1. Mwanafunzi aliyebakwa jina tunalihifadhi (umri 16), yeye ni Yatima, ana dada umri (20)
2. Shule anaposoma, ni Turian Sekondari – ipo Magomeni Jijini Dar es salaam, anakaa Gongolamboto, mwisho wa lami jijini Dar, majirani wapo wanajua
3. Rafiki wa Mwanafunzi aliyempeleka kwa baba yake ni mtoto wa aliyekuwa Diwani wa Sinza, Mwaking'inda, na Mwaking'inda ndio alimpeleka kwa Kapuya ili awe anamsaidia Ada
4. Kapuya amemsaidia Ada kwa masharti ya ngono bila kujali umri, na kwa mara ya kwanza akamfanya akiwa na bastola kwa malipo ya laki 7, mara ya pili ofisini kwake kwa malipo ya laki tatu na nusu baada ya mtoto kukataa kwenda hotelini akikumbuka alichofanyiwa mara ya kwanza, na akidhani ofisini ni salama lakini akafanywa kwenye kapeti, akatoka kwa huzuni, Mama wa mapokezi alipomwangalia akamhurumia akamhoji alipojieleza ndio Yule mama wa mapokezi akaanza kulia na kumhurumia huku akimwarifu kuwa jamaa ni mwathirika, mwanafunzi huyo anapiga kelele anakamatwa na walinzi na kupelekwa kituo kidogo cha polisi Mango Garden, kujieleza kuwa kabakwa ndio wakampeleka Oysterbay Kituo kikubwa, huko jamaa anaitwa kistaarabu wanayamaliza kwenye dawati la jinsia kisha akaandika na kuweka sahihi kuwa atakuwa analipa laki 3 kila mwezi, na amekuwa akitekeleza hili kupitia simu namba 0755993930. Anaweza kuulizwa alikuwa anamsaidia kama yatima au kama nani? Je kwanini alimpa gari T199 BGY, Marcedes Benzi ili atulie kwa kuwa yeye atakuwa Waziri Mkuu ajaye hivyo CV yake itachafuka baada ya 2015?
5. Kufuatia kupeleka Benzi ndio watoto wanamshitukia anataka kukwepa wajibu wa kulipa kila mwezi, wakataka kumpeleka Mahakamani, polisi wa Oysterbay wakafanya tena "ustaarabu" kuomba busara ya Katibu wa Bunge, na katibu wa Bunge ili kuonyesha ana busara zaidi kuliko kuruhusu watoto hawa, mwathirika na dada yake waende mahakamani anawaita Bungeni, amewakalisha Dodoma wiki mbili, akiwapatia usafiri na Malazi ili wamsubiri Kapuya aje wayamalize. Imeshindikana, Bunge limeisha wamepewa gari kuja Dar, taratibu zote zilifanywa chini ya msaidizi wa Kashilila anaitwa Mpanda
6. Kabla hawajaja Dar kwa maelekezo yaliyotolewa na Mwigulu Nchemba, aliyewapigia watoto hawa simu na kuwaandikia ujumbe mfupi wasiongee na waandishi jambo hilo litajulikana, alitumia simu yake 0714-008888, na aliwaandikia ujumbe mara 4. 6/11/2013, saa 7:25 mchana akitoa taarifa yupo kwenye kikao asubiriwe, 5/11/2013 saa 10:17 alasiri akiuliza kama watoto wamempigia Kapuya akubali wayamalize au bado?, 5/11/2013, saa 2:11 asubuhi akiwa singida, anamwarifu kwa ujumbe mtoto huyo, "ngoja nakuja leo tuongee" ingawa siku hiyo hiyo saa 12:00 Asb, alimwandikia Yule mtoto "je Umempigia Kapuya Simu?.
7. Watoto walikuja Dar kwa ushauri wa Mwigulu ili waweze kuonana na Philip mangula, walipomkosa walionana na Katibu Mkuu wa CCM , Kinana, na aliwajibu kuwa masuala ya kubaka ni ya mtu binafsi sio ya Chama, ni katika hilo mtoto anatoka analia, hakuridhika alipofika nje alitonywa na wanafunzi mwingine kuwa wale watu wanajadiliana kukuogesha maji yaliyo katika chupa (yawezekana tindikali), akakimbia akapotea kabla haokotwa na wasamaria na kufikishwa kwa waandishi wa habari. Akiwa tayari kwa waandishi wa habari, Mtu aliyewapeleka kwa Kinana kwa jina anaitwa Rehema Nchimbi, kupitia simu yake 0784886090, saa 6:43 Mchana amewatumia ujumbe "wewe mwanangu, nakupenda sana, nakuomba usiende kukashifu CCM elezea tu udhaifu wake nakuahidi tupo pamoja", na dakika nne baadaye 6:47 anamwandikia "naona hutaki kunielewa, sina la kufanya".
8. Licha ya hawa walioko Dar es Salaam, watoto hawa wakiwa Dodoma bungeni wamefanya vikao mbalimbali na spika na baadhi ya Wabunge, na huyu mwenye hii namba 0787597494, tarehe 18/10/2013 anaandika (……………jina la mtoto.) "kama mama niliamua kuwasaidia na pia kumsitiri mbunge mwenzangu, lakini mmeona jilivyojitahidi kifedha, muda wangu na uezo wangu, matokeo yake kapuya anaona mimi mzushi, muongo. Sina ninalofaidika ilikuwa roho yangu ya hurumasasa naomba kuanzia sasa msinihusishe na lololte kwani sipendi kuingia katika matatizo, kila la heri wanangu".
9. Wengine wanaotajwa kulijua hili kwa undani ni Spika mwenyewe, Lembeli, Rage, na mwingine aliyeweza kuguswa hadi akawapa pesa ya kujikimu nambayake (0715------39, Aliwatumia pesa katika simu yao saa 10:43, ujumbe wa tigo ni pp131030.1643.E.04731
10. MNYONGE MNYONGENI, HAKI YAKE MPENI…CCM wanajua jambo hili kwa undani, wanamlinda Kapuya ili kesi ya Ubakaji isimkute, na sasa anajitahidi kuwahi mahakamani awashtaki watoto hawa ili kesi ya msingi isisikilizwe. Nini maana ya neno haki katika Tanzania??????????