Leo IKULU Bashe kaanza vizuri japo kakosea

Leo IKULU Bashe kaanza vizuri japo kakosea

Mkuu ww unatupangia sisi wakulima tumuuzie nani mazao yetu wakati ww uko ofisini? Huo ukiritimba hatutaki, unataka kupangiwa mtu wa kumuuzia kalime na ww usubiri huo ukiritimba. Tunataka mteja afike anunue mazao yetu na atulipe hapo hapo. Sio wakulima tunakufa kwa umasikini nyie wenye vitambi huko maofisini mnajifanya kupanga utaratibu.
Hata mimi ni mkulima. Kuna deal kadhaa za mauzo ya nje nishawahi kuzipata. Soko halikuwa tayari na halitakuwa tayari kununua gunia 100. Wanataka tani kadhaa, na kila mwezi mzigo unaingia sokoni.

Naelewa namna gani ukiwa unauza peke yako gunia 10 (ambazo zina kg 100 kila moja)una-negotiate katika point of weakness.
Ni tofauti mkiwa wakulima 2000 mna magunia ya unga packaged in 50 kgs, 25kgs na 5kgs.

Kenya wana culture ya kununua vitu supermakets na small groceries. Tukiwa na mzigo ukaingia made in Tz huo ndiyo mpango mzima.

Ila kwa kuwa tumeamua kila mmoja auze peke yake, basi yote ni maamuzi na Naibu Waziri katoa maelekezo. Mimi sina mtoto wa kike na sina nguvu ya ku-negotiate mahari
 
Mambo yote ya achwe ya ende sambamba, mkulima auze mazao yake anapotaka na mwenye kuona kiwanda kina mlipa akianzishe aprocess mazao na ayauze kama semi processed au kwa mlaji wa mwisho.

Serikali isaidie kuanzisha vituo vya masoko ya mazao venye sifa stahiki na kuhakikisha wakulima wanapata farm gate price isiyo ya kupunjwa na dhuluma.

Kuwe na mpango ambao utawavutia wafanyabiashara wa viwanda wasitoke EA na kuhemea mahindi na ngano barani Amerika.
 
Wanabodi,
Naomba ku-declare interest kuwa sina ugomvi binafsi na Naibu Waziri Hussein Bashe.
Nimekuwa namkubali kwa namna ambavyo alikuwa aki-analyse dhana ya mnyororo wa thamani hususan kwenye sekta ya KILIMO kwa michango yake "mjengoni"

Nadhani, sio sawa kutoa ruhusa kwa Wakenya kuingia kwenda kununua mahidi kwa wakulima. Pengine hatuja-set regulations za namna ya kufanya biashara ya mazao mchanganyiko. Jambo hili litutake tujenge mfumo rasmi wa manunuzi ya mazao mchanganyiko. Sio waje kwenda kununua mahindi moja kwa moja kwa wakulima.

Intermediaries wana sehemu yake kwenye biashara kama watasajiliwa. Kwenye bima kuna Brokers, na agents kama intermediaries. Hata bank ni intermediary ambae tukiweka mfumo bora wa mauzo banks zitakuwa na mifumo rasmi ya kugusa wakulima na TRA ana-access ya kodi kuoitia wigo utakaopanuka.

Huwezi kwenda Marekani ukanunua maziwa kwa wakulima then ukapaleka kiwandani wakufanyie packaging halafu usafirishe. Haiko hivyo.

Mhe. Naibu Waziri you can do the best kwa kushirikiana na Mhe. Hasunga na mtengeneza mifumo rasmi ili mahindi yaunuliwe, yakobolewe/kusagwa moja kwa moja na Kenya asubiri mahindi kule kwao. Ikiwa hivyo kwa haraka haraka itaongeza mzunguko wa fedha kwa Watanzania kwa mfumo wa mauzo, ulinzi kwenye maghala, bima za hifadhi kwenye maghala na vyanzo vya ajira kwa kujenga mfumo.

Kama ambavyokwenye madini (hatuuzi raw kwa wageni ili wakachakate makinikia kwenye refineries kwa wageni) na kwenye mahindi tuwe na mfumo wa soko maalum la finished products.

