Mdaiwa-Sugu
JF-Expert Member
- Mar 8, 2020
- 284
- 910
Mapokezi anayopata Tundu lissu kila mahali anakopita ni ishara ya watu kuchoka na watu wamechoka kweli kweli wala siyo utani.
√ Vijana wanalia na ukosefu wa ajira
√ Watumishi wanalia na nyongeza ya mishahara
√ Wastaafu wanalia na malipo yao ya uzeeni
√ Wajasiriamali wadogo wanalia na vitambulisho vya machinga
√ Wananchi wanalia ugumu wa maisha kutokana na mzunguko mdogo wa pesa mtaani
√ CCM tunalia ila tumeamua kuwa wanafiki tusifukuzwe uanachama.
Ni vilio kila mahali. Umefika wakati uvumilivu umekosekana; watu wameamua kuonyesha hisia zao kwa Lissu wakiamini ndiye mkombozi wao na hiyo ndio siri ya kupokelewa na kulakiwa kwa maelfu kila mahali.
Kwakuwa ni karibu kila mtu ameguswa na utawala huu; ikitokea H.E Magufuli ameanguka Urais. Siku hiyo kutazuka sherehe baab kubwa na ndio utakuwa mwanzo wa kuwajua wanafiki wake wa karibu waliokuwa wanamshauri vibaya.
Huenda andiko hili likatimia kwa sababu apangalo Mungu mwanadamu hawezi kupangua.
√ Vijana wanalia na ukosefu wa ajira
√ Watumishi wanalia na nyongeza ya mishahara
√ Wastaafu wanalia na malipo yao ya uzeeni
√ Wajasiriamali wadogo wanalia na vitambulisho vya machinga
√ Wananchi wanalia ugumu wa maisha kutokana na mzunguko mdogo wa pesa mtaani
√ CCM tunalia ila tumeamua kuwa wanafiki tusifukuzwe uanachama.
Ni vilio kila mahali. Umefika wakati uvumilivu umekosekana; watu wameamua kuonyesha hisia zao kwa Lissu wakiamini ndiye mkombozi wao na hiyo ndio siri ya kupokelewa na kulakiwa kwa maelfu kila mahali.
Kwakuwa ni karibu kila mtu ameguswa na utawala huu; ikitokea H.E Magufuli ameanguka Urais. Siku hiyo kutazuka sherehe baab kubwa na ndio utakuwa mwanzo wa kuwajua wanafiki wake wa karibu waliokuwa wanamshauri vibaya.
Huenda andiko hili likatimia kwa sababu apangalo Mungu mwanadamu hawezi kupangua.