Mkuu umenena. Kama ambavyo tunaagiza ngano na kusagisha hapa nyumbani, hivyo hivyo wanunuzi wa mahindi wanataka kununua na kusagisha huko kwao watakavyo na kutokana na taste ya walaji wa kwao. Hatuwezi kuwalazimisha kununua unga wa kwetu, after all shelf life ya unga ni ndogo sana ukilinganisha na mahindi yanayoweza kuhifadhiwa kwa miaka.
saa ingine wanahitaji mahindi ya kupika makande,au kutengeza chakula cha kuku,wewe unataka kuuwauzia unga,hawakubali
Kalamu1
Nimesoma, lakini sikufika mwisho aisee, kwa sababu ninakubaliana na hoja yako moja kwa moja.
Nani yule, anauza unga wa ngano (AZAM). Kwa nini unga wa mahindi uwe shida?
Hakuna sababu hata ndogo kwa Tanzania kuuza mahindi Kenya. Kama ni mfanya biashara, weka mashine zako pale karibu na mpaka, nunua mahindi, saga kwa viwango vinavyotakiwa kwa bidhaa hiyo huko Kenya, package na nenda kasambaze kwenye supermarkets zao bidhaa zako. Shida ipo wapi
Mbali ya mahindi. Kwa nini tunaruhusu kuuza vitunguu kwa makampuni ya Kenya yanayo package na kuvisafirisha nje ya nchi hiyo kama bidhaa toka nchini humo. Hapa kwetu hatuna wafanya biashara wanaoweza kukusanya toka kwa wakulima, wakapackage' na kusafirisha nje kama bidhaa yetu, iliyotoka Tanzania?
Hawa wafanya biashara wetu wapiga kelele nyingi lakini akili ni kama zimelala.
Haya, sasa tunazungumza kuwauzia gesi, wakatengeneze umeme. Hivi hapa kwetu hatuwezi kuzalisha umeme na kuusafirisha hadi Kenya?
Tanzania tunayo matatizo makubwa!
Kalamu1 naungana na mawazo yako,mahindi yakiwa processed hapa kwetu hiyo maana yake tumebakisha ajira nyumbani.Mansander kwenye uzi huu majibu ya hoja zako nafikiri umeyaona,mtu kama kweli hii ni biashara yake yeye atajua wateja wake kule Kenya wanataka bidhaa katika hali gani mfano. mahindi yaliyokobolewa,unga wa sembe au dona ama anahitaji pumba. Uwezo wa kuwalazimisha hatuna lakini uhitaji wao ndo utawafanya waweke mezani wanahita end product ikiwa katika hali gani nasi tutatii kwakuwa tunaitaka pesa yao that is business. Shelf time ya unga kuwa ndogo ukilinganisha na ile ya mahindi ni sawa,kwa mfanya biashara makini ndo maana anakuwa na ghala la kufifadhia mahindi yake kwahiyo atakuwa akiyaprocess kulingana na mahitaji ya soko.
Elungata nawe nafikiri umeona majibu ya hoya zako. Kwahiyo kila mteja ataleta mahitaji yake na atapatiwa bidhaa yake.
Kalamu1 Tanzania tunayo matatizo makubwa! Na kinyume chake pia ni sahihi,matatizo hayo makubwa tuliyonayo ni ukubwa wa fursa tulizonazo kwahiyo tuendelee kuzichangamkia kadiri iwezekanavyo. Kila anayetatua matatizo yanayotuzunguka ndo hivyo hivyo anatengeneza fedha.