Leo 360 ya clouds tv wametendea haki u

Leo 360 ya clouds tv wametendea haki u

Time is time

Senior Member
Joined
Jul 17, 2013
Posts
180
Reaction score
36
360 Clouds leo mmenifrahisha sana kwa uchambuzi wa Gazeti flani lililohoji matumizi ya pesa za rambirambi Bukoba.

SAM:hivii zile pesa tungehimizwa kuchanga kwa ajili ya miundo mbinu ingekuwaje?
BABIE: aah...tungechanga tuuuu!!!!
SAM:Acha zako weweee...
SIMJUI: Kwani kitengo cha maafa ofisi ya waziri mkuu haina pesa?
SAM: Unajua watu walichomwa na hali halisi ya maisha wanayoishi wale wahanga ndo maana wakachanga, sasa huyu mkuu wa mkoaaaa........ Hahhaahaa
SIMJUI: Kwani tulipokuwa tunapiga chapuo kwa wananchi wachange tuliwaeleza kuwa ni za wahngaaaa miundo mbinu!?
BABIE:Lakini hii miundombinu ni kwa maslahi ya nani?
WOTE: "wananchi"
BABIESasa tatizo liko wapi?
SAM: skia baby, hivi kwanini serikali iliomba msaada kwa wasamaria?
Kwanini walitoa acount wachangiwee?
BABIE: walitaka kufanya msaada wa haraka kulingana na dharura ile..
SAM: sasa ikawaje tena pesa zielekee pengine?
SIMJUI: Au wale waliotengeneza acount feki walishajua mchezooooo nn!
WOTE: "Wanacheeeeeka

BABIE: Kwaiyo wahanga watafanyaje sasa!!
SAM: wanasubiri michango mingine ya wadau!
SIMJUI: Nani wakchanga tena!!
SAM: Kuna wimbo flani tumeuimba sana mwaka jana' hahaa
SIMJUI: Samahani jamani yawezekana mi ndo skuskia vizuri,
Hivi UINGEREZA walichanga sh ngapi vilee?
SAM :Bilion Sita.
BABIE:mbona mkuu wa mkoa katangaza bil 5.4 kama michango yoooote ya wadau
SAM: na imeshatumika 1.something,
SIMJUI: kwaiyo zimebaki 4.something?
BABIE:Ndioooo!!!!
SIMJUI: aaaah ...jamani mheshimiwa KIJUU!! Tafadhali baba...hivi huyu mtoto unaetaka kumjengea shule na barabara... Ataendaje iwapo ana njaa, kalala nje, hana nguo?
SAM: ataenda tu, maana mitoto nayo sku iz imekuwa mikorf ka nn, halafuuuu shuleni kuna amani kuliko home! Yes !!!
SIMJUI: Kwaiyooo yule MHINDI, Hakuchangia?
SAM: alichanga.
SIMJUI: Kenya je?
SAM: walipereka mabati na sement yawezekana yaliuzwa yakageuzwa pesa taslim.. Hahahaa
BABIE: Yoweri raisi wa Uganda?
SAM:Alileta...tena kaja mwenyewe na kesh kwenye begi...
SIMJUI: kwaiyo jumla ni sh ngapi?
SAM:Bilion 5.4
SIMJUI: Sam kuwa sirias ujue! Uingereza pekee si imetoa 6 bil ??
SAM: eeeh.....
BABIE: sasa inakuwaje 5.4 jamani.
SAM : Labda zimekatiwa bima!
BABIE: bimaaa!!!?
SIMJUI: Eeeeeh ....mbona sisi tumekata bima ya moto!!?

WOTE: "wanatizamanaaa.....
BABIE: hiviii...smahani hatuombei lakini tujiulize...
Ikitokea tena maafa tutapata moyo tena wa kuchangia wahanga?
SAM: Mtapata tu...
SIMJUI: me moyo ushapotea kabisa..
BABIE: hata mimi.
SAM: moyo ukipotea TUTAWAWEKEA BETRI ,mtachanga tu!!
WOTE: wanacheeeeeeeka....
SIMJUI:Jamani tukubali tukatae...mimi binafsi kw nafsi yangu sio 360, mi naona katika hiliiiii....mkuu wa mkoa ame...........
SAM: No!! Mkuu yuko sawa,
BABIE: Kivipi sam!!
SAM: Kasema hawatakosa kabisa,ila inabidi wasubiri awamu ya pili.
SIMJUI: Ipi sasa!
SAM: si ya wadau watakaojitokezaaa jamani!!!!
BABIE: kuchangia wahangaaa au miundombinu!!!
SAM: kwani mwanzo mmechangia nini!!?
WOTE: "wahangaaa"
SAM: Ndo ivo sasaaa!!! Bil 5.4 nyingine inatakiwa.
SIMJUI: Tutfikia kweli??
BABIE: Hata nusu yake tu ???
SAM: watanzania ni wakarimu bwanaa!!!
WOTE: wanacheeeeeeeeka.... Mwisho wanatupia kawimbo..
"Wachwa waisome namba eeeeeeh....ccm mbele kwa mbeleee......"
 
Taratiiibu naona vyombo vya habari kama vinaanza kujielewa. Hii yako sijaisikia,lakini baadhi ya vipindi na habari naona ile freedom of speech walau inadonoa.
 
Naona Ofisi ya Waziri Mkuu imetoa taarifa fasta ili kujibu malalamiko ya watu
 
KIUKWELI SIO KILA JAMBO LIFANYWALO NA SERIKALI NI ZURI KWA WANANCHI, HVI SERIKALI HAIJUI KAMA WANANCHI MAMBO MENGINE YANAWACHOSHA? AJIRA MPYA HAKUNA, WALIOSITISHIWA AJIRA HAWARUDISHWI, MIKOPO ELIMU JUU HAKNA, MASLAH YA WATUMISHI HAKNA USAWA,BADO HELA ZA WAHANGA KAGERA MPELEKE KWENYE MIUNDO MBINU TOFAUTI NA KUSUDIO LA WACHANGIAJI, MUNGU ANAWAINA NYIE JIFANYENI WABABE BASI! MWISHO WA VILIO VYA WA TZ UTAFIKA!
 
Duh hivi huwa wanaweka vipindi vyao YouTube hawa 360,kwa bandiko hilo nashawishika kutafuta hiyo video yake YouTube nijionee maana Sam chalii chalii sana
 
Watapona kweli??? Wasijeitwa wachochezi!!! Time will tell
 
Back
Top Bottom