Leo tena Yesu amenitendea muujiza mkubwa!

Leo tena Yesu amenitendea muujiza mkubwa!

20250814_055402.jpg
 
Kwa zaidi ya wiki moja nimekuwa nikihisi kana kwamba kuna mdudu anatambaa tambaa kwenye bega langu la kushoto. Nikipapasa sehemu hiyo sioni kitu. Leo nikasema "enough is enough"(yatosha sasa). Nikaweka mkono sehemu hiyo na kuikemea hali hiyo kwa Jina la Yesu. Hivi sasa hali ya mdudu kutambaa tambaa imetoweka kabisa katika eneo hilo! Hakika Yesu hajabadilika. Miujiza aliyoitenda miaka 2000+ iliyopita bado anaitenda hata leo kwa kila aaminiye.

Kisayansi, wenye dalili kama hizo, huambiwa kwamba wana "paresthesia." Wanapoenda hospitali, madaktari huwauliza maswali mengi ili kujua chanzo cha hali hiyo na kupima nguvu za misuli (muscle strength), kupima hisia (sensation testing), au kufanya Nerve Conduction Study (NCS) kwa kutumia vifaa kama Electromyography (EMG), MRI (Magnetic Resonance Imaging), au CT Scan na Ultrasound (USG). Baada ya hapo, wagonjwa hufanyiwa fisiotherapi, au kupewa dawa za kupunguza mgandamizo wa mishipa, au wakati mwingine kufanyiwa upasuaji.

Namshukuru Mungu nimepona bure kwa Jina la Yesu, bila kuingia gharama ya kulipia vipimo hivyo na madawa!

Miujiza kama hii ni vigumu kuiona maishani mwako kama huamini kuwa Yesu ni Mungu, Mtenda miujiza.
Amen
 
Ukimpata mwanaume wa kukukaza vizuri mbona unapona kabisa, enyi wagalatia mshughulikieni huyu kabla hali haijawa mbaya zaidi.
Ukimpata Yesu moyoni mwako mbona utapona kabisa kiroho. Enyi Wainjilisti mhubirieni kwa nguvu huyu aokoke kabla hali yake ya kiroho haijawa mbaya zaidi.
 
yeye Tu kilasiku
Yesu anawatendea miujiza watu wengi, lakini wanaokumbuka kumrudishia sifa Yesu ni wachache. Si unakumbuka habari ya wale wenye ukoma kumi aliowaponya Yesu? Ni mmoja tu aliyerudi kumshukuru Yesu (Luka 17:11–19.)
 
Why this works for you and for me, why?
Because the efficacy of divine intervention is neither arbitrary nor coincidental; it is the outworking of unwavering faith in Christ, whose power transcends circumstance and whose grace is impartial yet personal to all who believe.
 
Ooh jamani D-RICH
It’s not always me; God is faithful to all His children, and your testimony is on the way.

Mungu ni mwaminifu na ameahidi uponyaji kwa wote wamwaminio. Hata hivyo, kuna mambo muhimu ambayo mtu anapaswa kuyafanya ili apokee uponyaji. Nakutajia baadhi ya mambo hayo: Kwanza kabisa hakikisha umeokoka. Jiulize: Je, ulitubu dhambi na kuziacha? (Yakobo 5:16). Je, Yesu ni Bwana na Mwokozi wako? Kama unatambua wazi kuwa wewe ni mtoto wa Mungu, hatua inayofuata ni kuomba na kukemea. Yesu alisema tukiomba lolote tutapewa. na tena kila aliyeokoka amepewa mamlaka ya kukemea magonjwa na udhaifu wa kila aina.

Ukiishaomba na kukemea, uwe na imani isiyotetereka (Marko 11:24) – amini kwamba umepokea uponyaji hata kabla hujaona matokeo. Ukiona dalili zinaendelea, usiogope. Endelea kuamini tu. Mashaka huweza kuzuia miujiza (Yakobo 1:6-7). Kumbuka Petro alipoona upepo, aliogopa, akaingiwa na mashaka na kuanza kuzama.

