Lipumba awavaa viongozi CHADEMA

Lipumba awavaa viongozi CHADEMA

Kwa kuwa Cuf na ccm ni serikali. Mi naona ni sawa CUF kuwashambulia Wapinzani. Kwa sasa ni chama tawala(ccm/cuf..tlp,nccr) Vs upinzani cdm.) wako wako sawa tu.
 
Kwa kuwa Cuf na ccm ni serikali. Mi naona ni sawa CUF kuwashambulia Wapinzani. Kwa sasa ni chama tawala(ccm/cuf..tlp,nccr) Vs upinzani cdm.) wako wako sawa tu.
 
Siku hizi bila kuiongelea CHADEMA hauwezi kupata public atention ya kukusikiliza, sio kosa lake. kwani hata humu JF hamuoni kwamba hakuona tena hoja za msingi, kila siku thread ni CHADEMA iko hivi na Dr Slaa yuko vile. watu wamepatwa na stress kwa mziki wa CHADEMA.
 
CHADEMA msigombane na mbwa (read CUF) gombaneni na mwenye mbwa (read CCM)
 
Mtatiro, je Zanzibar kina mama hawaendi hospitali na viwembe? Ni bara peke yake? Huo uozo wa CCM upo upande mmoja tu wa nchi hii? Anayedharau hapa ni nani?

mh.Msando leo nakutuma,nakutuma naomba uende nakutuma. Nakutuma kwa uongozi wa cdm,akiwemo mh.Mbowe na katibu wake dakta Slaa,uwaeleze kuwa wananchi tumewaomba rasmi kutojiingiza ktk mchuano wowote na Prof.Lipumba na CUF nzima. Mkuu,cdm isitumie muda kujibizana na watu tuliowanyima kura wenyewe,tulijua hawaaminiki na tukawaacha. Mkuu,nakutuma wewe kwa kuwa nikifika hapa simuoni dr wala Mbowe ila najua kwa sasa wako busy na mikakati ya ndani ya chama. Nakuomba kwa heshimu kubwa ukifika uwaeleze kuwa wananchi wamesema waacheni CUF waropoke wala msiwajibu,wanatafuta sababu.
 
Yan badala ya kukosoa chama tawala we unakomaa na chadema, nahic cuf wamekosa mwelekeo
 
yaani wanaacha kugombana na ccm iliyoko madarakani wanagombana m2 wanayeona atachukua nchi soon,,,endeleeni na upinzani dhidi ya cdm mpaka itakapochukua nchi,,,uzeni sela zenu kwa wananchi,,,,,,,,ukitanga kutongoza dem uciingie kwa gia ya kumponda mwanaume mwenzako ili ufanikiwe,,,
 
Kwa kuwa Cuf na ccm ni serikali. Mi naona ni sawa CUF kuwashambulia Wapinzani. Kwa sasa ni chama tawala(ccm/cuf..tlp,nccr) Vs upinzani cdm.) wako wako sawa tu.
Chama Tawala? mbona hawana kauli yeyote katika serikali ya Znz? Hukumsikia Shein sikukuu ya mapinduzi kuwa wanatekaleza sera za CCM kwenda mbele na Maalim Seif akabaki anakodoa macho. CUF sio chama tawala ila ni hawara(concubine) wa chama Tawala.
 
Ndugu zangu wafanyabiashara na wapiga disko wa Chadema wanataka kuwang'oa mapapa ya ufisadi wa CCM ili wao manyangumi ya ufisadi waweze kuingia madarakani, hawana nia thabiti ya kupambana na rushwa,” alisema Profesa Lipumba.

Alisema aliingia kwenye siasa kwa lengo la kuwasaidia Watanzania sio kutafuta sifa kama walivyo baadhi ya wanasiasa wa Chadema.


"Sikuingia kwenye siasa kutafuta sifa, nimeingia kutumia elimu yangu kuwatafutia ukombozi Watanzania wenzangu, sasa hawa Chadema hawawezi kuiondoa CCM kwa kuwa wanachochea mgawanyiko mkubwa ndani ya nchi kwa kuwatukana Wanzanzibari waliokubali Serikali ya Umoja wa Kitaifa,” alisema Profesa Lipumba.


Hapa Profesa nimekukubali kabisaaaaaaa.

Wanataka kuleta machafuko makubwa sana na uvunjifu wa amani nchini
 
Ufisadi wa CHadema uko wapi jamani. Mmmmmh!!!! Nimegundua njaa haina cha msomi aisee. Usingetegemea maneno kama haya ayaseme profesa wa uchumi aliyekubuhu lakini mbele ya njaa na kujipendekeza imetokea. "Profesa" pekee ambaye tungemwelewa kama angesema maneno kama haya ni "profesa" maji marefu.

