JOHN MADIBA
JF-Expert Member
- Jan 30, 2011
- 251
- 155
MBUNGE wa Singida Mashariki, Tundu Lissu, (CHADEMA), amewataka vijana ambao ni wasomi kuacha woga na badala yake wafanye mapambano ya kimageuzi katika kutafuta haki pamoja na kulinda rasilimali za nchi.
Akizugunza na wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) kwa lengo la kuwajengea msimamo wa kisiasa, alisema wanafunzi wamekuwa wakitishwa na viongozi walio madarakani kwa madai kuwa vyama vya upinzani vinasababisha uvunjifu wa amani nchini, jambo ambalo alisema ni uzushi wa kisiasa.
Alisema ili Tanzania iweze kuwa na maendeleo ya kweli, ni lazima vijana kuhakikisha wanasimamia maamuzi ambayo ni ya kweli katika kutetea maslahi ya rasilimali ambazo zinatumiwa vibaya na viongozi walio serikalini.
Mbunge huyo aliwataka wanafunzi ambao wanatafuta ukombozi wa nchi yao watambue kuwa suala la kutafuta ukombozi na mabadiliko ya nchi si lelemama, bali unatakiwa ujasiri wa hali ya juu.
Katika mkutano huo pia Lissu amechoma kadi 35 za wanachuo ambao walikuwa wanachama Chama cha Mapinduzi (CCM) ambao wamejiunga na CHADEMA
Akizugunza na wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) kwa lengo la kuwajengea msimamo wa kisiasa, alisema wanafunzi wamekuwa wakitishwa na viongozi walio madarakani kwa madai kuwa vyama vya upinzani vinasababisha uvunjifu wa amani nchini, jambo ambalo alisema ni uzushi wa kisiasa.
Alisema ili Tanzania iweze kuwa na maendeleo ya kweli, ni lazima vijana kuhakikisha wanasimamia maamuzi ambayo ni ya kweli katika kutetea maslahi ya rasilimali ambazo zinatumiwa vibaya na viongozi walio serikalini.
Mbunge huyo aliwataka wanafunzi ambao wanatafuta ukombozi wa nchi yao watambue kuwa suala la kutafuta ukombozi na mabadiliko ya nchi si lelemama, bali unatakiwa ujasiri wa hali ya juu.
Katika mkutano huo pia Lissu amechoma kadi 35 za wanachuo ambao walikuwa wanachama Chama cha Mapinduzi (CCM) ambao wamejiunga na CHADEMA