Kiri/zitamke kwa imani ahadi za Mungu za uponyaji kila siku (Methali 4:20-22).
Haya hapa ni baadhi ya Maandiko yenye ahadi za uponyaji
Marko 9:23 – “Yote yanawezekana kwake aaminiye.”
1 Petro 2:24 – “Kwa kupigwa kwake tuliponywa.”
Zab 118:17 – "Sitakufa bali nitaishi, Nami nitayasimulia matendo ya BWANA."
Yeremia 30:17 – “Maana nitakurudishia afya, nami nitakuponya jeraha zako, asema Bwana.”

Wasamehe waliokukosea (Marko 11:25) – moyo usiosamehe unaweza kufunga mlango wa neema (Mathayo 6:15)

Weka tumaini lako kwa Mungu pekee, si kwa watu au njia za kibinadamu (Yeremia 17:7-8).

Hayo ni baadhi ya mambo muhimu ya kuzingatia ili uone miujiza ya uponyaji.

Yesu anakuona, anakujua kwa jina na anapenda kukuponya. Hana upendeleo, anaponya wagonjwa wote (Mathayo 8:16-17)

Kwahiyo, kama umeokoka, usikate tamaa; endelea kushikilia imani yako. Moyo wako uwe thabiti, siku yako ya kushuhudia muujiza itakuja, na wewe utaimba: ‘Yesu ameniona na mimi na kuniponya.’
Daah hapo kipengele
 
Ooh jamani D-RICH
It’s not always me; God is faithful to all His children, and your testimony is on the way.

Mungu ni mwaminifu na ameahidi uponyaji kwa wote wamwaminio. Hata hivyo, kuna mambo muhimu ambayo mtu anapaswa kuyafanya ili apokee uponyaji. Nakutajia baadhi ya mambo hayo: Kwanza kabisa hakikisha umeokoka. Jiulize: Je, ulitubu dhambi na kuziacha? (Yakobo 5:16). Je, Yesu ni Bwana na Mwokozi wako? Kama unatambua wazi kuwa wewe ni mtoto wa Mungu, hatua inayofuata ni kuomba na kukemea. Yesu alisema tukiomba lolote tutapewa. na tena kila aliyeokoka amepewa mamlaka ya kukemea magonjwa na udhaifu wa kila aina.

Ukiishaomba na kukemea, uwe na imani isiyotetereka (Marko 11:24) – amini kwamba umepokea uponyaji hata kabla hujaona matokeo. Ukiona dalili zinaendelea, usiogope. Endelea kuamini tu. Mashaka huweza kuzuia miujiza (Yakobo 1:6-7). Kumbuka Petro alipoona upepo, aliogopa, akaingiwa na mashaka na kuanza kuzama.

Kiri/zitamke kwa imani ahadi za Mungu za uponyaji kila siku (Methali 4:20-22).
Haya hapa ni baadhi ya Maandiko yenye ahadi za uponyaji
Marko 9:23 – “Yote yanawezekana kwake aaminiye.”
1 Petro 2:24 – “Kwa kupigwa kwake tuliponywa.”
Zab 118:17 – "Sitakufa bali nitaishi, Nami nitayasimulia matendo ya BWANA."
Yeremia 30:17 – “Maana nitakurudishia afya, nami nitakuponya jeraha zako, asema Bwana.”

Wasamehe waliokukosea (Marko 11:25) – moyo usiosamehe unaweza kufunga mlango wa neema (Mathayo 6:15)

Weka tumaini lako kwa Mungu pekee, si kwa watu au njia za kibinadamu (Yeremia 17:7-8).

Hayo ni baadhi ya mambo muhimu ya kuzingatia ili uone miujiza ya uponyaji.