Hapa ndipo unakata tamaa kabisa na wasomi wa nchi hii. Maana wako tayari kupeleka usomi wao likizo ili kujipendekeza kwa wanasiasa. Prof LiPUMBA anajua kabisa kuwa hoja anazoengea ni PUMBA tupu na zinadhalilisha usomi wake lakini bado yuko tayari kuzitetea kwa nguvu zote.

Nadhani msaada wetu sasa tuutegemee kwa Mungu tu. Heaven has to do something for this country to develop.
 
CUF ni chama ambacho kimeundwa ili kama CCM wakiwa na rais kafiri wale wasiotaka ongozwa na kafiri wanahamia huko. najua wengi watakasirika lakini siko hapa kuwaambia watu kile wanachopenda ila hiyo ni kweli. Alipokuwa mkapa CUF strong na huyu weak . Just wait 2015!
 
CUF ni chama ambacho kimeundwa ili kama CCM wakiwa na rais kafiri wale wasiotaka ongozwa na kafiri wanahamia huko. najua wengi watakasirika lakini siko hapa kuwaambia watu kile wanachopenda ila hiyo ni kweli. Alipokuwa mkapa CUF strong na huyu weak . Just wait 2015!

Mtamaliza matusi ote lakini Prof Ni msomi aliyebobea kwenye uchumi na ana uzoefu mkubwa sana na siasa za tanzania.

Ukweli unaumaaaaaa eheeeeeeee, badilikeni muwe na uso wa kitaifa sio ukanda, ukabila na udini.
 
kuchanganyikiwa alianza mtikila akaja ,mrema sasa imehamia kwa lipumba. tumsubiri na yeye akagombee ubunge tabora
 
Mtamaliza matusi ote lakini Prof Ni msomi aliyebobea kwenye uchumi na ana uzoefu mkubwa sana na siasa za tanzania.

Ukweli unaumaaaaaa eheeeeeeee, badilikeni muwe na uso wa kitaifa sio ukanda, ukabila na udini.
msomi akishachanganyikiwa ni bure, afadhali ambaye hajasoma lakini ni timamu
 

“Ndugu zangu wafanyabiashara na wapiga disko wa Chadema wanataka kuwang'oa mapapa ya ufisadi wa CCM ili wao manyangumi ya ufisadi waweze kuingia madarakani, hawana nia thabiti ya kupambana na rushwa,” alisema Profesa Lipumba.


Ukiona ''Profesa wa CUF'' anasema majungu badala ya kutoa hoja ya msingi ujue gamba la nje linaanza kujivua na kiumbe halisi kilijojificha kinaanza kuonekana na hapo ndo tunaanza kuwajua CUF halis ni nani hasa: hatari kuliko sumu.

Siasa za Tanzania zinafanya kazi kama biological evolution: kama mchujo vile wa asili ambapo taratibu tunaanza kuona chama kipi cha siasa kiko fit kwa kizazi chetu kijacho na vipi viko dhaifu ambavyo havipaswi kabisa kutuwakilisha katika vizazi vyetu vijavyo. Na kwa ufupi naweza kusema CUF ni chama dhaifu!
 
PROF. LIPUMBA Kapoteza muelekeo kabisa wa kisiasa na kiuongozi, Kweli usipofikia malengo ya kisiasa unapagawa na kuchanganyikiwa kweli leo CDM wamekuwa mafisadi NYANGUMI na CCM ndio mafisadi PAPA? Hata kama mimi sio Prof. huyo Prof wa CUF kachemsha na ana wivu wa chama chake kupoteza muelekeo na nafasi yake kuchukuliwa na CDM. Ila wakumbuke wananchi ndio waamuzi na wanajua chama gani makini kwa sasa. Kujiunga na ccm ktk serikali na kuwa kitu kimoja Bungeni.

Naloli! Naloli! Shida ni kuwa Prof Lipumba siye anayeongoza chama. CUF inaongozwa kutoka Zenji. Wasemacho wenye nacho, ndo asema na ndo afanya ati. Mbele ya Hamad Rashid hawezi kusema lolote.
Jana kuna mtu alirusha hotuba ya Hamad huku JF kwenye. Niliisikiliza nikachoka kabisa. Anasema yeye aliichukia CCM kutoka alipoachishwa unaibu waziri wa fedha. Nani alimwambia alipewa cheo hicho milele yote. Hapo ndo nilipojua ajenda ya CUF ni kutafuta maslahi yao binafsi tu. Chama chake kilipokosa asilimia ya kumwezesha kuwa Kiongozi wa upinzani akaja kwa mlango wa nyuma. Iliposhindikana akatengeneza ajenda ya kuwatibulia CDM.
Yetu macho na masikio. Mpaka 2015 tutakuwa tumeona pumba nyingi na kusikia kelele za kutosha za madebe tupu.
 
Back
Top Bottom