Mungi
JF Gold Member
- Sep 23, 2010
- 16,975
- 9,566
MBUNGE wa Arusha Mjini, Godbless Lema (Chadema), amedai kipigo alichokipata kutoka kwa Jeshi la Polisi mkoani hapa, wakiongozwa na Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Arusha (OCD), Zuberi Mombeji, ni matokeo aliyotarajia kutoka kwa Jeshi hilo siku nyingi, lakini hatarudi nyuma kudai haki za msingi na yuko tayari kufa.
Lema alipata kibano kutoka kwa polisi na kusekwa rumande katika Kituo Kikuu cha Polisi kwa madai ya kufanya vurugu ndani ya Ukumbi wa Manispaa wakati madiwani wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wakifanya uchaguzi wa kumchagua Meya wa Jiji la Arusha.
Akizungumza jana mjini hapa, Lema alidai ni siku nyingi OCD Mombeji alikuwa akimtafuta na alishawahi kumtamkia kuwa iko siku ataingia katika anga zake, hivyo kipigo alichopata juzi kutoka kwa Mkuu huyo wa Polisi Wilaya pamoja na askari wake, ni matokeo ya ahadi alizokuwa ameahidi kumshughulikia.
Alisema yuko tayari kufa kwa ajili ya kudai haki ya msingi ya wananchi wa Jimbo la Arusha kwa kuhakikisha Meya anachaguliwa kwa kufuata haki na kanuni za uchaguzi za halmashauri zilizowekwa na Serikali ya Chama Cha Mapinduzi na sio kupindisha kama walivyofanya juzi.
Alisema kanuni ziko wazi katika suala la akidi, Kifungu cha 8(3) kinaeleza bayana kuwa uchaguzi utafanyika kwa wajumbe (madiwani) kufika theluthi mbili na hilo ndilo tatizo kwa CCM wako 17 pamoja na diwani wa TLP, lakini sheria inakinzana na hilo na ili uchaguzi ufanyike lazima kuwe na wajumbe zaidi ya 21.
Lema alisema hawezi kumtambua wala kumuunga mkono Meya aliyechaguliwa na CCM, Gaudence Lyimo pamoja na Naibu Meya wake wa chama cha TLP, Michael Kivuyo, kwani hawakuchaguliwa kihalali.
Kesho (leo) tutaonana na wanasheria wa Chadema kuangalia hatua gani za kisheria zichukuliwe juu ya kumpinga meya huyo katika vyombo vya sheria na pia tutautangazia umma kuwa Mkurugenzi wa Jiji la Arusha, Estomi Changah anapaswa kulaaniwa kwa kukiuka sheria kwa makusudi, alisema mbunge huyo.
Akizungumzia kitendo cha Kivuyo kuwaacha solemba dakika za mwisho, alisema kinapaswa kulaaniwa na kuwataka wakazi wa Kata ya Sokoni One kumjua kwa kina diwani wao, aliyedai ameanza kazi kwa usaliti.
Lema alisema Kivuyo ni msaliti wa kupindukia na anapaswa kuelezwa kwa umma ni namna gani alivyoamua kufanya umafia katika dakika za mwisho na kukimbilia CCM na kuambulia kupewa Unaibu Meya.
Alisema Chadema katika Uchaguzi Mkuu iliamua kwa makusudi kutosimamisha mgombea katika kata hiyo kwa kumheshimu kuwa ni mpinzani wa kweli na anapaswa kuungwa mkono kumbe tulibeba chatu ndani ya gunia.
Kwa upande wake, Kivuyo akizungumza kwa simu, alisema Chadema wamepagawa na hawajui wanaloongea kwani kwenda kwake katika ukumbi na CCM kumchagua, sio kwamba amesaliti chama hicho.
Kivuyo alisema kinachopaswa kufanywa na Chadema ni kufuata taratibu za kisheria na sio kuleta vurugu na kutuhumiana kwani huo sio wakati muafaka kwa sasa.
Alisema kanuni ziko wazi na hata kipofu anajua hilo na kinachopaswa kufanywa na Chadema ni kwenda katika vyombo vya sheria na sio kuleta vurugu na kupayuka ovyo barabarani.
