Kamgomoli
JF-Expert Member
- May 3, 2018
- 1,865
- 3,802
Swala la Simba na Yanga kubebwa na marefa ni kitu endelevu na haitatokea siku itaisha. Leo Simba wanawazomea Yanga kwa kupewa penati isiyo ya halali kesho hao hao Simba watafunga goli la offside ya wazi dhidi ya kitimu fulani.
Anayepinga aingie YouTube atapata majibu. Kuna ile mechi ya Yanga na Azam mpira ulitoka refa akaacha baadae likawa goli, vile vile mechi ya Prison na Simba Mbeya Kibu Denis akiwa offside aliurudisha ndani mpira uliokuwa umetoka na Mkude akafunga.Huu ndio ukweli wasiopenda kuusikia mashabiki wa hizi timu kongwe.
Kila mtu anaezaliwa nchi hii, eitha ni Simba au Yanga. Hata kama hafuatilii mpira ila kimoyomoyo kuna moja kati ya hizi timu itamvutia. Ndivyo ilivyo hata kwa marefa wetu nao wamechagua upande toka walipozaliwa.
Kama Rais wa TFF mwenyewe anashutumiwa kuipendelea moja ya hizi timu sembuse marefa? Thubutu! Simba na Yanga kubebwa na marefa ni mwendo wa kupokezana leo Doto, kesho Kulwa sema atakayekuwa vibaya kwenye hicho kipindi ndo atahisi mwenzake anahonga marefa.
Subirini kituko kingine kesho.
Anayepinga aingie YouTube atapata majibu. Kuna ile mechi ya Yanga na Azam mpira ulitoka refa akaacha baadae likawa goli, vile vile mechi ya Prison na Simba Mbeya Kibu Denis akiwa offside aliurudisha ndani mpira uliokuwa umetoka na Mkude akafunga.Huu ndio ukweli wasiopenda kuusikia mashabiki wa hizi timu kongwe.
Kila mtu anaezaliwa nchi hii, eitha ni Simba au Yanga. Hata kama hafuatilii mpira ila kimoyomoyo kuna moja kati ya hizi timu itamvutia. Ndivyo ilivyo hata kwa marefa wetu nao wamechagua upande toka walipozaliwa.
Kama Rais wa TFF mwenyewe anashutumiwa kuipendelea moja ya hizi timu sembuse marefa? Thubutu! Simba na Yanga kubebwa na marefa ni mwendo wa kupokezana leo Doto, kesho Kulwa sema atakayekuwa vibaya kwenye hicho kipindi ndo atahisi mwenzake anahonga marefa.
Subirini kituko kingine kesho.