Swali, je makampuni yanayonunua madeni ya serikali yanapata manufaa gani?
Mimi nielewavyo ktk nchi zilizoendelea kuna makampuni kazi yake kununua madeni sugu kwa bei pungufu kutoka kwa mdai na kisha kampuni nunuzi ya madeni kuchukua mzigo wa kuhakikisha inalipwa pesa zote toka kwa mdaiwa ( hapa Mohammed Enterprise na kina-MMN watailipa Libya pesa pungufu halafu kuikomalia serikali ya Tanzania ilipe deni lote).
Sasa basi kama ndivyo ilivyo, je serikali ya Tanzania ina uwezo wa kuilipa Moh'd ent. au MMN kiasi gani na serikali ya Tanzania itapata unafuu gani kudaiwa na Moh'd Ent/ MMN deni hili litakalouziwa na serikali ya Libya kwa makampuni ya ki-Tanzania? Je serikali ya Tanzania italipa hawa watarajiwa wa ununuzi wa deni kwa pesa za Shillingi za Tanzania au kwa pesa za kigeni? au watapewa migodi au madini n.k kama malipo ya deni hili lililoshindikana? Jambo hili linahitaji kufafanuliwa kwa undani jinsi Moh'd ent au MMN watakavyolipwa na serikali hii iliyofilisika ya Tanzania na walipa kodi watabebeshwa zigo gani?.
Inaonekana kuna watu humu ndani wamelipwa kupotosha ukweli wa kilicholetwa kama taarifa. Suala hapa ni kesi iliyokuwa mahakamani inayohusu fedha za Libya ambazo Serikali ya Tanzania ilikopa mafuta miaka ya themanini. Suala la misikiti linatoka wapi
Baada ya kumalizika kwa kesi hii, sasa akina Mohamed Dewji wasubiri kesi ya jinai kwa kujipatia fedha za Serikali kwa njia ya udanganyifu
Misikiti ya Iran na Saud Arabia yana Masharti Makali
Mohamed Dewji hakujua kuwa anaingizwa ktk matatizo baada ya kupotosha ukweli kuhusu deni la Libya. Nasubiri kuona gazeti la Mtanzania litasema nini baada ya kuumbuliwa kwa MeTL leo mahakamani. Nasubiri kuona pia wataandika nini baada ya siku chache zijazo pale tutakaposhuhudia dola ikichukua mkondo wake kwa kuwapeleka mahakamani wezi hawa
Nadhani unahitaji darasa la Debt Swap maana inaonekana ni concept mpya kabisa kwako. Lakini ukweli ni kwamba kununua deni kunakupa hela ambazo riba yake ni ndogo kuliko ukikopa benki maana inerest ya benki wakati mwingine hufikia hata 25% wakati hili linaweza kuwa 8% tu. Hii inahitaji kampuni inayonunua kuwekeza katika miradi iliyochaguliwa hapa nchini kama vile viwanda au kilimo kwa nia ya kuongeza ajira na uuzaji bidhaa nje.
Mbopo,
Ni kweli nahitaji ufahamu wa 'Debt Swap' ktk sakata la hili deni la Taifa la Tanzania kugombaniwa kati ya Moh'd Ent na MMN.
Je wanunuaji hawa(Metl au MMN) wa deni la mamilioni ya dolari za Kimarekani deni la taifa la Tanzania watalipwa nini, maana umenijibu kijumla-jumla hujafafanua kwa 'mifano' mingine (ambayo kesi haziko mahakamani wanafaidika vipi).
Serikali ya Tanzania ni muflisi je watatoa government bonds/treasury bonds au watagawiwa viwanda/migodi/majengo kama fidia ya 'debt swap'?
Kumbuka JamiiForums si mimi na wewe tu, bali hata jamii nzima ya ki-Tanzania inapaswa kuelewa kiundani hii kitu Mr. Mbopo unayoiita 'Debt Swap' kwani unanipa matumaini unajua kiundani lakini unatoa jibu la kimkato-mkato.
Mbopo tupe dozi tuelewe kwa undani mikataba ya 'debt swap' katika hili la serikali ya Tanzania na makampuni ya kitanzania (Metl /MMN), vipi serikali tajiri ya Libya imeamua kuuza deni kwa thamani ya chini kwa Metl/MMN na vipi serikali masikini kama ya Tanzania inawezaje kuilipa Metl/ MMN deni lote ili Metl /MMN waibuke na faida kibiashara?
Mfano Metl ina visheni ya kufikia USD One Billion group company by 2015 ''A visionary organization, the MeTL Group continues to pave the path to industrial development in Tanzania, by continually striving for excellence and ethically sound growth. Today we contribute two and a half percent of the GDP of the country and aim to be a USD one billion Group by 2015.'' source Company Profile | METL - Mohammed Enterprize Tanzania Ltd je EPA ya USD 100 million debt swap kuilipa Libya Metl wanayo au watakopa toka mabenki ya ndani ya nchi (Tanzania) na kama ni hivyo kwa nini mabenki ya Kitanzania hawataki hizo treasury bonds/miradi n.k
Mzee haigharimu kitu kwa kukaa kimya kama hujui kitu. Infact ungeheshimiwa sana! Sasa tunashuku uwezo wako wa kukusanya taarifa zenye usahihi.
nashukuru sana kwa kutuweka sawa.kweli ushabiki wakati mwingine ni upofuunajua ndugu yangu humu kuna watu wenye nia ya kuongeza idadi ya post zao bila kujali kile wanachochangia kina mchango gani kwa taifa au jamii. Halafu hili tatizo la udini linaelekea kuwatia upofu watu kiasi cha kushindwa kufanya tathmini ya mambo kwa macho mawili. Katika historia ya nchi hii serikali haijawahi kukopa kulipia masuala ya kiimani, lakini kwa bahati mbaya kwa sababu watu walidhani ni deni lilitokana na uongozi wa rais wanayemchukia kwa sababu zao basi wakadhani huu ni wakati wa kumtia 'hatiani' kumbe maskini ni deni linaloihusu awamu inayoheshimika sana, tena kwa masuala ya kimaendeleo kwa nchi yetu! What a shame for these irresponsible people.
Tatizo ni Mikopo gani tunaipata toka kwa Libya; the nation supposed to be our Enemy? Why should we embraced them? Sisi Nyumba zetu zilibomolewa na Ndege za Walibya Serikali haikuwa na pesa za kusaidia kujenga nyumba zetu; tuliishi kwa tabu sasa tunasikia huyu Mlibya anaidai serikali pesa...
unajua sometime nikifikiria mambo ya nchi yangu inavyochezewa!natamani viongozi wotee wa chama waje hapo niwaulize maswali huku nikiwalamba makofi vibaya sana.
basi usishangae huyu tapeli wa METL akavutwa pembeni akafundishwa jinsi ya kupiga hilo dili ukashangaa kampuni hii ikalipwa hayo mapesa kwa mkono wa nyuma.kwa bongo ya mkwe re yote yanawezekana