Meya amechaguliwa kinyume na kanuni na hata mimi nimechaguliwa kinyume na kanuni sasa Chadema wanalia nini? Sheria si ziko wazi, mahakama zipo kwa ajili ya watu wafuate taratibu kudai haki zao za msingi na sio kulaumu watu eti nimenunuliwa? alisema Diwani huyo wa Sokoni One.
Lema alipata kibano kutoka kwa polisi na kusekwa rumande katika Kituo Kikuu cha Polisi kwa madai ya kufanya vurugu ndani ya Ukumbi wa Manispaa wakati madiwani wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wakifanya uchaguzi wa kumchagua Meya wa Jiji la Arusha.
Akizungumza jana mjini hapa, Lema alidai ni siku nyingi OCD Mombeji alikuwa akimtafuta na alishawahi kumtamkia kuwa iko siku ataingia katika anga zake, hivyo kipigo alichopata juzi kutoka kwa Mkuu huyo wa Polisi Wilaya pamoja na askari wake, ni matokeo ya ahadi alizokuwa ameahidi kumshughulikia.
Alisema yuko tayari kufa kwa ajili ya kudai haki ya msingi ya wananchi wa Jimbo la Arusha kwa kuhakikisha Meya anachaguliwa kwa kufuata haki na kanuni za uchaguzi za halmashauri zilizowekwa na Serikali ya Chama Cha Mapinduzi na sio kupindisha kama walivyofanya juzi.
Alisema kanuni ziko wazi katika suala la akidi, Kifungu cha 8(3) kinaeleza bayana kuwa uchaguzi utafanyika kwa wajumbe (madiwani) kufika theluthi mbili na hilo ndilo tatizo kwa CCM wako 17 pamoja na diwani wa TLP, lakini sheria inakinzana na hilo na ili uchaguzi ufanyike lazima kuwe na wajumbe zaidi ya 21.
Lema alisema hawezi kumtambua wala kumuunga mkono Meya aliyechaguliwa na CCM, Gaudence Lyimo pamoja na Naibu Meya wake wa chama cha TLP, Michael Kivuyo, kwani hawakuchaguliwa kihalali.
Kesho (leo) tutaonana na wanasheria wa Chadema kuangalia hatua gani za kisheria zichukuliwe juu ya kumpinga meya huyo katika vyombo vya sheria na pia tutautangazia umma kuwa Mkurugenzi wa Jiji la Arusha, Estomi Changah anapaswa kulaaniwa kwa kukiuka sheria kwa makusudi, alisema mbunge huyo.
Akizungumzia kitendo cha Kivuyo kuwaacha solemba dakika za mwisho, alisema kinapaswa kulaaniwa na kuwataka wakazi wa Kata ya Sokoni One kumjua kwa kina diwani wao, aliyedai ameanza kazi kwa usaliti.
Lema alisema Kivuyo ni msaliti wa kupindukia na anapaswa kuelezwa kwa umma ni namna gani alivyoamua kufanya umafia katika dakika za mwisho na kukimbilia CCM na kuambulia kupewa Unaibu Meya.
Alisema Chadema katika Uchaguzi Mkuu iliamua kwa makusudi kutosimamisha mgombea katika kata hiyo kwa kumheshimu kuwa ni mpinzani wa kweli na anapaswa kuungwa mkono kumbe tulibeba chatu ndani ya gunia.
Kwa upande wake, Kivuyo akizungumza kwa simu, alisema Chadema wamepagawa na hawajui wanaloongea kwani kwenda kwake katika ukumbi na CCM kumchagua, sio kwamba amesaliti chama hicho.
Kivuyo alisema kinachopaswa kufanywa na Chadema ni kufuata taratibu za kisheria na sio kuleta vurugu na kutuhumiana kwani huo sio wakati muafaka kwa sasa.
Alisema kanuni ziko wazi na hata kipofu anajua hilo na kinachopaswa kufanywa na Chadema ni kwenda katika vyombo vya sheria na sio kuleta vurugu na kupayuka ovyo barabarani.
Meya amechaguliwa kinyume na kanuni na hata mimi nimechaguliwa kinyume na kanuni sasa Chadema wanalia nini? Sheria si ziko wazi, mahakama zipo kwa ajili ya watu wafuate taratibu kudai haki zao za msingi na sio kulaumu watu eti nimenunuliwa? alisema Diwani huyo wa Sokoni One.