Lishe kwa mtoto - Unampikia nini mtoto wako (miezi 6-12)

nilianza na uji wa unga wa muhogo

nilikua naupika wa nazi siweki sukari wala chumvi

nambadiliahia naweka maziwa nikiweka maziwa nikawa naweka sukar kwa mbali na chumvi

nikajamsagia lishe, nauchanganya na maziwa anakumywa asubuh

mchana namsagia ndiz mbivu au nachanganya ndiz mbivu na parachichi sometimes chungwa nalikamua nampa

wakati mwengine namchemshia ndizi bukoba kwenye supu aidha yasamaki au nyama then nablend nachanganya na maziwa narudisha jikoni
vichemke kidogo naepua vikipoa nampa vikkwa vya uvuguvugu saa kum jion maziwa fresh baada ya hapo analinyonya tu ziwa la mama yake

pia hua napenda kumbadilishia badilishia sometimes nachemsha mchele has uive naepua naweka kwenye blender lakini namwaga maji badala ya kisaga na maji nasagia maziwa fresh narudisha kwenye sufuria naweka sukari kidogo narudisjha jikon vichemke pamoja

au

nachukua yai na ndizi bukoba nachemsha vikiwa tayari naepua namenya yai nachukua kiini na ndizinasaga pamoja na vijichumvi kwa mbaaali na maziwa kidogo nampa
 
Wangu ana miezi & anapenda sana mchanganyiko wa ndizi parachichi na embe.
Namsagia inakuwa smooth kwa blenda.
Uji nampa dona.nachanganya na maziwa,blubend,
Anapenda machungwa mno.
Kila siku nambadilishia smoothie ya matunda mchanganyiko ili asikinai.
Anaku ugali pia.
Alianza kuota meno na 4 morth
Sasa ana miezi 8,
Ana meno 6,
Anasimamia vitu na kuna mda mwingine anasimama dede mwenyewe
 
Wangu ana miezi saba.
Asubuhi anakula rojo la samaki mbichi+ maini siku moja moja+mboga ya majani iliosagwa/carrot
Mchana, ugali laini + mboga yoyote iliopo wakati huo
Jioni kiini cha yai la kienyeji+maziwa
Usiku kunyonya tu kwa mama ake.
 
Wangu ana miezi & anapenda sana mchanganyiko wa ndizi parachichi na embe.
Namsagia inakuwa smooth kwa blenda.
Uji nampa dona.nachanganya na maziwa,blubend,
Anapenda machungwa mno.
Kila siku nambadilishia smoothie ya matunda mchanganyiko ili asikinai.
Anaku ugali pia.
Alianza kuota meno na 4 morth
Sasa ana miezi 8,
Ana meno 6,
Anasimamia vitu na kuna mda mwingine anasimama dede mwenyewe
Maziwa gan mkuu haya ya kopo ama
 
kweli mkuu mimi wangu kiukweli alianza uji mwepesi akiwa na mwezi 1. alitusumbua sana usiku halali ni kulia mwanzo mwisho.tuka gundua mtoto alia kwa ajili ya njaa, pili tukagundua kuwa maziwa ya mama ni mepesi hali iniyo mfanya mtoto asiwe anashiba.

siku tulipo kapa uji mwepesi usiku aisee kesho yake kaliamka saa mbili asubuhi badal ya saa kumi au kumi na moja
Wooow maskini
 
Habari zenu

Leo nimeona ni vyema wana jikoni na wazazi tujadili na tubadilishane mawazo kuhusu lishe za watoto wetu kuanzia umri wa miezi 6 hadi mwaka.....

Nini madhumuni hasa

1)kwa wale watoto ambao hawapendi kula au hatujatambua bado nini wanapenda lakini kuna mzazi yeyote ameona chakula flani kime work kwake basi tu share nasi kujaribu kama kitapendwa pia....


2)tujuzane trick gani unatumia wakati wa kumlisha mtoto binafsi mimi huwa namfunga kwenye kiti chake alafu nampa kijiko au kipaja cha kuku sasa wakati anafungua mdomo kutafuna alichokikamata mie namuwahi kupitisha kijiko cha chakula hii inasaidia sana na tricks nyengine tutazidi kujuzana...


Karibuni wote tujadili au tupia recipe zako.


===============================


Lishe (1) - UJI WA OATS NA NDIZI/APPLE


Mahitaji

Oats kiasi

Apple 1 au ndizi ya kuwiva...

Maziwa...

Sukari (sio lazima)...