Tukisaga unga kwetu na ku-package sisi ni vema pia tuka-control logistics. Walau sio mbaya Kenya apokee mzigo mpakani kwake ili Magari ya Watanzania yahusike kusafirisha unga uliosindikwa. Hii ina akisi kutoa ajira na kuongeza wigo wa mzunguko nchini hali kadhalika kodi.

Kama ambavyo niliwahi kushauri hapa JF wakati wa zoezi la kupekeka mahindi Zimbabwe na Namibia; tunaposema tunajenga Tanzania ya viwanda kwa kuongeza thamani kwenye mazao ghafi na kupata tija kwa kuuza packaged final product, sasa tufanye kwa vitendo.
Mhe. Hasunga hakuona hiyo fursa, naomba pia mhe Bashe usianze vibaya.

Natoa ushauri mapema kabla mambo hayajaharibika. Kama mtasonga mbele na maamuzi hatuna namna ya kuwazuia ila tuna jukumu la kuwashauri namna gani mfanye vyema. Mnachokifanya kiwe na taswira ya kujenga uchumi na kukuza uchumi kupitia sekta ya viwanda.

Mungu Ibariki Tanzania
Nilivyomwelewa watanunua kwenye Bodi ya mazao mchanganyiko bila kupitia kwa madalali ni kwenda kusaga kwenye vinue vyetu ndiposa wasafirishe kama unga
 
Kwa hiyo kama mtu anataka kula kande huko kenya inakuaje? Hata wao wanafuga na wanashida na pumba vile vile acha roho mbaya.
Mkuu umenena. Kama ambavyo tunaagiza ngano na kusagisha hapa nyumbani, hivyo hivyo wanunuzi wa mahindi wanataka kununua na kusagisha huko kwao watakavyo na kutokana na taste ya walaji wa kwao. Hatuwezi kuwalazimisha kununua unga wa kwetu, after all shelf life ya unga ni ndogo sana ukilinganisha na mahindi yanayoweza kuhifadhiwa kwa miaka.
 
Mimi sikubaliani kabisa kuwepo kwa madalali/watu wa kati/walanguzi.

Ila kwenye biashara intermediaries huwa zipo. Kama ambayo una hela unamtumia mtu, kuna bank au mobile money kama mtu kati.

Shauku yangu, warasimishwe ili naoa mfumo uwatambue. Likifanyika kila mmoja ana-win.

Mbona hatuendi kununua Cement Tanga au Mbeya au kokote. Tunanunua kwa retailers ambao nao wananunua kwa wholesalers.

Tukirasimisha mfumo, tunaongeza mzunguko wa fedha katika organized systems.

Ila kama Serikali ikiamua, mimi ni nani kuzuia mambo hayo yasifanyike. Maana jana nimeona moja ya lecture the boss is always right. So far if that is true, I can just advise professionally na sio vinginevyo.
Sijajua vema maana ya "intermediaries" niweze kutofautisha na "Mtu kati". Hata hivyo napingana na interpretation yako kuwa Bashe ameruhusu kwenda shambani kwa mkulima bali amewahakikishia hawatafanya biashara na mtu kati. Utambue hili la kuuziwa mahindi ni ombi la serikali ya Kenya kwa serikali na Bashe amesema kama kuna wafanyabiashara wanatakiwa wakutane na wizara watawatengenezea "Modality" ikiwa pamoja na kuwashauri wasage katika vinu vyetu vya Umma na wasafirishe processed product.
Umetoa mfano mzuri wa Cement, inapokuwa buck procurement si kweli mnunuzi toka nje atanunua kwa retailer! Atanunuwa moja kwa moja kiwandani kwa usimamizi wa serikali na kulipa kodi zote halali.
 
Jibu ni vyama vya ushirika ndio wawe na dhamana ya kununua nafaka zote na hao wakenya waende kwenye vyama vya ushirika.
 
Hata mimi ni mkulima. Kuna deal kadhaa za mauzo ya nje nishawahi kuzipata. Soko halikuwa tayari na halitakuwa tayari kununua gunia 100. Wanataka tani kadhaa, na kila mwezi mzigo unaingia sokoni.

Naelewa namna gani ukiwa unauza peke yako gunia 10 (ambazo zina kg 100 kila moja)una-negotiate katika point of weakness.
Ni tofauti mkiwa wakulima 2000 mna magunia ya unga packaged in 50 kgs, 25kgs na 5kgs.

