Leo nimeshuhudia pepo linamuingia mtu

Leo nimeshuhudia pepo linamuingia mtu

Asifanye nyumbani. Akafanye hayo mambo nje huko. Inamaanisha leo nisingekuwepo inawezekana wangefanya mambo yao sebuleni au jikoni. Na vipi kuhusu usalama wa mali zetu na hata usalama wetu wengine? Hii hali ya kutojali ni hatari sana.
Popote ni kambi...


Cc: mahondaw
 
Yesu ana nafasi katika kila ninalolifanya katika maisha yangu, kwenye hilo sioni aibu wala kujiuliza. Bakora hizo amepigwa sana na ndugu zake wa kike lakini hazijasaidia. Mimi anajua sana ukali wangu ila sijawahi kumgusa. Maandiko yanasema vita yetu siyo ya mwili na damu. Leo nimekemea na pepo ameshindwa, na anayeamini na aamini.
Huo ni upumbafuuuuu
 
Wewe si ndiyo umekana uwepo wa Mungu? Subiri kwa wakati wake atakuja kujidhihirisha kwako. Kila goti litapigwa.
Huu nao ni upumbafuuuu.
Nimekana wapi? Yaani kukataa kulitaja ovyo jina la Yesu ina maana ni kukataa uwepo wa Mungu?
Akili za kiazi hizi.
Halafu kwani ukilitaja jina la Mungu mara nyingi ndio ibada? Ndio atakusamehe madhambi yako siyo?
 
Huu nao ni upumbafuuuu.
Nimekana wapi? Yaani kukataa kulitaja ovyo jina la Yesu ina maana ni kukataa uwepo wa Mungu?
Akili za kiazi hizi.
Halafu kwani ukilitaja jina la Mungu mara nyingi ndio ibada? Ndio atakusamehe madhambi yako siyo?

Unaanza kukana maneno yako mwenyewe, hiyo ni hatua ya kwanza. Ila nenda zaidi, mkiri Yesu kwamba ni Bwana na Mwokozi wako, fanya hivyo bila aibu bali kwa furaha, sifa na shangwe. Yesu hana muda maalumu wa kumtaja. Namshukuru nikiwa nalala, na nikiwa naaamka. Namshukuru kabla na hata baada ya kula. Namshukuru hata nikiwa naoga. Namshukuru nikiwa napita mtaani. Yaani nalitaja jina lake wakati wowote, ni shetani tu na mawakala wake ndiyo hawapendi kulisikia jina lake.

Hamna aliyeongelea dhambi kwenye uzi huu mzima na hamna aliyehukumiwa, ukiacha baadhi ya walionihukumu mimi. Nimeanzisha uzi kuthibitisha uwepo wa mapepo lakini zaidi uwezo wa nguvu za Mungu kutenda kwa jinsi anavyoona yeye inafaa. Nina ushuhuda mwingi wa rehema, huruma na baraka za Mungu katika maisha yangu mwenyewe naweza kuandika vitabu.

Mungu amenipenda sana ili Yeye atukuzwe. Hata nafurahi sana kuanzisha uzi huu NAJUA Jina lake litatukizwa tu, hamna namna.
 
Unaanza kukana maneno yako mwenyewe, hiyo ni hatua ya kwanza. Ila nenda zaidi, mkiri Yesu kwamba ni Bwana na Mwokozi wako, fanya hivyo bila aibu bali kwa furaha, sifa na shangwe. Yesu hana muda maalumu wa kumtaja. Namshukuru nikiwa nalala, na nikiwa naaamka. Namshukuru kabla na hata baada ya kula. Namshukuru hata nikiwa naoga. Namshukuru nikiwa napita mtaani. Yaani nalitaja jina lake wakati wowote, ni shetani tu na mawakala wake ndiyo hawapendi kulisikia jina lake.