Yesu anakuona, anakujua kwa jina na anapenda kukuponya. Hana upendeleo, anaponya wagonjwa wote (Mathayo 8:16-17)

Kwahiyo, kama umeokoka, usikate tamaa; endelea kushikilia imani yako. Moyo wako uwe thabiti, siku yako ya kushuhudia muujiza itakuja, na wewe utaimba: ‘Yesu ameniona na mimi na kuniponya.’
Hapo kipengele sana as niko Ktk situation ambayo sihitajiki kuzimu na mbinguni pia.
 
Hapo kipengele sana as niko Ktk situation ambayo sihitajiki kuzimu na mbinguni pia.
Tafadhali fafanua vizuri situation yako. Sijaelewa unaposema huhitajiki kuzimu na mbinguni??!!
 
Namshukuru Mungu nimepona bure kwa Jina la Yesu, bila kuingia gharama ya kulipia vipimo hivyo na madawa!

Miujiza kama hii ni vigumu kuiona maishani mwako kama huamini kuwa Yesu ni Mungu, Mtenda miujiza.
Wametulia hao minyoo kwa muda tu subiri wakianza kupiga kazi kwenye Ubongo
 
Wametulia hao minyoo kwa muda tu subiri wakianza kupiga kazi kwenye Ubongo
Jina la Yesu lina nguvu kubwa sana ndugu. Yesu akiponya, anaponya complete. Sio kama waganga wa kinyeji wanaotuliza tu mashetani halafu baadaye yanaamka tena.
By the way, Yesu ni Mungu, ndiye aliyeumba ubongo. Aliyeumba ubongo anashindwa kuwatoa minyoo wakiingia kwenye ubongo?
 
Kwa zaidi ya wiki moja nimekuwa nikihisi kana kwamba kuna mdudu anatambaa tambaa kwenye bega langu la kushoto. Nikipapasa sehemu hiyo sioni kitu. Leo nikasema "enough is enough"(yatosha sasa). Nikaweka mkono sehemu hiyo na kuikemea hali hiyo kwa Jina la Yesu. Hivi sasa hali ya mdudu kutambaa tambaa imetoweka kabisa katika eneo hilo! Hakika Yesu hajabadilika. Miujiza aliyoitenda miaka 2000+ iliyopita bado anaitenda hata leo kwa kila aaminiye.

Kisayansi, wenye dalili kama hizo, huambiwa kwamba wana "paresthesia." Wanapoenda hospitali, madaktari huwauliza maswali mengi ili kujua chanzo cha hali hiyo na kupima nguvu za misuli (muscle strength), kupima hisia (sensation testing), au kufanya Nerve Conduction Study (NCS) kwa kutumia vifaa kama Electromyography (EMG), MRI (Magnetic Resonance Imaging), au CT Scan na Ultrasound (USG). Baada ya hapo, wagonjwa hufanyiwa fisiotherapi, au kupewa dawa za kupunguza mgandamizo wa mishipa, au wakati mwingine kufanyiwa upasuaji.

Namshukuru Mungu nimepona bure kwa Jina la Yesu, bila kuingia gharama ya kulipia vipimo hivyo na madawa!

Miujiza kama hii ni vigumu kuiona maishani mwako kama huamini kuwa Yesu ni Mungu, Mtenda miujiza.
Una ugonjwa wa akili psychiatrist yoyote ange kutibu sio mythical person who is supposed to have lived two thousand years ago
 
Jina la Yesu lina nguvu kubwa sana ndugu. Yesu akiponya, anaponya complete. Sio kama waganga wa kinyeji wanaotuliza tu mashetani halafu baadaye yanaamka tena.
By the way, Yesu ni Mungu, ndiye aliyeumba ubongo. Aliyeumba ubongo anashindwa kuwatoa minyoo wakiingia kwenye ubongo?
Wameshaingia kwenye Ubongo au bado?
 
Una ugonjwa wa akili psychiatrist yoyote ange kutibu sio mythical person who is supposed to have lived two thousand years ago
Yesu ni zaidi ya psychiatrists. Psychiatrists wanakufa na kuoza. Yesu alikufa akafufuka. Yuko hai hata leo. Anaendelea kutenda miujiza kwa kila aaminiye.
 
Back
Top Bottom