mkuu kwa nini tusijadili maendeleo ya mtwara kwa kina na kwa mantiki ya kutatua matatizo ya mtwara na siyo kutatua kwa vurugu kama unavyofikili wewe,na unafikiri vurugu na mandamano ndiyo yataleta maendeleo.
mkuu dua la kuku halimpati mwewe unaweza kutangulia ukamwacha jk kwa sabu mungu siyo athumani kaka؛
AGRRECO Wameacha kuzalisha umeme na sasa wanafanya biashara ya mafuta?
nikukumbushe tu kuwa Maendeleo yaliyoletwa na Gaddafi kule Libya yalitokana na Mapinduzi, Rwanda ya leo haishikiki kimaendeleo kwa sababu watawala wanajua nini kitatokea wakifanya fyongo makusudi, China ya leo iko vile unajua source yake, hebu angalia Cuba ya Fiedel Casto uone. Target ni maendeleo, njia ilosaidia kupatikana kwake does not make any difference, kikubwa ujue hakuna machafuko ya kudai haki yalodumu milele na yote yalipomalizika maendeleo yamekuwepo
Umeshawahi kujiuliza dunia ya leo ingekuwaje kama Hiltler asingetolewa na vita ya pili ya dunia? Marekani ingekuwa wapi kama siyo mapinduzi ya 1770's, ingekuwa wapi ufaransa ya leo, Mkwawa je, angeishi miaka 100 ka bi Kidude kama asingepapana na wajerumani?
Yuko wapi Steven Bicco, wapi Lumumba, au unajua sababu ya mapinduzi Zanzibar?
halafu AGGRECO inawauma sana kuona tatizo la umeme linaisha nchini. wanafurahia matatizo haya ili wao waendelee kutuuzia umeme kwa bei kubwa na waiuzie tanesco mafuta kwa bei kubwa kupitia hayo makampuni yao ya mafuta
mkuu, tamaa za madaraka na fedha ndo zinawaponza
Hebu CCM tekelezeni hayo madai ya Wana Mtwara tuone kama kutakuwa na FUJO huko Mtwara. Nayo ni Kujenga kiwanda cha mbolea, kujenga viwanda vya kuchakata gesi Mtwara, sio Bagamoyo na DSM, Kujenga mitambo ya kuzalisha umeme wa gasi Mtwara na baadaye kuuiingiza kwenye gridi ya Taifa, Kupanua bandarini ya Mtwara etc.
Wananchi wa Mtwara hawatazubaishwa na hizo propaganda zenu za mwaka 47