Leonardo Da-Vinci

 
 
ni jukumu lako kunielimisha..usiponielimisha unatenda dhambi kwa kutotimiza ajibu

nimekutoa hofu kila ulichopost huku jf amini ipo siku utaujua ukweli, ushauri wangu bure kabisa tumia muda Wako mchache unaoishi hapa duniani kufanya mambo sahihi,
 
 
​monalisa

picha hiyo ya monalisa imekuwa maarufu sana kwa sababu inasadikika kuwa ilichorwa kwa ustadi mkubwa sana, mchoraji alitumia vipimo vya kipekee kwa wakati huo hakukuwa na mwingine aliyeweza namna hiyo, ukiiangalia kwa pande mbalimbali kuna vitu kitaalamu mchoraji alivitumia katika uchoraji wake huu na kusababisha kuwa gumzo, lakini pia kilichosababisha kingine kuwa gumzo ni nani haswa alikuwa amechorwa katika picha ile.

ukitaka kujua mengi juu ya picha ya monalisa na mkasa mzima unaweza ingia mtandaoni na kupata taarifa nyingi ukishachuja utakuwa umepata kitu.

kuna siku bbc walikuwa wanaonesha watu waliojaribu kuchora picha kama ya monalisa lakini vituko vilivyotoka hapo vilithibitisha kuwa picha ya monalisa ilichorwa kwa ustadi mkubwa sana.
 
muthe_x;

leonardo da vinci ni moja ya wanasayansi waliojaribu kufanya kila aina ya ubunifu . Aliweza fanya ubunifu wa mwanzo kabisa wa baroon, aliweza kubuni aina ya mwanzo kabisa ya kifaru [kifaa cha vita] na vingine vingi…lakini pia alikua na kipaji cha ajabu cha uchoraji mfano picha maarufu ya monarisa.
Lakini kitu kilicho amsha umakini juu ya mtu huyu ni suala lake la kudai ya kuwa yesu kristu alimuoa marry Magdalena na alikua na watoto wawili ambao kizazi chao kipo huko ulaya..kwa ufupi ni hayo tu


Leonardo Da Vinci hajawahi kusema kwamba Yesu alimuoa Mary Magdalene. Watu wanatafsiri hivyo kutokana na painting yake iitwayo "The last Supper" inayoonyesha Yesu na wanafunzi wake wakila karamu ya mwisho ambapo mtu ambaye yuko karibu kabisa na Yesu ni mwanamke.
 
 

Hapa ndipo wanaJF tunatakiwa tusome zaidi na kuelewa sana.Kuna Conspiracy Theories nyingi sana ambazo zinaendeshwa na watu mbali mbali kuhusiana na vitu vingi tu hasa hasa masuala ya imani.Wachangiaji wote wa uzi huu wameelezea kuhusiana na Leonardo Da Vinci lakini hawajaelezea kisa kilichosababisha watu Fulani Fulani wazushe ya kuwa Yesu Kristo alikuwa na mke na alizaa.Leonardo Da Vinci alikuwa mwanasayansi mzuri aliyefanya ubunifu wa vitu vilivyokuja kuboreshwa na wanasayansi wa zama zetu.Mbali na kubuni vitu kama vifaru vya kivita vilivyoboreshwa kipindi cha vita kuu ya I ya dunia alikuwa mchoraji mzuri.Usanii wake aliufanya Italia kwenye makanisa ya RC na hasa kwa katika makazi ya papa na majengo mbali mbali.Alichora michoro mingi na mingine alikufa bila kuimaliza na wasaidizi wake na watu waliokuwa karibu waliimalizia.Michoro maarufu zaidi ni The Last Supper,Monalisa na ule unaoonesha watu kadhaa wasio na nguo wamesimama .

Ili kujua zaidi kuhusu uzushi huu inabidi umjue DAN BROWN mtunzi wa vitabu kadhaa ambavyo kiubunifu anaibua madai kuwa Yesu alimuoa Maria Magdalena na wakazaa watoto.Kitabu hicho kinaitwa THE DA VINCI CODE
ambacho pia kimetengenezewa filamu iliyoigizwa na mhusika mkuu ni Tom Hanks.Vitabu vyake vingine ni DIGITAL FORTRESS,DECEPTION POINT,INFERNO,THE LOST SYMBOL na ANGELS AND DEMONS. Unaweza kutembelea hapa nilipogoogle The Da Vinci Code - Dan Brown - Google Books

