Nimegombana na Mke wangu leo mpaka nimeshangaa

knows

JF-Expert Member
Nov 9, 2021
1,403
2,006
Habar wana JF,

Nashukuru mungu wote ni wazima
Mtanisamehe mimi sio muandishi mzuri sana wakuu.

Nimetoka kugombana na wife mpaka nimebaki nashangaa na kuwaza kwa maneno alioyasema wife, nikwamba wife ni mjamzito wa miezi 4 sasa anatimiza ikifika tarehe 13 sasa leo nimetoka kazini nikawa nimekaa kwenye gari nawaza sana kutokana na maisha na life style anayoishi wife sio kabsa kiupande mwingine.

Kutokana na maisha yalivyo toka wife amebeba mimba anaishi life style ambayo kwa upande mwingine bado haijanivutia lakin ni kawaida sana yeye ni 24hrs/7days yupo ndani amelala akichoka anafungua insta atashinda mitandaoni akichoka sebleni kuangalia TV tamthilia zake mwenyewe.

Ni vizuri kupata muda wa kupumzika kwa hali yake lakini mimba sio mzigo au mimba sio ugonjwa ukufanye ushinde ndani 24hrs. Nikampigia sim kumjulia hali kashindaje leo then nikamuuliza unafanya nini akajibu yupo kitandani amelala.

Nikamwambia kiupole sana na kiutaarabu kuwa mkewangu em bas uwe unatoka na kuchakarika kuna duka la biashara now yupo kijana uwe hata unakwenda basi kuangalia mambo yanaendaje sio hadi mimi nitoke kazini nimechoka nipitie tena huko wakati wewe upo tu nyumbani umetulia vituvingine ni kuichangamsha akili na kupambana kuliko kushinda tu ndani mamaangu wewe sio mgonjwa.

Kusema kwamba huwez kutembea mbona kuna wanawake wana mimba lakini wanachakalika wengine unakutana nao anatumbo kubwa kabeba beseni lake la mboga anatembeza mitaani wengine wanakimbiza maofisi na matumbo yao tena makubwa lakin wanachakalika asubuh na mapema kashafika ofisi nikamwambia hayo siyo maisha uyaotaka kuishi.

Sijajua nihilo tu au kuna mengine ila Alivimba na kuanza kuongea kwa hasira na kuongea maneno mengi sana ambayo sikutegemea na kusema kuwa namnyanyasa mara kisa kubeba mimba naanza kumuona mjinga so nisimfananishe na hao wajinga ye anaakili zake na anajua anachofanya, mara nimeanza kumuona mzigo kwangu kwakuwa kabeba mimba duuh wakuu nilibaki nimeishiwa nguvu maana sikutegemea kama ndo yangekuwa hayo mara sasa ataondoka ataenda kukaa kwao duuh.

Kiukweli sikumjibu chochote nikaamua kutumia hekima tu maana yeye teali alishapanda kaamua kushuka nakumuacha nikakata simu yangu nikawaza sana huyu skuiz amekuaje kwamba ndo mimba inampeleka hivyo au nikaacha kama yalivyo lakin narud nyumbani njiani ninawaza sana yale maneno Nikafika home nikaingia ndani nikamkuta kakaa sebleni, sikumsemesha chochote nikapitiliza jikoni nikamkuta beki 3 anapika nikamuuliza kuwa dadaako kala akasema ndio alikula na saivi ndio napika chakula cha usiku nikasema powa nikapitiliza chumbani nikaingia bafuni nikaoga nikamaliza nikapanda kitandani nikapumzika.

Dakika 3 akaja chumbani kimya sikumsemesha kakaa nikamwambia jiandae kesho nakupa nauli yakuendea huko kwenu iliuepuke hayo manyanyaso unayosema.

Nikainuka nikavaa nikafungua mlango kabla sijatoka nikamwambia natoka napiga simu kwenu kesho wakupokee nikaondoka zangu now nipo somewhere nimetulia kwanza ila kweli nimewaza huyu kesho namsafirisha kweli sioutani acha aende kwanza kwao akatulie akikaribia kujifungua nitamfata wakuu kwasababu najitahdi sana anapopanda namimi nisipande maana minajijua nina hasira sana.
 
Habar wana JF,

Nashukuru mungu wote ni wazima
Mtanisamehe mimi sio muandishi mzuri sana wakuu.

Nimetoka kugombana na wife mpaka nimebaki nashangaa na kuwaza kwa maneno alioyasema wife, nikwamba wife ni
1. Una umri gani mkuu?
2. Hii ni mimba ya kwanza?
3. Uliwahi kusikia habari za wajawazito?
4. Ulikuwa na haraka gani ya kupiga simu na
Uongee maneno mengi kiasi hicho?.

Makosa ni ya kwako umebwabwaja sana kwa mjamzito.

Uliposwa uwe na subra, ufike home mnaongea kirafiki huku ukipapasa kitumbo chake taratiiibu.
 
Angekuwa mtumishi ingekuaje

Weacha tu mkuu sababu kuna dada nafanya nae kazi ofisi moja yule dada alikuwa mjamzito yule dada alikuwa anakuja kazini mbaka anajifungua ndo wakampa likizo ya uzazi lakin alikuwa na uwezo wa kuomba likizo before hata ya kujifungua akajifungulie hata kwao lakini wapi mbakatulikuwa tunamuonea huruma kazi nyingine za kiofisi tunamsaidia katoka kujifungua January mtoto wa kiume
 
1. Una umri gani mkuu?
2. Hii ni mimba ya kwanza?
3. Uliwahi kusikia habari za wajawazito?
4. Ulikuwa na haraka gani ya kupiga simu na
Uongee maneno mengi kiasi hicho?.

Makosa ni ya kwako umebwabwaja sana kwa mjamzito.

Uliposwa uwe na subra, ufike home mnaongea kirafiki huku ukipapasa kitumbo chake taratiiibu.

2:Mimba ya kwanza
3:ndio nafahamu mkuu
4: kwani nikosa kuongea na mkewangu tena kwa upendo lakin nalo kosa?
 
IMG_1039.jpg
 
shida sio mimba wala nini ana mambo yake tu huyo, na itakuwa vizuri ukichukua maamuzi ya kiume vunginevyo ndo anakusoma na atakupanda kichwani huko mbele, usiamue hili jambo kwa hisia za mapenzi nakuambia mapenzi yamewaangusha wengi, tumia akili na mamlaka yako kama mume, mpeleke nyumbani kweli, hapo atajua huyu akisema nakuacha ananiacha kweli hatanii, ukilegeza mzee itakula kwako ndo anakusoma huyo
 
Back
Top Bottom