Kenya wana culture ya kununua vitu supermakets na small groceries. Tukiwa na mzigo ukaingia made in Tz huo ndiyo mpango mzima.

Ila kwa kuwa tumeamua kila mmoja auze peke yake, basi yote ni maamuzi na Naibu Waziri katoa maelekezo. Mimi sina mtoto wa kike na sina nguvu ya ku-negotiate mahari

Hayo makundi au vikundi vya ushirika vya manunuzi ya mazao tuna uzoefu nayo, kinachoendelea huko ni dhuluma na siasa zisizo na tija. Kama ww umepata soko linalokulipa nje, andika proposal nenda bank kopa hela kisha kanunue mzigo kwa wakulima fullstop. Mambo ya vikundi mwisho wake ni utapeli na kuleta siasa na Majungu kwenye mazao ya wakulima.
 
Mahindi yauzwe kwa mfumo wa stakabdhi ghalani.Mkenya kwenda kwa mkulima ni kumuibia tu. Mifano ipo mingi, huko Mpwapwa Dodoma, kuna kata inaitwa Lumuma, maarufu kwa kilimo cha Kitunguu. Wakenya wanakwenda na sandarusi la 120kg, linakuwa regarded ni la 100Kg. Huko Lindi na Mtwara mfumo wa stakabadhi ghalani, umeonyesha mafanikio si tu kwa korosho bali hata kwa ufuta. Vinginevyo, NFRA wanunue kwa bei nzuri mahindi toka kwa wakulima halafu wao wauze Zimbabwe na nk.
 
Ukiwa nje ya uwanja unaweza kucheza utakavyo kwa kukisia tu na kutikisa kichwa, huyo Msoma Ali ni lopo lopo tu na sioni kama kuna weredi wowote labda aendelee kuchukua huo unaoita ushauri.... kwa mfano wa uandishi kama huu ni mashaka makubwa kuhusu set up ya kichwa chake. [emoji1484][emoji1484][emoji1484][emoji1484]
View attachment 1161465
Naomba ufahamu kuwa Bashe ni mtoto wa sheikh pale Nzega sijaelewa kwanini uone alichoandika hakina mantiki?
 
saa ingine wanahitaji mahindi ya kupika makande,au kutengeza chakula cha kuku,wewe unataka kuuwauzia unga,hawakubali
 
Tukisaga unga kwetu na ku-package sisi ni vema pia tuka-control logistics.
Nimesoma, lakini sikufika mwisho aisee, kwa sababu ninakubaliana na hoja yako moja kwa moja.
Nani yule, anauza unga wa ngano (AZAM). Kwa nini unga wa mahindi uwe shida?

Hakuna sababu hata ndogo kwa Tanzania kuuza mahindi Kenya. Kama ni mfanya biashara, weka mashine zako pale karibu na mpaka, nunua mahindi, saga kwa viwango vinavyotakiwa kwa bidhaa hiyo huko Kenya, package na nenda kasambaze kwenye supermarkets zao bidhaa zako. Shida ipo wapi

Mbali ya mahindi. Kwa nini tunaruhusu kuuza vitunguu kwa makampuni ya Kenya yanayo package na kuvisafirisha nje ya nchi hiyo kama bidhaa toka nchini humo. Hapa kwetu hatuna wafanya biashara wanaoweza kukusanya toka kwa wakulima, wakapackage' na kusafirisha nje kama bidhaa yetu, iliyotoka Tanzania?
Hawa wafanya biashara wetu wapiga kelele nyingi lakini akili ni kama zimelala.

Haya, sasa tunazungumza kuwauzia gesi, wakatengeneze umeme. Hivi hapa kwetu hatuwezi kuzalisha umeme na kuusafirisha hadi Kenya?

Tanzania tunayo matatizo makubwa!
 
Hayo makundi au vikundi vya ushirika vya manunuzi ya mazao tuna uzoefu nayo, kinachoendelea huko ni dhuluma na siasa zisizo na tija. Kama ww umepata soko linalokulipa nje, andika proposal nenda bank kopa hela kisha kanunue mzigo kwa wakulima fullstop. Mambo ya vikundi mwisho wake ni utapeli na kuleta siasa na Majungu kwenye mazao ya wakulima.
tindo. Hapana.

