Hawa ndugu zetu wa kaskazini wana tatizo la kutojua namna ya kula na kipofu. Juzi juzi kupitia channel ten amesikika mmoja wa wanasheria kutoka kwa huyu mama somebody Mkindi, alichokuwa anaeleza ni kama kwamba haki za binadamu means haki za cdm. Yeye ni mwanasheria lakini alichokuwa akisisitiza juu ya naibu spika ni kwamba tulia anatakiwa atumie hekima binafsi badala ya sheria kwa sababu inaonekana matumizi ya sheria hayawezi kuleta harmony bungeni. Sikushangaa kwa sababu Mkindi anavyoonekana na kuongea ni lazima atakuwa kutoka kaskazini na bahati mbaya hawa jamaa zetu bado hawajaamini kama uchaguzi uliisha na kwa vyovyote vile kama kuna uhai rais ni JPM kwa miaka minne ijayo mbeleni.LHRC kwa sasa ndiyo NGO pekee inayosaidia wanyonge kwenye mswala ya kisheria. Ukitaka ushahidi tembelea vituo vyao makao makuu na mikoani uone watu wanavyotetewa bure kuanzia kwa waajiri waonevu, kesi za kubambikiwa za jinai, wajane wanaodhulumiwa mirathi, kesi dhidi vyombo vya dola vinavyonyanyasa wananchi n.k. kwenye siasa ni lazima wapige kelele iwapo demokrasia inapuuzwa. Ulitaka wafanye nini zaidi? CCM kubalini kukosolewa kwani nchi hii ni yetu wote na hata inawezekana wengi wanaotetewa na shirika hili wengi ni wanachama wenu.