kama ni uongo wewe tumia dawa zako za Ma-hospitalini nani kakukataza kutumia hizo dawa za hospitalini? Tuache sisi tunao tumia Dawa zetu za Nature za Mitishamba wewe katumie sumu zenu za Hospitalini.cc broski
Wapi nilisema bora utumie dawa za hospitali? Labda hujasoma vizuri nilichoandika.
Mimi sipendi kutumia dawa, naamini ni bora uongeze nguvu ya mwili ili usiumwe kuliko kuumwa na kuhitaji kumeza dawa. Ndo maana hata mimi natumia vitamins.
Nilichoandika ni kwamba hata dawa za mitishamba zinazo side effects. Na pia vitamins zenyewe zinazo side effects ukimeza ovyo.
Hoja yangu ni kuwaambia usifikiri kuna dawa yoyote - ya kawaida au ya mitishamba - ambayo haina side effects. Hata kama dawa za mitishamba ni bora kuliko dawa za kawaida, bado zinazo side effects. Kwa hiyo usiwadanganye wateja wako.