MWANASIASA HURU
Senior Member
- Oct 4, 2012
- 181
- 239
Habari wana MMU,
Nina mpenzi wangu ambaye tuna muda kidogo. Hapa kati niligundua anachepuka baada ya kuona msg kwenye simu yake,nilipomuuliza akakataa katakata na ugomvi juu nkajishusha yakaisha but moyoni mwangu nlikua namchunguza kimya kimya.
Kwa kawaida huwa tunapitiana asbh kwenda kazini kwan ofisi zetu zipo karibu, basi Leo nimeenda kama kawa nikagonga but hakufungua ila nilisikia movement ndani ameamka akawasha gesi na kubandika Maji ya kuoga basi nikajua atafungua mlango, nikaona kimya ila machale yakanicheza nikapanga kukaa nje mpaka nione mwisho, simu zangu nikaweka silent baada ya dk 40 hivi nikasikia sauti ya mwanamke ndani kumbe ndo alikua anamwandalia maji.
Ile kufungua mlango akakutana na macho yangu makavu nikamsalimia nikaingia chumbani nikamsalimia binti nikarudi kukaa sebuleni, bidada akanikaribisha kwa adabu zote nikamwambia apumzike tu asijali, kaka katoka kuoga anajishaua kuniuliza eti kwanini sijaenda kazini nimesimama tu nje m sikumjibu ktu akaingia rum kuvaa mi nimekaa tu sebuleni.
Sikutaka ugomvi kiukweli coz najijua hasira zangu ningechoma mtu kisu bure, basi bidada akavaa nguo huyo akaondoka na akaniaga eti Dada bye nikamwambia ok karibu tena! Alipoondoka nikamuuliza is it me or her akakosa jibu, nikaondoka zangu!
Now msg kibao za maelezo mimi sijajibu hata moja, hivi wanaume kwanini hamtosheki jamani? Bora nibaki single tu kuliko kuleteana magonjwa
samahani, nimesoma mara mbili ila sijaelewa. nilitegemea na wenzangu wacomment the same ila naona kama wameelewa. kiukweli sijapata picha halisi. aliyefumania ni ke au me? bidada ni nani? kifupi sijaelewa.
uliyeelewa unisamehe pia. kama unaweza nieleweshe.