliwao.' Tumeliwa!!!!

Kuhusu Bombardier za Magufuli:

Nimeambiwa kuwa mojawapo kati ya zile Bombardier mbili za mwanzo imeharibikia Mwanza kitambo sasa. Apparently, zote mbili hazikuwa mpya.

Na kati ya mbili zilizobaki, ile iliyokuwa imekamatwa Canada kwa sababu ya Magufuli kuvunja mkataba nayo ni mbovu. Ilikwenda Mwanza ikashindwa kurudi kwa sababu engine haikuwa na nguvu na kulikuwa na crack kwenye mojawapo ya rotor blades zake.

Naambiwa aliyekuwa Waziri wa Uchukuzi Profesa Makame Mbarawa aliunda Tume ya wataalamu wa Wizara yake kuchunguza masuala haya.

Tume ilikabidhi Taarifa yake na, naambiwa, imethibitisha kuwa tuliuziwa ndege kuukuu. Taarifa hiyo imekaliwa mahali.

Kuhusu Dreamliner:

Bila shaka mnafahamu kwamba safari pekee iliyofanya nje ya Tanzania ni ile ya kutoka Seattle, Marekani, kuja Tanzania. Tangu ifike inafanya safari za Dar, KIA na Mwanza tu.

Sababu ni hii: Air Tanzania haina certificate ya Ukaguzi wa Usalama wa Uendeshaji wa shirika la ndege (IOSA - IATA Operational Safety Audit) inayotolewa na Shirika la Kimataifa la Usafiri wa Anga (IATA) kwa kila shirika la ndege mwanachama.

Kwa taarifa nilizopewa, mainjinia wote waliopelekwa Marekani kwa ajili ya mafunzo ya kuendesha Dreamliner ile wamefeli mitihani yao mara mbili. Hawawezi kuruhusiwa kuirusha.

Kwa hiyo, hadi sasa, Dreamliner inaendeshwa bado na mainjinia wa Boeing Corporation walioileta Tanzania. Na hadi hapo ATCL itakapopata IOSA certification, haitaruka popote nje ya Tanzania.

Sio tu ATCL haikuwa na, na bado haina, business plan, inaelekea hakukuwa hata na maandalizi ya kuwa na shirika la ndege lenye kutimiz masharti ya kusafirisha abiria nje ya Tanzania.

Narudia tena: wajinga ndio waliwao!!!!!
upumbavuuuu mtupu....ko yule captain alie iletaa ni wa Boeing au siooo.....wait and see...#mtapata_tabu_sanaaa
 
Captain Shahid kumbe ni mtu wa boeing?? Mbona Tundu anadanganya uma
Ndege hairushwi na mtu mmoja, unayemtaja ni msaidizi wa mruchaji pia lazima use na uhakika kwenye chumba cha marubani kinatakiwa kiwe na watu wangapi, ndege kubwa ni zaidi ya wawili.
 
Back
Top Bottom