Waliokujibu hawako sahihi. KWANZA LIKIZO YA UZAZI INA PISHANA KWA VIPINDI SI CHINI YA MIAKA MIWILI. ukizaa ndani ya miaka miwili mara mbili utapata likizo ya uzazi moja tu ile iliyotangulia.Nashukuru wanazuoni wa Sheria maana ofisi nyingine tunanyimwa haki ya likizo kwa kisingizio kuwa ati ukichukua likizo ya uzazi basi inafuta likizo yako ya kawaida. Sijui ni umbumbumbu wa sheria au ni ukandamizaji? jamani ni kweli tutafika?
Wana JF mliobobea katika sheria za kazi. Hivi nikichukua likizo ya uzazi ya siku 84 sitakuwa na haki ya kuchukua likizo yangu ya mwaka ya siku 28? nisaidieni
Waliokujibu hawako sahihi. KWANZA LIKIZO YA UZAZI INA PISHANA KWA VIPINDI SI CHINI YA MIAKA MIWILI. ukizaa ndani ya miaka miwili mara mbili utapata likizo ya uzazi moja tu ile iliyotangulia.
ukipata likizo ya uzazi mwaka 2011, mwaka unaofuata kama ulichukua likizo ya kawaida mwaka 2011 hutopata likizo ya kawaida(annual leave) kwa mwaka 2012.
kwa maelezo uliyotoa yaani siku 56 plus 28 inaleta jumla siku 84. Maana yake ni kuwa na likizo ya mwaka huo inahesabiwa. Endapo ulikuwa umeshachukua siku 28 kabla ndani ya mwaka huo inamaanisha utakuwa umechukua likizo ya mwaka mara mbili. Hivyo, mwaka utakaofuata hutopata likizo kwa kuwa ulishachukua siku 28 zilizoleta jumla ya siku 84.Samahani weka majibu yako katika maelezo mepesi, sijapata kitu kabisa hapo.
Ulikusudia kueleza nini?
Ninavyoelewa mimi likizo ya uzazi ni siku 56 plus siku 28 za likizo ya mwaka husika na inatolewa mara moja katika mzunguko wa miaka mitatu.
kwa maelezo uliyotoa yaani siku 56 plus 28 inaleta jumla siku 84. Maana yake ni kuwa na likizo ya mwaka huo inahesabiwa. Endapo ulikuwa umeshachukua siku 28 kabla ndani ya mwaka huo inamaanisha utakuwa umechukua likizo ya mwaka mara mbili. Hivyo, mwaka utakaofuata hutopata likizo kwa kuwa ulishachukua siku 28 zilizoleta jumla ya siku 84.