VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,140
- 18,004
Godbless Lema anapendwa jamani. Kaeni msikie tu,wengine tumejionea. Jana nilishindwa kuhudhuria kwenye kesi ya mteja wangu Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha.Nilijikuta nimefika viunga vya Mahakama Kuu(kwakuwa Mahakama ya Rufani nayo uliketi humo jana) kushuhudia na kusikiliza kusikilizwa kwa Rufaa ya Mbunge huyo wa zamani wa Arusha Mjini.
Kwakuwa katika Rufaa hiyo kumewasilishwa Pingamizi la Awali kuwa Rufaa ni batili,Mahakama ya Rufaa jana ilianza kusikiliza pingamizi hilo kama inavyopasa. Pingamizi liliwekwa na upande wa Wajibu Rufaa ukioongozwa na Mawakili Wasomi Alute Mughwai na Akida. Kwa siku itakayopangwa,kutatolewa uamuzi wa pingamizi hilo baada ya maelezo juu ya suala hilo kutolewa jana Mahakamani hapo. Uamuzi huo wa pingamizi utafanya Rufaa ya Lema iendelee au isiendelee. Ni hivi,kama pingamizi litakubaliwa rufaa itatupwa yote. Kama pingamizi likitupwa,usikilizaji wa Rufaa utaanza.
Godbless Lema,kwa hapa Arusha,hufananishwa na Malema wa Afrika Kusini. Eti kwakuwa wote ni 'vipenzi' wa vijana nchini mwao. Lakini,kadiri nimjuavyo Malema wa kwa Mandela na Lema wa Tanzania,Lema yuko juu. Arusha nzima ilisimama jana.Mimi nisiwe msemaji sana.Ujumbe wangu ni kuwa Lema ni kiboko. Wana-Arusha bado wanamhitaji sana. 'God bless our King' wameandika bangoni wana-Arusha.
Kwakuwa katika Rufaa hiyo kumewasilishwa Pingamizi la Awali kuwa Rufaa ni batili,Mahakama ya Rufaa jana ilianza kusikiliza pingamizi hilo kama inavyopasa. Pingamizi liliwekwa na upande wa Wajibu Rufaa ukioongozwa na Mawakili Wasomi Alute Mughwai na Akida. Kwa siku itakayopangwa,kutatolewa uamuzi wa pingamizi hilo baada ya maelezo juu ya suala hilo kutolewa jana Mahakamani hapo. Uamuzi huo wa pingamizi utafanya Rufaa ya Lema iendelee au isiendelee. Ni hivi,kama pingamizi litakubaliwa rufaa itatupwa yote. Kama pingamizi likitupwa,usikilizaji wa Rufaa utaanza.
Godbless Lema,kwa hapa Arusha,hufananishwa na Malema wa Afrika Kusini. Eti kwakuwa wote ni 'vipenzi' wa vijana nchini mwao. Lakini,kadiri nimjuavyo Malema wa kwa Mandela na Lema wa Tanzania,Lema yuko juu. Arusha nzima ilisimama jana.Mimi nisiwe msemaji sana.Ujumbe wangu ni kuwa Lema ni kiboko. Wana-Arusha bado wanamhitaji sana. 'God bless our King' wameandika bangoni wana-Arusha.