Limbwata huuwa na kuvunja ndoa

UMASIKINI BWANA

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2013
Posts
942
Reaction score
567
Hbr JF.

Mwaka jana nilikuwa kwenye mazishi ya rafiki yangu alikufa ghafla, minong'ono msibani ikawa kuwa amelishwa limbwata na mkewe.

Mke alivyo hojiwa akasema alienda kwa mganga kupewa dawa apendwe, kwa kuwa alifanya hivyo tangu zamani kila dawa inapopungua nguvu anagombana sana na mumewe.

Mpaka kutengana akimpa dawa wanarudiana kamuua mwenzie

Sasa wadau mnalisemeaje hili?
 
Unyenyekevu na utiifu kwa mwanamke ni limbwata tosha kabisa hayo mengine nikuumizana tu
 
Bila Shaka alimpa limbwata la radi, mume alipoingia bafuni kuoga, mamba mkubwa akatoka kwenye beseni Na radi ikatokea kwenye maji yaliyo sambaa sakafuni Na kumpiga marehemu
 
Limbwata kutoka Ifakala-Moro....yaani siyo tu zuzu, unakuwa mwehu kabisa..
 
Hakuna kitu kinachoitwa Limbwata.., hiyo ni aina ya Utapeli unaofanywa na hao wanaojiita Waganga ili kuhalalisha malipo atakayopata toka kwa Wateja wake, ila kimsingi Mwanaume kuwa Zuzu hadi kufikia kutumikishwa na Mke ni Maisha aliyojiamulia Mwenyewe kwa kuruhusu akili, Utashi na Maamuzi yafanywe na Mke wake kwa niaba yake!!!
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…