kilimasera
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 3,068
- 268
Mbunge wa Kahama (CCM), James Lembeli, amesema anaishangaa serikali kuibuka na kuelezea hukumu ya Mahakama ya Kimataifa ya Migogoro ya Biashara (ICC) kwamba, imeliamuru Shirika la Umeme nchini (Tanesco) kuilipa kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Dowans Tanzania Limited mabilioni ya shilingi.
Amesema hukumu hiyo ina utata na imezua mkanganyiko mkubwa miongoni mwa Watanzania kwani hajawahi katika maisha yake kupata kusikia serikali ikiwaeleza wananchi kwamba, Dowans Tanzania Limited imeishtaki Tanesco mahakamani. Lembeli aliyasema hayo jana alipozungumza na NIPASHE jijini hapa kuhusiana na sakata la malipo kwa Dowans Tanzania Limited.
Alisema serikali makini lazima iwaarifu watu mapema mambo ya kitaifa yatakayowakabili ili baadaye kusiwe na maswali, kama ilivyokuwa enzi za Mwalimu Julius Nyerere.
Alisema kinachotokea sasa ni cha kusikitisha kuona viongozi wa serikali, wanatoa kauli tofauti kuhusu Dowans, hali inayomfanya mwananchi wa kawaida kuzidi kuchanganyikiwa, maana anashindwa ashike la nani na kuacha lipi.
Utasikia mara kampuni hii feki, mara vigogo wa serikali wanahusika na serikali imekaa kimya bila ufafanuzi. Jambo hilo ni baya na linaleta mkanganyiko kwa jamii, alisisitiza Lembeli.
Alisema kwa mfano kwenye suala la mgawo wa umeme, waziri husika aliutangazia umma kwamba, mgawo umekwisha, lakini baadaye lilipotokea tatizo, hakueleza kilichosababisha tatizo hilo kuendelea kinyemela na kusema jambo hilo linazidi kuchafua serikali na watu wake.
Kuhusu bei za gesi, alisema nayo hivyo hivyo, serikali imekaa kimya, badala ya kuwaeleza wananchi sababu za kupanda kwa nishati hiyo, huku wananchi wakilalamika kwamba, hawapewi majibu sahihi.
Alisema kitendo cha serikali kuendelea kukalia kimya masuala mazito ya taifa, ni cha hatari kwa siku za usoni, kwani kinaweza kusababissha mvurugano usio na sababu.
CHANZO: NIPASHE
Amesema hukumu hiyo ina utata na imezua mkanganyiko mkubwa miongoni mwa Watanzania kwani hajawahi katika maisha yake kupata kusikia serikali ikiwaeleza wananchi kwamba, Dowans Tanzania Limited imeishtaki Tanesco mahakamani. Lembeli aliyasema hayo jana alipozungumza na NIPASHE jijini hapa kuhusiana na sakata la malipo kwa Dowans Tanzania Limited.
Alisema serikali makini lazima iwaarifu watu mapema mambo ya kitaifa yatakayowakabili ili baadaye kusiwe na maswali, kama ilivyokuwa enzi za Mwalimu Julius Nyerere.
Alisema kinachotokea sasa ni cha kusikitisha kuona viongozi wa serikali, wanatoa kauli tofauti kuhusu Dowans, hali inayomfanya mwananchi wa kawaida kuzidi kuchanganyikiwa, maana anashindwa ashike la nani na kuacha lipi.
Utasikia mara kampuni hii feki, mara vigogo wa serikali wanahusika na serikali imekaa kimya bila ufafanuzi. Jambo hilo ni baya na linaleta mkanganyiko kwa jamii, alisisitiza Lembeli.
Alisema kwa mfano kwenye suala la mgawo wa umeme, waziri husika aliutangazia umma kwamba, mgawo umekwisha, lakini baadaye lilipotokea tatizo, hakueleza kilichosababisha tatizo hilo kuendelea kinyemela na kusema jambo hilo linazidi kuchafua serikali na watu wake.
Kuhusu bei za gesi, alisema nayo hivyo hivyo, serikali imekaa kimya, badala ya kuwaeleza wananchi sababu za kupanda kwa nishati hiyo, huku wananchi wakilalamika kwamba, hawapewi majibu sahihi.
Alisema kitendo cha serikali kuendelea kukalia kimya masuala mazito ya taifa, ni cha hatari kwa siku za usoni, kwani kinaweza kusababissha mvurugano usio na sababu.
CHANZO: NIPASHE