Hamna aliyeongelea dhambi kwenye uzi huu mzima na hamna aliyehukumiwa, ukiacha baadhi ya walionihukumu mimi. Nimeanzisha uzi kuthibitisha uwepo wa mapepo lakini zaidi uwezo wa nguvu za Mungu kutenda kwa jinsi anavyoona yeye inafaa. Nina ushuhuda mwingi wa rehema, huruma na baraka za Mungu katika maisha yangu mwenyewe naweza kuandika vitabu.
Ujinga namba moja.
 
Imebidi nigeuze simu ndo nielewe hii story eniwei hilo pepo lake limekaa sehemu mbaya sana.Anahitaji maombi ya nguvu.
 
Kuna tatizo la kiafya linaitwa PERSISTENT SEXUAL AROUSAL SYNDROME hivyo unahitaji kuwaona wataalamu wa Afya japo sikushauri uache maombi unayoyafanya
 
Imebidi nigeuze simu ndo nielewe hii story eniwei hilo pepo lake limekaa sehemu mbaya sana.Anahitaji maombi ya nguvu.

Nashukuru kama umeelewa. Sikuiandika nikitegemea kushinda Pulitzer Prize.
 
mlokole at work,ukibanwa kimba unafkiri ni popobawa unaanza kukemea,huo binti ana nyege tu nandio umri wake kupigwa miti mfukuze basi km hutaki akanyagwe

Kuna tatizo la kiafya linaitwa PERSISTENT SEXUAL AROUSAL SYNDROME hivyo unahitaji kuwaona wataalamu wa Afya japo sikushauri uache maombi unayoyafanya

Kwa nini sasa anatongoza mwanaume halafu wakiwa wanakaribia tendo anageuka? Kumbuka alishawahi kusema kuna mtu alitaka kumbaka, na nani anajua hayo matukio yamekuwa mangapi mpasa sasa na ni mara ngapi amebakwa kweli. Leo nimeshuhudia advances zake halafu mihemko ikiwa juu ni kama fahamu zinamrudia anabadili mawazo. Ni story ya kusikitisha, sikuileta kufurahisha kadamnasi.
 
Usimbane MPE nafasi ya kutiwa hata Mara moja moja yaonekana una wivu sana usimbane we endelea Na maombi yako.atazichoka maana mbo@@ hazina utani.
 
Kuna mtu alinishauri nimuwekee mikono ila yasije kunitokea ya wale walikimbizwa na mapepo. Namuamini Mungu sana tu lakini mambo mengine yanahitaji kuwa na karama zake otherwise ni hatari tupu.

Jana nilikuwa naangalia video ya TB Joshua, kuna mchugaji Kenya alikuwa mahiri wa kukemea mapepo na alikuwa anatumia hata physical means. Siku moja yakamshambulia, jamaa alikuwa hata hawezi kutembea alikuwa anatambaa. TB Joshua akamwambia kila mtu ana karama zake, haya ya kuconfront mapepo one on one ni mambo hatari sana. Nitaendelea kumuweka katika maombi, definitely.
sure you better be sure with your God

Sent from my SM-J100H using JamiiForums mobile app
 
Pole na hilo tatizo,lakini kwa maoni yangu,unapoajiri mtu wa kukufanyia kazi unatakiwa uangalie vigezo,na kigezo cha kwanza kwa dada wa ndani ni usafi kwa ujumla na afya yake pia,ili kujilinda wewe na familia yako na wageni wako,pamoja na majirani zako,sasa basi umesema si msafi ,so kwanini unaishi na dada wa ndani mchafu?je unajitahidi kufundisha usafi?
Kuhusu afya yake,umesema amemchikoza fundi wa watu,huoni kama umemkosea huyo fundi kwa kumuweka jirani na dada ambaye unajua anamatatizo?ni vema kama unaona unamuhitaji kumsaidia au kuendelea kuishi nae fanya maamuzi haraka,mpeleke hospitali akapimwe afya yake,na kamakunauhitaji wa ushauri kuna wataalam huko hospitali watakushauri,pia endelea na maombi yako,au la mrudishe kwao ,usichekecheke utakuja pata kesi kubwa ,maana hujui anamatatizo gani.ni maoni tu yangu.
 
Pole na hilo tatizo,lakini kwa maoni yangu,unapoajiri mtu wa kukufanyia kazi unatakiwa uangalie vigezo.........