Vitabu vyote hivi ni Fiction ambayo maana yake kwa mujibu wa Concise Oxford English Dictionary toleo la 11 maana yake ni Prose literature,especially novels describing imaginary events or people,a thing that is invented or untrue na a false belief or statement,accepted as true because it is expedient to do so.Maana ya neno expedient inamaanisha convenient and practical although possibly improper or immoral.
Ni kweli kuna vitabu ambavyo vilikataliwa na watheologia wa madhehebu ya kiprotestanti walivikataa kuingia katika Biblia sababu ikiwa zilikuwa ni hadithi ambazo waliona havifai kuwa neno la Mungu.Vinaitwa vitabu vya APOKRIFA mfano Hekima ya Yoshua Bin Sira,Beli na Joka,Wamakabayo nimetajaavichache.
Kwa kumalizia Leonardo Da Vinci alichora picha na alibuni vitu vizuri ambavyo leo wajuzi wasioamini na wenye malengo tofauti wanatumia sanaa zake kuwapotosha wengi.Si kweli Yesu alimuoa Maria Magdalena na walipata watoto.
Nakaribisha mawazo mbadala na uchangiaji mpana zaidi kuhusu mada hii
 
Hpo ndipo mtu mwenye akili timamu ataanzia kuutafuta ukweli

Kuna vita inaendelea ndugu yangu ya kumpaka matope huyu aliyebadilisha historia ya dunia!

Alipakwa matope,kudhalilishwa na kuuwawa msalabani na hapo ndipo hiyo vita iliposhindwa mkuu maana baada ya siku tatu alifufuka akayashinda mauti,akashinda vita vyote dhidi yake,dhidi ya ubinadamu alishinda yeye ana alitushindia sisi hamna vita inayoweza mshinda tena yeye wala wafuasi wake usiwe na hofu kaa kwa amani mkuu
 

Naona umeanza kwa kujadili vizuri, lakini umemalizia kwa kufunga mjadala badala ya kuuacha wazi. Kwa nini unasema kuwa si kweli yesu alimuoa Mary Magdalene? Ni kwa sababu tu haikuandikwa hivyo kwenye biblia au una sababu nyingine ya kusema hivyo?
 
Naona umeanza kwa kujadili vizuri, lakini umemalizia kwa kufunga mjadala badala ya kuuacha wazi. Kwa nini unasema kuwa si kweli yesu alimuoa Mary Magdalene? Ni kwa sababu tu haikuandikwa hivyo kwenye biblia au una sababu nyingine ya kusema hivyo?

Mkuu familia sio jambo la siri na wala haliwezi kufunikwa kirahisi kama unavyofikiria kwani hao watoto wa Yesu wasingependa kufahamika kama watoto wa Yesu? Nina mwenye uwezo wa kuifunika hii familia ya Yesu muda karne zote hizo kuna uwezekano Yesu alikuwa karibu na Magdalena lakini sio ukaribu wa kimahaba kama baadhi ya watu wanavyotaka kuwaaminisha watu na huo ukaribu ndio msingi wa huu uvumi wa kua Yesu alizaa na Magdalena
 

mkuu hebu tuambie kwa nini watu wamzushie.........kaka hao wanatheologia waliokataa vitabu coz ni simulizi ndio walionza kuijua siri na kuzificha...kama bible iliandikwa kwa uwezo wa roho mtakatifu...nani aliwapa mamlaka wanatheologia kutambua huyu alikuwa na upako na huyu hakuwa na upako waite maandishi yake ni simulizi......ndugu kumbuka mengi sana yamefichwa na utawala wa Roma..kiasi ambacho yakifumuka..unaweza kuona aibu kuitwa mkristu
 

mkuu huyo mwandishi DAN BROWN aliandika vitabu vyake vyote baada ya miaka mingi sana kupita tangu kufa kwa Leonardo Davinci ,kutokana na michoro ya davinc..hakuibua yeye taarifa hizo.....Leonardo alizikuta taarifa hizo......, usimuhukumu mwandishi...tuambie uzushi huo ulianza lini na kwa nini.....kwa nini wanatheologia wanawashambulia sana watu wanaoleta taarifa hizo..kwa nini wengine waliuwawa, kwa nini waliokuwa wanahoji kuhusu bible na ukristu kwa ujumla waliishi kwa tabu sana zama hizo?.........mkuu usichezeshe Lugha......tunajua fiction ni kitu cha Kubuni....lakini hii kitu ni Fact though is highly probable
 

Uko sahihi mkuu, vitabu vingi mno vimefichwa vyenye mambo makubwa. Hapa ukiwaambia watu kuwa Yesu aliwahi kuuwa alivyokuwa mtoto watasema abomination..lol!
 

Ni kweli familia si jambo la siri, lakini ukumbuke kipindi cha yesu mpaka kifo chake alikuwa "NO BODY" amekuja kupata umaarufu miaka mingi baada ya kifo chake. Kama watu mashuhuri wakina Kaizari koo zao zilifutika kitambo, ni kitu gani kinakufanya uamini kuwa ukoo wa yesu ungeprevail? Hata ukoo wa Yosefu babaake yesu ulishafutika with no single trace!
 

