Zitto
Former MP Kigoma Urban
- Mar 2, 2007
- 1,562
- 10,890
Lindi yaweza kuwa Sri Lanka ya Tanzania|Zitto Kabwe, Mb
Siku hizi napenda sanakujua historia za nchi katika kupambana na umasikini wa watu wao. Lengo nikuelewa juhudi za nchi mbalimbali katika kuleta maendeleo ya watu na kujifunzapale ambapo nchi zimefanikiwa. Ukitembea mitaa ya Jiji la Colombo unaona mjimzuri msafi uliopangwa vema na kila mtu anaonekana kushughulika. Njia nzuri yakujua ukweli wa maisha ya watu ni kuongea na watu wenyewe. Mara nyingi hutumiamadereva wa taxi au Bajaji kwa jiji kama la Colombo. Katika mazungumzo nabaadhi ya madereva wa Bajaji nilizokuwa natumia pale Colombo niliona mwelekeommoja wa. Kwamba katika kipindi cha miaka 10 iliyopita maisha yao yamebadilikasana. Wakisifia kuisha kwa vita dhidi ya Tamil Tigers na kuongezeka kwa mapatoyao kwa watu kutumia zaidi usafiri. Dereva wa Bajaji wa Jiji la Colomboanaingiza wastani wa rupia 4000 (shilingi45,000) kwa siku. Nikataka kujua nini kimepelekea mabadiliko haya ya kipatoambacho mpaka wenye Bajaji wanafaidika nayo. Takwimu zao zinaeleza mengi sana.Serikali iliamua kupambana na umasikini na hasa umasikini wa vijijini.
Mwaka 2002 asilimia 22.7ya wananchi wote wa Sri Lanka walikuwa wanaishi chini ya mstari wa umasikini.Ilipofika mwaka 2011 kiwango cha umasikini kilikuwa asilimia 6 tu. Umasikiniulishuka kwa kiwango kikubwa katika maeneo ya vijijini. Katika kipindi chamiaka mitatu kati ya mwaka 2007 mpaka 2010 umasikini wa wananchi wa Sri Lankawalio kwenye sekta ya Chai (Estate sector) ulishuka kutoka asilimia 32 yawaliokuwa wanaishi chini ya mstari wa umasikini mpaka asilimia 11.4 na wale wa vijijini nje ya sekta ya Chai umasikiniulishuka kutoka asilimia 24.7 mpaka asilimia 9.4 katika kipindi hicho. Nilipoulizazaidi kwa wanasiasa na viongozi wa Serikali nikaambiwa kuwa mabadiliko makubwayaliyotokea miaka ya karibuni yalitokana na Serikali kufanya maamuzi mahususiya kuelekeza fedha nyingi zilizokuwa zinakwenda vitani kwenye uwekezajivijijini. Wanasema walitumia fedha nyingi kwenye ruzuku ya mbolea kwa wakulima,kusambaza umeme vijijini na kujenga barabara za vijijini. Siku niliyofikaniliona kwenye moja ya magazeti yao lakila siku Rais wao akizindua Mtambo wa kuzalisha umeme katika mji waTrincomalee uliopo Mashariki ya nchi hiyo.
Nikajiuliza mbona na sisitunatekeleza MKUKUTA na tunasema kwamba tunawekeza fedha nyingi sana vijijini?Mbona na sisi tunatoa ruzuku ya Mbolea yenye thamani ya zaidi ya shilingibilioni 60 kwa mwaka? Inakuwaje wenzetu wafanikiwe sisi tusifanikiwe? Tanzaniaimeanza kutoa mbolea ya ruzuku katika msimu wa mwaka 2006/2007 kama ilivyo kwaSri Lanka. Wenzetu katika miaka 3 kiwango cha umasikini kimepungua kwa asilimia15 kwa wananchi walio katika sekta hiyo ya Kilimo na wanaoishi vijijini. Sisikatika kipindi cha muongo mmoja, 2001 mpaka 2011, umasikini umepungua kwaasilimia mbili tu. Moja ya sababu ya sisi kushindwa ni kwamba mfumo wa mboleaya ruzuku umegubikwa na ufisadi wa hali ya juu sana. Mfumo huu umedhihirishanamna ambavyo kazi ya kupambana na Ufisadi ni ya kimfumo zaidi maana kwa namnaviongozi wa vijiji wanavyoiba mbolea ya ruzuku unaweza kiurahisi kabisa kusemarushwa ni sehemu ya utamaduni wa Mtanzania. Siamini hivyo. Ninaamini kwambamfumo wetu unazalisha wala rushwa, walafi na watawala wenye tamaa nawasiotosheka kama nilivyoeleza katika makala zangu zilizotangulia. Je tukiondoaufisadi wa mbolea ya ruzuku tunaweza kupata mafanikio ambayo wenzetu wameyapata?Sina jibu wala jawabu la swali hili. Hata hivyo ninaamini kwamba kutofanikiwakwetu ni zaidi ya ufisadi. Ni kutofanya kazi kwa bidii? Ni kukosa umakini? Nikutofurahia mafanikio? Ni kukosa uongozi thabiti unaoweza kusimamia mchakato wamaendeleo kuanzia ngazi ya kijiji mpaka Taifa?