Ushirika unalipa sana, na ndio unaowainua waKenya hasa waliopo kwenye 'Horticulture'.

Na 'Horticulture' sasa hivi ndio inashika nafasi ya pili, nyuma ya 'diaspora' katika kuingiza hela za kigeni nchini humo.

Kuvurugika kwa hivyo vikundi kwa kukosa weledi sio sababu ya kuvikataa moja kwa moja. Serikali iweke taratibu za uendeshaji na usimamizi, pakiwa pamoja na sheria maalum zinazohusu ushirika huo ili ufanye kazi vizuri.
 
saa ingine wanahitaji mahindi ya kupika makande,au kutengeza chakula cha kuku,wewe unataka kuuwauzia unga,hawakubali
Mbona zote hizi ni fursa? Kwani makande si ni mahindi yaliyopondwapondwa tu. Chakula cha mifugo hakiwezi kutengenezwa hapa kikauzwa huko?
 
Mkuu japo naona kama unajibu jambo ambalo Bashe amelisema au kulianzisha pamoja na kwamba sijui ni nini na wewe huelezi....naunga mkono wakenya waende kwa wakulima kununua mahindi yao...hao walanguzi wa katikati ni wabaya sana na kuwagandamiza wakulima !!
Nadhani huyu bwana hajawahi kufanya biashara ya kilimo, hakuna watu wananyonya wakulima kama hawa watu wa kati yaani walanguzi hawa watu wakidhibitiwa wakulima wataneemeka sana, hawa walanguzi wanakula bila jasho lolote.

Kuna kipindi nilikuwa nafanya kilimo cha mpunga sasa walanguzi wao wakawa wanaunua guni la kilo 80 kwa elfu 70 wakenya wakija wanatoa laki moja hapo ndio utajua ni jinsi gani wakulima wanaibiwa.

Ushauri wangu kwa Mh. Bashe aangalie ni namna ya kuondoa hii kero ikiwezekana wizara ikutane na wakulima kama anavyofanya Mh. Raisi hii itasaidia kujua changamoto za wakulima na kuzipatia ufumbuzi,. Maisha ya kilanguzi tuliyoyazoea athari zake tumeziona kwenye korosho watu wanapanga kuwanyonya wananchi bahati mbaya wengine ni viongozi tulio wachagua wakatuwakilishe, Serikali ikiingilia wanahujumu. Kweny sekta ya kilimo ulanguzi ukidhibitiwa kilimo kinaweza changia ajiri nyingi sana na pato la taifa maana vijana wengi watakimbilia kilimo.
 
Jibu ni vyama vya ushirika ndio wawe na dhamana ya kununua nafaka zote na hao wakenya waende kwenye vyama vya ushirika.
Ni chama gani cha ushirika kwa sasa kinachofanya kazi na kina uwezo wa kununua mazao ya wakulima.

Kwa sasa, cha muhimu ni kuondoa barriers zote katika uzalishaji na uuzaji. Wakulima waneteseja sana. Serikali badala ya kuwasaidia wakulima, imekuwa ndiyo chanzo cha udunishaji wa wakulima.
 
Mahindi yauzwe kwa mfumo wa stakabdhi ghalani.Mkenya kwenda kwa mkulima ni kumuibia tu. Mifano ipo mingi, huko Mpwapwa Dodoma, kuna kata inaitwa Lumuma, maarufu kwa kilimo cha Kitunguu. Wakenya wanakwenda na sandarusi la 120kg, linakuwa regarded ni la 100Kg. Huko Lindi na Mtwara mfumo wa stakabadhi ghalani, umeonyesha mafanikio si tu kwa korosho bali hata kwa ufuta. Vinginevyo, NFRA wanunue kwa bei nzuri mahindi toka kwa wakulima halafu wao wauze Zimbabwe na nk.
Wanunuzi wote wawe huru kwenda kununua kwa mkulima. Mkulima ataamua wa kumuuzia. Masharti mengine yoyote yamethibitika kutokumsaidia mkulima.
 
Mtoa mada nadhan hukumsikia Bashe...mbn ulichoandika ndo bashe alikiongea hvyo?
 
Ni sawa, mzee Msekwa kwenye muktadha wa nyaraka alisema unaposhauri, sio sawa na kutoa amri. Mtu mwenye asie na mtoto wa kike hana power ya ku-dictate suala la mahari kwa kuwa hana mtoto wa kike.