Mkuu naona kuna maswali mawili hapo ya Msingi kwenye comment yako moja ni kwanini watu Wamzushie? Pili ni kwanini vitabu vyote havikuingizwa kwenye biblia.Ntajaribu kukujibu kwa kadri ya uwezo wangu na kwa bahati nzuri comments zako zinaonyesha ni mtu unayeweza kuargue kwa facts na bila dharau/dhihaka kwa anayetofautiana mawazo na wewe
1. Kwanini wamzushie - Utakubaliana na mimi kuwa watu wasiokupenda au maadui zako wanaweza kufanya lolote kukuharibia kwa namna yoyote ile so sio kila mtu anaipenda imani ya Ukristo na hivyo watafanya kila hila ili kuonyesha Imani hiyo na muanzilishi wake hawana maana kuna maadui wengi sana wa ukristo na wameshafanya mengi sana kuonyesha kuwa ukristo na huyo Yesu mwenyewe havina maana na wapo waliodiriki hata kusema ya Kuwa Yesu hakuwahi kutokea duniani (Sasa sijui hata hiyo idea ya Yesu ilitoka wapi hawaelezi) wapo waliosema Yesu hakufa na kufufuka sasa kama wameweza kuzusha ya Kuwa hakuwahi kuja Duniani na baadae wakakurupuka tena wakajikana wakasema oooh ndio alikuwepo lakini hakufa wala kufufuka watashindwa nini kuzusha ya kuwa alitembea na kuzaa na Maria Magdalena? Mbona uzushi huu ni mdogo kuliko wa kutokuzaliwa/kuja duniani au ule wa kutokufa na kufufuka?

2. Kwanini vitabu vyote havikuweka kwenye biblia? Ndugu yangu vitabu vyote vya agano jipya viliandikwa baada ya Yesu kufufuka na kupaa mbinguni na vilianza kuandika takribani miaka hamsini baada ya Yesu kupaa mbinguni vitabu hivyo vilikuwa vinaelezea maisha ya Yesu,Maisha ya Mitume na Wakristo wa Kwanza na hivyo kupelekea watu wengi sana walio ona matukio hayo kuandika vitabu mbalimbali kwa mfano kuna vitabu vingi sana vilielezea maisha ya Yesu lakini ni vinne tu (Injili) ndivyo unavyovikuta kwenye biblia sababu ni kuwa Maisha ya Yesu yalikuwa na mambo mengi sana ya kuandikia na hata kwenye biblia imeandikwa (siukumbuki ule mstari ila nadhani ni Luka au Mathayo ) Kila kitu kuhusu Yesu kingewekwa kwenye maandishi basi ulimwengu mzima usingetosa kujaza hivyo vitabu offcourse akimaanisha ni vingi sana kumbuka kila siku ya Yesu hapa duniani ilitosha kuandikia kitabu kuna mambo mengi sana yaliandikwa mathali kuna injili ambayo ilielezea utoto wa Yesu jinsi alivyokuwa akicheza na wenzake alikuwa na uwezo wa kutengeneza ndege wa udongo akawapulizia pumzi na wakapeperuka,jinsi alivyokuwa anawasaidia watoto wenzake wasipigwe majumbani wakichelewa kurudi na offcourse jinsi alivyokuwa anawawajibisha watoto wenzie waliokuwa wanajifanya wababe na kumpiga sasa kanisa lililazimika kuchambua baadhi ya vitabu tu na kuviingiza kwenye biblia ili kuepuka kuwa na biblia ndefu sana inayoweza kufanya watu wakashindwa kuisoma kwa ukubwa wake na wakaamua kuweka vitabu vichache tu vyenye umuhimu na kutujenga kiroho.
Nadhani nimejaribu kidogo kukujibu mheshimiwa
 

Kwanini waliohoji kuhusu bible na Ukristo waliishi maisha ya tabu zama hizo? Hilo ni kosa ambalo kanisa lilitenda na linakiri kuwa lilikuwa ni kosa na ndio maana kanisa limeomba msamaha kwa kumuua Galileo Galilee aliyesema kuwa dunia ni duara na inazunguka jua tofauti na kanisa lilivyokuwa linaamini kuwa dunia ni kama meza na ukienda mbali sana unaweza poromoka huko ni zama za giza katika kanisa,Kanisa halikuwa tayari kubadilika kuendana na sayansi bila kuathiri Imani

"tunajua fiction ni kitu cha Kubuni....lakini hii kitu ni Fact though is highly probable" Come again sir mbona unajikanganya mwenyewe unakubali kuwa Dan Brown anaandika Fiction na unajua Fiction sion ukweli ni nini kinachokufanya uamini kuwa suala la Yesu kuoa ni Fact? Ingekuwa Fact kwanini asingeandika kwa mtindo mwingine na sio Fiction? Kwanini unataka kuigeuza Fiction kuwa Fact? Wewe unajua zaidi kuliko Dan Brown? Kwani yeye hakujua kuwa hizo ni facts na akaziweka katika mtindo wa facts na sio fiction? Kwanini unamlisha Maneno na kutengeneza lijikiwanda la uongo ili mradi tu uendane na unachotaka kuamini? (Inaonyesha unataka kuamini kuwa Yesu alitembea na kuzaa na Maria Magdalena - Sina uhakika!!) Acha Fiction iwe Fiction mkuu na Facts ziwe Facts
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…