Hebu tutazame pamojatakwimu hizi. Sri Lanka ina ukubwa wa kilometa za mraba 65,000. Mkoa wa Lindiuna ukubwa wa kilometa za mraba 66,000. Sri Lanka ina Pato la Taifa la dola zakimarekani 60 bilioni mwaka 2011, Tanzania Pato lake la Taifa ni dola zakimarekani 24 bilioni. Sri Lanka ina jumla ya watu milioni 20, Tanzania inajumla ya watu milioni 45, Mkoa wa Lindi una jumla ya watu 750,000 hivi. SriLanka na Tanzania zote zina Bajeti ya dola za kimarekani bilioni Tisa hivi.Uchumi wa Sri Lanka unategemea sana zao la Chai na Utalii kwa fedha za kigeni.Mkoa wa Lindi una eneo kubwa zaidi la Kilimo kuliko Sri Lanka nzima hasaukizingatia katika hekta 5.2m zinazofaa kwa Kilimo ni hekta 500,000 tu ndiozinalimwa. Zao la Korosho laweza kuwa Chai ya Lindi. Kilometa za mraba 18,000za mkoa wa Lindi ni Selous Game Reserve, Kilwa ni kivutio tosha cha utalii wakila namna na Mkoa wa Lindi una fukwe ambazo hazijawahi kuguswa toka duniaiundwe na mola.
Sri Lanka hawana GesiAsilia. Lindi na hasa Wilaya ya Kilwa ndio mzalishaji mkubwa wa Gesi asiliahapa nchini. Pia sehemu kubwa ya Gesi iliyogunduliwa hapa nchini ipo katikamkoa wa Lindi inagwa wengi wetu hudhani kwamba ipo mkoa wa Mtwara. Lakini Lindina Mtwara sawa tu. Mtwara ina kilometa za mraba 16,000 (chini ya eneo la Lindilililopo Selous). Tufanye Lindi na Mtwara kwa pamoja ndio Sri Lanka yaTanzania. Tunaweza kujenga uchumi wa dola za kimarekani bilioni 60 kwa Lindi naMtwara? Tunaweza kufanya mikoa hii iwe na kiwango cha umasikini chini yaasilimia 3 ya wananchi wake? Tunaweza kuingiza watalii 800,000 kwa mwaka kwamikoa hii tu? Tunaweza kuuza nje Korosho yenye thamani ya dola za kimarekaniangalau 600 milioni? Tunaweza kutumia sehemu ya Mapato yatokanayo na Gesi asilikujenga miundombinu ya barabara, umeme, reli na maji kwenye wilaya zote za hiiSri Lanka yetu? Tunaweza kuwekeza kwenye Elimu kuhakikisha kila motto anapataelimu bora? Tunaweza kuhakikisha kuwa asilimia 97 ya wakazi hii Sri Lanka yetuwanapata huduma za Afya?
Majibu ya maswali yotehaya ni NDIO. Utashi. Utayari. Uthubutu. Hebu tuthubutu kuiweka Sri LankaTanzania. Lindi na Mtwara ni zaidi ya Sri Lanka. Nikipata fursa ya kuandikatena nitaandika kuhusu uwekezaji kwenye Elimu nchini Sri Lanka na kwamba Hakiya kupata Elimu mpaka Chuo Kikuu ni haki ya kikatiba yenye kuweza kudaiwamahakamani.