Anyway, siongei kwa kushadadia, ila naweza kukupa mfano mdogo tu... PPF, LAPF, PSPF, GEPF (ambazo kwa sasa ni PSSSF) na NSSF ni jumuia/mifuko inapokea say elfu 40, 30, 100... mashirika ya bima wakati yanaanza premium zilikuwa ndogo sana elfu 25, 30.... wanasema law of large numbers.
Hao wakulima wadogo ndio wanailisha nchi hii na Kenya, Congo, Rwanda Burundi...
Inatakiwa ije mifumo tu ya kuwa-organize kwa wingi wa wanachovuna na Umoja wao wawe na command ya kukopesha na kumiliki processing machinery.
This is very very workable.

Huwezi kwenda India ukanunua maziwa kwa mkulima hata kama ana ng'ombe 5. Hatauza kwako. Wana organized system ya kuuza maziwa viwandani na kila mwenye maziwa ana share kiwandani.

It just a way of creating a system ambapo wakulima hao hao wa gunia 2, 6, 10 wanakuwa na mfumo ambao unawathamini ili wauze hizo gunia 2 zilizosindikwa na kuvuta kikubwa….

Anyway, mie tunashauri. Hatuna mamlaka wala vikao rasmi vya kumtaka Naibu Waziri au yeyote yule kufuata ushauri wangu. Ni ushauri tu
Ushauri wako ni mzuri lakini ni mapema sana kuufuata.
 
tindo. Hapana.

Ushirika unalipa sana, na ndio unaowainua waKenya hasa waliopo kwenye 'Horticulture'.

Na 'Horticulture' sasa hivi ndio inashika nafasi ya pili, nyuma ya 'diaspora' katika kuingiza hela za kigeni nchini humo.

Kuvurugika kwa hivyo vikundi kwa kukosa weledi sio sababu ya kuvikataa moja kwa moja. Serikali iweke taratibu za uendeshaji na usimamizi, pakiwa pamoja na sheria maalum zinazohusu ushirika huo ili ufanye kazi vizuri.

Sipingi usemacho ila naona unaongea mambo mazuri ya nadharia. Ni hivi, mimi ni mkulima sina muda wa hizo porojo za ushirika, navuna mazao yangu na kumuuzia mwenye pesa, mambo ya kupeleka mazao yangu kusimamiwa na watu wasio hata na bustani ya mchicha sina. Huna pesa kaa kushoto na mazao yangu, wakajiunge na ushirika wale wenye muda wa kupigiwa siasa mfu.
 
Nadhani huyu bwana hajawahi kufanya biashara ya kilimo, hakuna watu wananyonya wakulima kama hawa watu wa kati yaani walanguzi hawa watu wakidhibitiwa wakulima wataneemeka sana, hawa walanguzi wanakula bila jasho lolote.

Kuna kipindi nilikuwa nafanya kilimo cha mpunga sasa walanguzi wao wakawa wanaunua guni la kilo 80 kwa elfu 70 wakenya wakija wanatoa laki moja hapo ndio utajua ni jinsi gani wakulima wanaibiwa.

Ushauri wangu kwa Mh. Bashe aangalie ni namna ya kuondoa hii kero ikiwezekana wizara ikutane na wakulima kama anavyofanya Mh. Raisi hii itasaidia kujua changamoto za wakulima na kuzipatia ufumbuzi,. Maisha ya kilanguzi tuliyoyazoea athari zake tumeziona kwenye korosho watu wanapanga kuwanyonya wananchi bahati mbaya wengine ni viongozi tulio wachagua wakatuwakilishe, Serikali ikiingilia wanahujumu. Kweny sekta ya kilimo ulanguzi ukidhibitiwa kilimo kinaweza changia ajiri nyingi sana na pato la taifa maana vijana wengi watakimbilia kilimo.

Mahindi na Mpunga sio mazao ya biashara mkuu. Mkitaka wakulima mle wenyewe hela zote basi uzieni tu kwa mlaji wa mwisho anaeenda kupika kama inawezekana.

Maana hata wenye maduka ni wachuuzi pia, sasa unafikiri viwanda wananyonywa kuwauzia wenye maduka?
 
Back
Top Bottom