Hapa ndipo wanaJF tunatakiwa tusome zaidi na kuelewa sana.Kuna Conspiracy Theories nyingi sana ambazo zinaendeshwa na watu mbali mbali kuhusiana na vitu vingi tu hasa hasa masuala ya imani.Wachangiaji wote wa uzi huu wameelezea kuhusiana na Leonardo Da Vinci lakini hawajaelezea kisa kilichosababisha watu Fulani Fulani wazushe ya kuwa Yesu Kristo alikuwa na mke na alizaa.Leonardo Da Vinci alikuwa mwanasayansi mzuri aliyefanya ubunifu wa vitu vilivyokuja kuboreshwa na wanasayansi wa zama zetu.Mbali na kubuni vitu kama vifaru vya kivita vilivyoboreshwa kipindi cha vita kuu ya I ya dunia alikuwa mchoraji mzuri.Usanii wake aliufanya Italia kwenye makanisa ya RC na hasa kwa katika makazi ya papa na majengo mbali mbali.Alichora michoro mingi na mingine alikufa bila kuimaliza na wasaidizi wake na watu waliokuwa karibu waliimalizia.Michoro maarufu zaidi ni The Last Supper,Monalisa na ule unaoonesha watu kadhaa wasio na nguo wamesimama .
Ili kujua zaidi kuhusu uzushi huu inabidi umjue DAN BROWN mtunzi wa vitabu kadhaa ambavyo kiubunifu anaibua madai kuwa Yesu alimuoa Maria Magdalena na wakazaa watoto.Kitabu hicho kinaitwa THE DA VINCI CODE
ambacho pia kimetengenezewa filamu iliyoigizwa na mhusika mkuu ni Tom Hanks.Vitabu vyake vingine ni DIGITAL FORTRESS,DECEPTION POINT,INFERNO,THE LOST SYMBOL na ANGELS AND DEMONS. Unaweza kutembelea hapa nilipogoogle
The Da Vinci Code - Dan Brown - Google Books
Vitabu vyote hivi ni Fiction ambayo maana yake kwa mujibu wa Concise Oxford English Dictionary toleo la 11 maana yake ni Prose literature,especially novels describing imaginary events or people,a thing that is invented or untrue na a false belief or statement,accepted as true because it is
expedient to do so.Maana ya neno expedient inamaanisha convenient and practical although possibly improper or immoral.
Ni kweli kuna vitabu ambavyo vilikataliwa na watheologia wa madhehebu ya kiprotestanti walivikataa kuingia katika Biblia sababu ikiwa zilikuwa ni hadithi ambazo waliona havifai kuwa neno la Mungu.Vinaitwa vitabu vya APOKRIFA mfano Hekima ya Yoshua Bin Sira,Beli na Joka,Wamakabayo nimetajaavichache.
Kwa kumalizia Leonardo Da Vinci alichora picha na alibuni vitu vizuri ambavyo leo wajuzi wasioamini na wenye malengo tofauti wanatumia sanaa zake kuwapotosha wengi.Si kweli Yesu alimuoa Maria Magdalena na walipata watoto.
Nakaribisha mawazo mbadala na uchangiaji mpana zaidi kuhusu mada hii