Namna ya kutaarisha

Chemsha maji

Weka oats acha zichemke hadi kuwiva

Ponda ponda ndizi vizuri weka maziwa kidogo ipondeke vizuri....

Mimina kwenye oats alafu weka na maziwa acha ichemke kidogo kwa dakika 3

Epua mlishe mtoto.....



Lishe (3) - WALI WA YAI

Mahitaji

Yai 1....tumia kiini tu

Siagi kidogo

Mchele....

Namna ya kutaarisha...

Pika wali kama wa kawaida ila weka maji mengi uwe laini bwabwa wengine wanaita bondo

Ukikaribia kuwiva weka yai ulolivunja koroga haraka haraka uchanganyike vizuri

Weka siagi na chumvi kidogo ukipenda....

Epua mlishe mtoto....


Lishe (3) - KAROTI NA KUKU


Mahitaji

Karoti

Kuku kiasi


Namna ya kutaarisha

Chemsha kuku hadi kuwiva iwe na supu kidogo

Weka karoti na subiria kuwiva...

Toa kuku pembeni alafu mchambue mifupa tupa

Weka katika blenda kuku na katoti na supu yako saga

Tayari kwa kumlisha mtoto

Ukipendeza waweza weka na viazi



Endelea kufuatilia mjadala kwa ushauri na lishe zaidi....
Kutayarisha na SIO
Kutaarisha!
Kiswahili fasaha.
Asante.
 
Lishe ya mtoto kwanzia miezi 6 na kuendelea,hata mtu mzima anaweza tumia pia.
1.Maindi lishe
2.Soya
3.Karanga/Korosho
4.Mbegu za maboga
5.Iriki
 
Habari zenu

Leo nimeona ni vyema wana jikoni na wazazi tujadili na tubadilishane mawazo kuhusu lishe za watoto wetu kuanzia umri wa miezi 6 hadi mwaka.....

Nini madhumuni hasa

1)kwa wale watoto ambao hawapendi kula au hatujatambua bado nini wanapenda lakini kuna mzazi yeyote ameona chakula flani kime work kwake basi tu share nasi kujaribu kama kitapendwa pia....


2)tujuzane trick gani unatumia wakati wa kumlisha mtoto binafsi mimi huwa namfunga kwenye kiti chake alafu nampa kijiko au kipaja cha kuku sasa wakati anafungua mdomo kutafuna alichokikamata mie namuwahi kupitisha kijiko cha chakula hii inasaidia sana na tricks nyengine tutazidi kujuzana...


Karibuni wote tujadili au tupia recipe zako.


===============================


Lishe (1) - UJI WA OATS NA NDIZI/APPLE


Mahitaji

Oats kiasi

Apple 1 au ndizi ya kuwiva...

Maziwa...

Sukari (sio lazima)...

Namna ya kutaarisha

Chemsha maji

Weka oats acha zichemke hadi kuwiva

Ponda ponda ndizi vizuri weka maziwa kidogo ipondeke vizuri....

Mimina kwenye oats alafu weka na maziwa acha ichemke kidogo kwa dakika 3

Epua mlishe mtoto.....



Lishe (3) - WALI WA YAI

Mahitaji

Yai 1....tumia kiini tu

Siagi kidogo

Mchele....

Namna ya kutaarisha...

Pika wali kama wa kawaida ila weka maji mengi uwe laini bwabwa wengine wanaita bondo

Ukikaribia kuwiva weka yai ulolivunja koroga haraka haraka uchanganyike vizuri

Weka siagi na chumvi kidogo ukipenda....

Epua mlishe mtoto....


Lishe (3) - KAROTI NA KUKU


Mahitaji

Karoti

Kuku kiasi


Namna ya kutaarisha

Chemsha kuku hadi kuwiva iwe na supu kidogo

Weka karoti na subiria kuwiva...

Toa kuku pembeni alafu mchambue mifupa tupa

Weka katika blenda kuku na katoti na supu yako saga

Tayari kwa kumlisha mtoto

Ukipendeza waweza weka na viazi



Endelea kufuatilia mjadala kwa ushauri na lishe zaidi....
Waoohhh asante kwa somo
 
Thread muhimu kama hizi kibongobongo utaona zinaenda zinafika page moja, mbili.

Tena hapo kwa kujipigia self promo wenyewe sana.

Leta stories za shoga kaenda kwa mganga kalirudisha buzi lake uone, thread itafika mpaka page mia kama ripoti ya Kamati ya Mahesabu ya bunge.
Kaka upo kimya sana
 
Back
Top Bottom