Leo nawatukana!

Leo nawatukana!

Wewe kijana tulia
Wenzako tunajua
Acha zako kelele
Nenda kabebe zege
Wenzako tunajua tunashindwa kugagadua
Kazi yako ni uganga
Ofisi yako iko tabata
Tulia Fanya yako. Watoto wale bata
 
tafuta kazi we pumbavu,badala ya kuandika kitabu "how to be rich`"au ujasisiriamali uuze km mwenzio shigongo we unaleta mashairi ya sa nane,huyo ushaambiwa na wenyewe manyumbu yupo mzima wa afya na vijiwe vyake vya kahawa anaonekana,msitupotezee muda nyumbu
 
Beni keshapotea kama farujoni
Hataandika tena phd yake joni
Wauza tisheti feza waesabu jioni
Gazeti laandika anywa kahawa jioni
tuamini atapatikana hata kama jioni.
 
Kuna wale misukule, waliofugwa akili,
Na wamefungwa kengele,na hawa watu katili,
kazi kupiga kelele,si wa moja si wa mbili,
Ndiyo wanaowadekeza.
 
Beni huyu Saa nane, kenda karibu na kumi
Bora sana tusinene, mukatuona wahuni
La moyoni tuliseme, isiwe yu aridhini
Siri wanayo wanene, yazungumzwa vikaoni

Beni siyo alibino, kama angekuwa dili
Ni mweusi kama wino, na hanao mwingi mwili
Iweje leo hayumo, humu ndani kwa ipi siri
Wametaka yake meno, tuwaulize majangiri!

Beni ni kitendawili, ajuwae ategue
Kajificha cha tumbili, ndio nionavyo mie
Hatunae tena kimwili, ajuwae atwambie
Haisemwi hii siri, hata na bosi wake Mbowe

Sitaki kusema sana, nitakwe kuomba radhi
Leo sote tumeona, nisije poteza hadhi
Ikiwa hatujamuona, kazongwa na nyingi kazi
Ni nyingi zimembana, tokea hayo majuzi

Beni urudi nyumbani, usikawie mwanetu
Watutia kisirani, sote tafrani mtu
Tusikii hatuoni, tumefika kwa Wahutu
Kama uko kwa jirani, urudi nyumbani kwetu

Unajua Mkuu!
 
Deko lao makatili, chanzo chake sisi sisi,
tunapokubali dhalili,na ladha ya ukakasi,
Wabaya tumekubali, tumewapa ukasisi,
Hilo ndiyo kosa letu.
 
Mwenyekiti katangaza, ukurasa amefunga,
Acha domo kusambaza, wabaya watamzonga,
Mbowe keshawamaliza, chake chama kinasonga.

Mbona wewe hajakumaliza??Un akili kama za wenzko Mafisi
 
Acheni wenu uzushi,
wenzenu hawakanushi,
hawaleti kashikashi,
uvundo msinakshi,
wanajua walotenda.

Tabia yenu asili,
mnapenda kubadili,
kile kilicho halali,
mnakifanya dhalili,
Ben mrudisheni.

Awe hai awe mfu,
kwetu hajatukifu,
msijipe utukufu,
mkatuvika upofu,
Mnahusika.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom