Lipi bora, kujua au kutojua?

Lipi bora, kujua au kutojua?

Khantwe

JF-Expert Member
Joined
Dec 20, 2012
Posts
59,468
Reaction score
119,622
Habari zenu.
Swali hili linawalenga wanawake wenzangu waliopo kwenye ndoa na wale wanaotarajia kuingia huko.

Kwanza nianze kwa kusema hivi kwa imani yangu mimi, ukishaingia kwenye ndoa hutoki mpaka kifo kimkute mmoja wenu hata kwa wale wenzetu ambao talaka inaruhusiwa sidhani kama wanafurahia kuvunjika kwa ndoa.

Tumaini na furaha ya mwanandoa yeyote ni kuona ndoa yake inadumu na kustawi siku hadi siku, kuvunjika kwa ndoa si jambo la kufurahisha.

Kwa maana hiyo ni wajibu wa kila mwanandoa kuilinda ndoa yake isivunjike kwa kuvumilia mapungufu,makosa na vikwazo vinavyoibuka kwenye maisha ya ndoa.

Back to the topic.

Kuna tabia hii ambayo wanaume wanayo ya kuchepuka, najua wapo wanawake wanaochepuka lakini kwa hapa niko upande mmoja.

Let's say unaishi na mumeo, wewe hujaona dalili zozote za kuchepuka, yaani anawahi kurudi, matunzo anatoa, haki zako zote unapata pasipo longolongo kuna ulazima wowote wa kujua kwamba anachepuka na anachepuka na nani?

Ikitokea nimemshuhudia mumeo anaingia kabisa na mwanamke gesti au huwa namuona anaingia nyumba fulani kwa siri na inasemekana amemjengea hawara hiyo nyumba natakiwa nikwambie au nipige kimya?

Nikiuambia utapata faida /hasara gani wewe kama mke?

Na nikipiga kimya utapata faida/hasara gani?

Nimeamua niulize hivi maana mara nyingi kumetokea mabishano kuhusu hili wapo watu wanaoona raha kuletewa habari za waume zao, na ikitokea wamegundua kuwa wewe ulikuwa na taarifa za uchepukaji wa wanaume wao na hujawaambia kama ni rafiki utaitwa mnafiki.

Pia wapo wale ambao hawapendi kusikiliza habari za kuwahusu waume zao as long as macho yake yanaona mambo yako sawa kwa hiyo anaassume yako sawa even behind their backs?

Ni lipi bora? Mtazamo wako please
 
...aaah, Khantwe mie nikimuona shemeji anafanya ngono zembe, ntapiga kimya kama sijui kinachoendelea...!
...Na mimi ukinionea huko, jaribu tu kunyamaza, sitaki kujua..!!
 
Last edited by a moderator:
Sitaki kijua anachepuka au la halaf hata nimshuhudie mume wa mwenzangu anachepuka domo langu kulifungua nop
 
...aaah, Khantwe mie nikimuona shemeji anafanya ngono zembe, ntapiga kimya kama sijui kinachoendelea...!
...Na mimi ukinionea huko, jaribu tu kunyamaza, sitaki kujua..!!

Teh teh subiri ulee watoto wa wenzio ndo utie akili lol
 
Last edited by a moderator:
Sitaki kijua anachepuka au la halaf hata nimshuhudie mume wa mwenzangu anachepuka domo langu kulifungua nop

Hahaaa siku mwanaume akihamia jirani na kwangu napishana nae koridoni kama simjui atii
 
Habari zenu.....
Swali hili linawalenga wanawake wenzangu waliopo kwenye ndoa na wale
wanaotarajia kuingia huko.....
Kwanza nianze kwa kusema hivi......Kwa imani yangu mimi,ukishaingia
kwenye ndoa hutoki mpaka kifo kimkute mmoja wenu....hata kwa wale
wenzetu ambao talaka inaruhusiwa.....sidhani kama wanafurahia kuvunjika
kwa ndoa....tumaini na furaha ya mwanandoa yeyote ni kuona ndoa yake
inadumu na kustawi siku hadi siku...kuvunjika kwa ndoa si jambo la
kufurahisha. Kwa maana hiyo ni wajibu wa kila mwanandoa kuilinda ndoa
yake isivunjike kwa kuvumilia mapungufu,makosa na vikwazo vinavyoibuka
kwenye maisha ya ndoa.

Back to the topic...
Kuna tabia hii ambayo wanaume wanayo...ya kuchepuka,najua wapo wanawake
wanaochepuka lakini kwa hapa niko upande mmoja.
Let's say unaishi na mumeo.wewe hujaona dalili zozote za kuchepuka,yani
anawahi kurudi, matunzo anatoa,haki zako zote unapata pasipo
longolongo....kuna ulazima wowote wa kujua kwamba anachepuka na
anachepuka na nani??... Ikitokea nimemshuhudia mumeo anaingia kabisa na
mwanamke gesti au huwa namuona anaingia nyumba fulani kwa siri na
inasemekana amemjengea hawara hiyo nyumba....natakiwa nikwambie au
nipige kimya?
Nikiuambia utapata faida /hasara gani wewe kama mke?
Na nikipiga kimya utapata faida/hasara gani?
Nimeamua niulize hivi maana mara nyingi kumetokea mabishano kuhusu
hili....wapo watu wanaoona raha kuletewa habari za waume zao,na ikitokea
wamegundua kuwa wewe ulikuwa na taarifa za uchepukaji wa wanaume wao na
hujawaambia kama ni rafiki utaitwa mnafiki. Pia wapo wale ambao
hawapendi kusikiliza habari za kuwahusu waume zao...as long as macho
yake yanaona mambo yako sawa kwa hiyo anaassume yako sawa even behind
their backs?
Ni lipi bora? Mtazamo wako pliiz....

mkuu haina haja ya kusema ili iweje sasa? sijui kamjengea nyumba sijui gar sijui kiwanja! pilipili usizokula za kuwashia nn? bora piga kimua,
 
mkuu haina haja ya kusema ili iweje sasa? sijui kamjengea nyumba sijui gar sijui kiwanja! pilipili usizokula za kuwashia nn? bora piga kimua,

Eeeh....haya ngoja nitulie
 
Teh teh subiri ulee watoto wa wenzio ndo utie akili lol

Nitalea tu wala sio shida...!
Sitaki kuanza kufikiri jinsi jamaa linavyoanza kuchojoa nguo zake..aaah!
 
Teh teh subiri ulee watoto wa wenzio ndo utie akili lol

tahadhari kabla ya hatari....usivamie vamie tu thamini moyo wako sio unakabidhi kichaa angalia mtu anayefaa kwa ajiri ya afya na ustawi wa maisha yako....kwa experience hizi habari za watoto wako na wamwenzako huwa zinaleta malumbano sana ktk familia
 
tahadhari kabla ya hatari....usivamie vamie tu thamini moyo wako sio unakabidhi kichaa angalia mtu anayefaa kwa ajiri ya afya na ustawi wa maisha yako....

Vichaa wana alama usoni??? My dia haya mambo magumu acha tu...utakutana na Eli79 hapa (ni mfano tu) utasema mwanaume si ndo huyu...??!!! Subiri siku ujue mambo yako utajutraaa kumfahamu
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom