Further thoughts apropos makinikia na Bombardier za Magufuli:
Je, makinikia yaliyokuwa yamezuiliwa bandarini bado yapo??? Mimi nimeambiwa na a highly placed source kwamba yameachiliwa kimya kimya na kusafirishwa nje.
Kwa hiyo hatujalipwa shilingi trilioni 495 alizozisema Jiwe na professorial rubbish yake.
Hatujalipwa dola milioni 300 walizodai Wazungu wa makinikia wamekubali kulipa ex gratia.
Acacia Mining, tulioambiwa hawana hata leseni za uchimbaji, wanaendelea na uchimbaji Nyamongo wilayani Tarime, na wanasafirisha dhahabu yote nje ya Tanzania kama ilivyokuwa zamani.
Na Acacia Mining wameshafunga Mgodi wa Buzwagi baada ya kumaliza dhahabu yote, na wamesimamisha uzalishaji Bulyanhulu kusubiri uamuzi wa kesi ya arbitration, waliyoitolea notisi mara baada ya Magufuli kukamata makinikia.
Wahenga walisema 'wajinga ndio waliwao.' Tumeliwa!!!!
Kuhusu Bombardier za Magufuli:
Nimeambiwa kuwa mojawapo kati ya zile Bombardier mbili za mwanzo imeharibikia Mwanza kitambo sasa. Apparently, zote mbili hazikuwa mpya.
Na kati ya mbili zilizobaki, ile iliyokuwa imekamatwa Canada kwa sababu ya Magufuli kuvunja mkataba nayo ni mbovu. Ilikwenda Mwanza ikashindwa kurudi kwa sababu engine haikuwa na nguvu na kulikuwa na crack kwenye mojawapo ya rotor blades zake.
Naambiwa aliyekuwa Waziri wa Uchukuzi Profesa Makame Mbarawa aliunda Tume ya wataalamu wa Wizara yake kuchunguza masuala haya.
Tume ilikabidhi Taarifa yake na, naambiwa, imethibitisha kuwa tuliuziwa ndege kuukuu. Taarifa hiyo imekaliwa mahali.
Kuhusu Dreamliner:
Bila shaka mnafahamu kwamba safari pekee iliyofanya nje ya Tanzania ni ile ya kutoka Seattle, Marekani, kuja Tanzania. Tangu ifike inafanya safari za Dar, KIA na Mwanza tu.
Sababu ni hii: Air Tanzania haina certificate ya Ukaguzi wa Usalama wa Uendeshaji wa shirika la ndege (IOSA - IATA Operational Safety Audit) inayotolewa na Shirika la Kimataifa la Usafiri wa Anga (IATA) kwa kila shirika la ndege mwanachama.
Kwa taarifa nilizopewa, mainjinia wote waliopelekwa Marekani kwa ajili ya mafunzo ya kuendesha Dreamliner ile wamefeli mitihani yao mara mbili. Hawawezi kuruhusiwa kuirusha.
Kwa hiyo, hadi sasa, Dreamliner inaendeshwa bado na mainjinia wa Boeing Corporation walioileta Tanzania. Na hadi hapo ATCL itakapopata IOSA certification, haitaruka popote nje ya Tanzania.
Sio tu ATCL haikuwa na, na bado haina, business plan, inaelekea hakukuwa hata na maandalizi ya kuwa na shirika la ndege lenye kutimiza masharti ya kusafirisha abiria nje ya Tanzania.
Narudia tena: wajinga ndio waliwao!!!!!
Je, makinikia yaliyokuwa yamezuiliwa bandarini bado yapo??? Mimi nimeambiwa na a highly placed source kwamba yameachiliwa kimya kimya na kusafirishwa nje.
Kwa hiyo hatujalipwa shilingi trilioni 495 alizozisema Jiwe na professorial rubbish yake.
Hatujalipwa dola milioni 300 walizodai Wazungu wa makinikia wamekubali kulipa ex gratia.
Acacia Mining, tulioambiwa hawana hata leseni za uchimbaji, wanaendelea na uchimbaji Nyamongo wilayani Tarime, na wanasafirisha dhahabu yote nje ya Tanzania kama ilivyokuwa zamani.
Na Acacia Mining wameshafunga Mgodi wa Buzwagi baada ya kumaliza dhahabu yote, na wamesimamisha uzalishaji Bulyanhulu kusubiri uamuzi wa kesi ya arbitration, waliyoitolea notisi mara baada ya Magufuli kukamata makinikia.
Wahenga walisema 'wajinga ndio waliwao.' Tumeliwa!!!!
Kuhusu Bombardier za Magufuli:
Nimeambiwa kuwa mojawapo kati ya zile Bombardier mbili za mwanzo imeharibikia Mwanza kitambo sasa. Apparently, zote mbili hazikuwa mpya.
Na kati ya mbili zilizobaki, ile iliyokuwa imekamatwa Canada kwa sababu ya Magufuli kuvunja mkataba nayo ni mbovu. Ilikwenda Mwanza ikashindwa kurudi kwa sababu engine haikuwa na nguvu na kulikuwa na crack kwenye mojawapo ya rotor blades zake.
Naambiwa aliyekuwa Waziri wa Uchukuzi Profesa Makame Mbarawa aliunda Tume ya wataalamu wa Wizara yake kuchunguza masuala haya.
Tume ilikabidhi Taarifa yake na, naambiwa, imethibitisha kuwa tuliuziwa ndege kuukuu. Taarifa hiyo imekaliwa mahali.
Kuhusu Dreamliner:
Bila shaka mnafahamu kwamba safari pekee iliyofanya nje ya Tanzania ni ile ya kutoka Seattle, Marekani, kuja Tanzania. Tangu ifike inafanya safari za Dar, KIA na Mwanza tu.
Sababu ni hii: Air Tanzania haina certificate ya Ukaguzi wa Usalama wa Uendeshaji wa shirika la ndege (IOSA - IATA Operational Safety Audit) inayotolewa na Shirika la Kimataifa la Usafiri wa Anga (IATA) kwa kila shirika la ndege mwanachama.
Kwa taarifa nilizopewa, mainjinia wote waliopelekwa Marekani kwa ajili ya mafunzo ya kuendesha Dreamliner ile wamefeli mitihani yao mara mbili. Hawawezi kuruhusiwa kuirusha.
Kwa hiyo, hadi sasa, Dreamliner inaendeshwa bado na mainjinia wa Boeing Corporation walioileta Tanzania. Na hadi hapo ATCL itakapopata IOSA certification, haitaruka popote nje ya Tanzania.
Sio tu ATCL haikuwa na, na bado haina, business plan, inaelekea hakukuwa hata na maandalizi ya kuwa na shirika la ndege lenye kutimiza masharti ya kusafirisha abiria nje ya Tanzania.
Narudia tena: wajinga ndio waliwao!!!!!