Asante sana kwa ulichosema. Umesema na kuuliza mambo ya msingi sana. Uzuri vitu ulivyosema tayari nimevitafakari kwa muda mrefu, ndiyo maana hata sikufikiria kuifanya hii issue kubwa zaidi in terms of polisi, nk. Usafi amefundishwa saaaana tu, mimi bado naamini kuna vitu vya kukemea vimtoke pamoja na psychological issues.

Kuhusu kuzingatia sifa stahiki za mtu unayemuajiri, ni fundisho kubwa ambalo nashukuru Mungu nimejifunza first hand. Kumuajiri the wrong person for the right job, or the right person for the wrong job. Nalitumia hilo fundisho hata kwenye shughuli zangu zingine. Nimejifunza mengi.

Kwa wanaosema nina wivu sijui vitu gani, jana tumemkalisha chini atupe maelezo yake, yeye mwenyewe kwa kauli yake amesema bila mimi kuingilia, jambo baya lingemtokea. Najua hajatupa maelezo yote ila hiyo ndiyo kauli yake.

Nitafanya maamuzi ya haraka kwa usalama na faida ya wote.
 
Endeleeni kusingizia "mapepo" wakati tamaa za "ngono" zipo ndani ya miili yenu wenyewe. Nakerwa sana na hawa Manabii feki kama TB Joshua ambao kila dhambi wao wanasingizia ni "mapepo". Mtu akiwa mlevi ni mapepo, mtu akiwa malaya ni mapepo, mtu akiwa jambazi ni mapepo, mtu akiwa shoga ni mapepo, mtu akiwa mpiga punyeto ni mapepo, mtu akiwa mwongo, mwongo ni mapepo, yaani kwao kila kitu ni mapepo.

Ni uwongo mkubwa sana kusema dhambi zinasababishwa na mapepo. Biblia iko wazi kabisa na imeandikwa kuwa mtu anajaribiwa kwa tamaa zake mwenyewe. Siyo kwamba mapepo hawapo, hapana; wapo sana lakini siyo kweli kwamba unapofanya dhambi eti ni pepo linakulazimisha. Ingekuwa tunatenda dhambi sababu ya kulazimishwa na mapepo, basi MUNGU asingeweka hukumu juu yetu, MUNGU asingeleta gharika duniani wala asingeichoma moto miji ya Sodoma na Gomora, badala yake angetuma jeshi la Malaika waje wayakamate hayo mapepo yanayowalazimisha watu wake kutenda dhambi na kuyachoma moto.

Ukweli ni kwamba tunatenda dhambi kwa hiari yetu wenyewe na ndiyo maana Biblia imesema wazi kabisa kuwa watenda dhambi wote watachomwa moto. Acheni kudanganywa na hawa manabii wa uongo wanaosingizia mapepo na kufanya maigizo makanisani ili wapate waumini wengi na watazamaji wa Tv zao. Shetani ni mjanja sana, anawadanganya watu waone kuwa kumbe kutenda dhambi ni sababu ya kulazimishwa au kuendeshwa na PEPO, matokeo yake watu wanaendelea kutenda dhambi na kusingizia MAPEPO. Kutenda dhambi ni hiari, na kutenda mema ni hiari pia.

BWANA MUNGU alimwambia Kaini maneno haya; "dhambi iko mlangoni inakuotea na tamaa yake iko juu yako, walakini yakupasa uishinde". Bwana MUNGU anajua fika kuwa Mwanadamu anauwezo wa kuishinda dhambi na ndiyo maana akamwambi Kaini maneno hayo. YESU KRISTO alikuwa mwanadamu wa kawaida kama mimi na wewe na aliishinda dhambi. Nuhu aliishinda dhambi, Danieli aliishinda dhambi, Ayubu alikuwa mtu wa kawaida kama mimi na wewe na aliishinda dhambi.

Soma EZEKIELI 18:21-23
 
Ungeeleza tu kwa mlengo wa Dini, umechanganya changanya sana
 
Back
Top Bottom