Habari zenu
Leo nimeona ni vyema wana jikoni na wazazi tujadili na tubadilishane mawazo kuhusu lishe za watoto wetu kuanzia umri wa miezi 6 hadi mwaka.....
Nini madhumuni hasa
1)kwa wale watoto ambao hawapendi kula au hatujatambua bado nini wanapenda lakini kuna mzazi yeyote ameona chakula flani kime work kwake basi tu share nasi kujaribu kama kitapendwa pia....
2)tujuzane trick gani unatumia wakati wa kumlisha mtoto binafsi mimi huwa namfunga kwenye kiti chake alafu nampa kijiko au kipaja cha kuku sasa wakati anafungua mdomo kutafuna alichokikamata mie namuwahi kupitisha kijiko cha chakula hii inasaidia sana na tricks nyengine tutazidi kujuzana...
Karibuni wote tujadili au tupia recipe zako....
Mniwie radhi kwa uandishi wangu usio rasmin lol
Mwanangu alipokua na umri huo alikua foodie mashallah, asbh anapata uji wa oats mchana natengeza bondo nalikmix na supu km ya kuku , carot, mchicha etc then tunablend unakua km uji anakula vizuri na choo anapata kizuri
Nimeipenda hiyo trick yeye anakusudia kula nyama lakini anajikuta kachomekewa chakula asichotarajia
MaashAllah wa kwangu anapenda ukubwa anataka kula mwenyewe ati na akila anajiramba utacheka ila vyakula vyake hapendi sana yaani kwa ugomvi nimfanye namlisha yeye baba ake na mie nile apo kidogo atakula siku akiamua hataki kitu ni nyonyo tu nakomajeee
Watoto wanakinai chakula haraka, hivyo ni vyema kuwa na ratiba ya kumbadilishia chakula kila baada ya siku 2 au 3. Mtoto wetu ana miezi 9 nikimlisha mimi anakataa, akimlisha mama yake anakubali. Ushauri kwa wazazi: Acheni kuwapa watoto wachanga chakula kilicho andaliwa kwa ajili xa watu wakubwa chenye chumvi nyingi.
Mimi mwanangu hapendi kula lkn anapenda maji sana kwa hiyo nikimlisha nampa kijiko kimoja chakula na vijiko viwili vya maji basi anakula vizuri na anakuwa anameza ata km hataki