@Phillemon Mikael, ahsante sana kwa salamu kutoka kwa Bashe.
Kuhusu suala la Uraia, hilo ni la kisheria na lilishaisha. Bora mimi niliyefanyiwa uchunguzi na kuthibitishwa kuwa ni Mtanzania halisi nisiye na shaka, kwangu hilo limeisha for good...sijui kama na wewe ulishafanyiwa uchunguzi au bado, maanake kama bado ujue hatuna uhakika na uraia wako! Pengine wewe ni msomali, au Mkenya sijui ni Taifa gani? Na kuna siku ukigombea tu watu wataibuka na hiyo kashfa yako ya Uraia...
@Matola, ninaamini wewe ni mtu mwenye upeo mkubwa sana wa kuelewa mambo na sikutegemei kwa kuwa una itikadi tofauti ya chama na ya kisiasa basi ndo uwe unawatukana wanaotofautiana na wewe na hata taasisi nyingine ambazo zipo kisheria, zinafanya kazi nzuri na zaidi pengine hata hujui zinafanya nini! WAMA ni taasisi inayotoa misaada tu kwa akinamama na watoto wa Tanzania na haina chembe ya utapeli, wewe nikikuuliza una taarifa gani ya utapeli wa WAMA utakuwa hauna...basi tu kwa kuwa ina uhusiano na mke wa kiongozi wa CCM, na wewe huipendi CCM basi ushaitukana na kuipa majina...its not fair na wala tabia za aina hiyo haziendani na watu wenye weledi!
Pili nilishawahi kupambanua kuhusu mahusiano yangu na WAMA na ulichokiandika hapa wala siyo...uwe unasoma threads au unafanya utafiti kabla haujakurupuka tu n issues...
[B said:Originally Posted by Mwawad[/B]o]
Kwangu mimi namchukulia Lazaro Nyalandu kama ni kiongozi mzuri ukilinganisha na viongozi wengi waliopo katika serikali yetu.Kama binadamu wengine,Hon.Nyalandu hajakamilika ana mapungufu mengi,lakini bado ni mtu mwenye mapenzi na Nchi yake na kama akipata muongozo mzuri ni kiongozi mzuri...kwa sasa na siku za baadaye kwa maana ya kwamba ni msikilizaji,mbunifu na mpenda kujifunza mambo mapya.
Hon.Nyalandu hana Elimu ya shahada kama inavyojulikana na wengi,alisoma elimu ya sekondari O'Level Kibaha (Pwani) na baadaye kwenda Ilboru (Arusha) kwa elimu ya A'Level,baada ya kumaliza elimu ya sekondari alikwepa kwenda Jeshini (JKT) na kujikita katika mambo ya UKWATA ambako alifikia level ya kuwa mwenyekiti wa Ukwata Tanzania.Kipindi hicho Lazaro alijihusisha na Viongozi wengi na watu wengi mashuhuri wa mji wa Dar-es-salaam na kufanikiwa kupata contact ya kupeleka wanafunzi USA kwa njia za makanisa,wanafunzi hao wengi walikwenda kwenye majimbo ya Michigan,Minnesota na Iowa.Alikuwa mmoja kati ya watu wengi waliokuwa wanatafuta I-20 katika vyuo vya Marekani na kuziuza kwa Vijana wengi waliokuwa wanamaliza shule na kukosa nafasi za vyuo vikuu nyumbani.Katika kufanya zoezi hilo alifanikiwa kuwapatia watoto wengi wa Viongozi serikali I-20,kwani watoto wa wakulima (Walalahoi) hawakuweza kumudu kununua I-20 hizo.Kwa kufanya hivyo aliweza kupata contacts za Wazee wa watoto hao na kuangukia kumfahamu Mama Mkapa kwani baadhi ya ndugu wa Mama huyo walipata Vyuo USA kwa kupitia Lazaro.Kwa mtu yeyote mwenye umri mkubwa na anayejali maadili ya Kitanzania akikutana na Lazaro atampenda.Ni mnyenyekevu,msikivu na mwenye haiba ya kuvutia.
Hon.Nyalandu baada ya kushughulika na I-20 kwa muda mrefu nae alikwenda Marekani kwa ajili ya masomo ya shahada yake,kama walivyo Watanzania aliowapatia I-20,Nyalandu alikwenda katika Jimbo la Iowa mji uitwao Forest City na alisoma Chuo kiitwacho Waldorf,Chuo hicho kilisoma Watanzania wengi na wengi waliendeleza kujishughulisha na maswala ya dini na masomo,hali hiyo iliwavutia walimu na watu wengi waliosoma katika chuo hicho.Hon.Nyalandu kwa kutumia uwezo wake,na uwezo wa kuleta wanafunzi wengi katika chuo hicho,alimuunganisha Mama Mkapa na Utawala wa Chuo na Mama huyo kupatiwa Shahada ya Heshima katika Chuo hicho.Hon.Nyalandu aliendelea kuunganisha watu wa Iowa na Asasi binafsi mbalimbali za maendeleo Tanzania na haswa Singida.Kwa kutumia Dini na kujulikana Nyalandu aliweza kushiriki katika NGO inayoitwa Books of Africa ambayo ilikuwa inakusanya vitabu mbalimbali vilivyotumika katika majimbo ya Iowa na Minnesota na kuvipeleka Afrika (Tanzania) haswa Kilimanjaro na Singida.Mama Mkapa,Nyalandu na baadhi ya ndugu wa Mama Mkapa kwa vipindi tofauti wamewahi kuwa Board Members katika Books of Africa.
Mheshimiwa Nyalandu hakumaliza shule yake huko Waldorf na inasemekana pia alikuwa na kesi ya kumbaka mwanafunzi wa Kike wa Zimbabwe alipokuwa anasoma huko,lakini si kweli kwamba amezuiwa kuingia Marekani,alikuja Marekani mara ya mwisho 2009 kuhudhuria harusi ya ndugu yake ambaye anaishi Minneapolis,Minnesota.
Si kweli kwamba Hon.Nyalandu amewekwa na watu wa Marekani ktk Uongozi wa juu katika Tanzania,Nyalandu amefanikiwa kupata Ubunge kwa juhudi binafsi za Mama Mkapa ambaye amefanya nae kazi kama katibu wake na anamchukulia kama mtoto wake,pia ameishi kwa karibu na watoto wa Mama Mkapa na ndugu zake ambao walisoma Minneapolis huko Minnesota.Kwa kupitia NGO's na Waldorf College Hon.Nyalandu anafahamiana na Senators Chuck Grassley kutoka Iowa na Norm Coleman kutoka Minnesota,Rais na Mwalimu wa Chuo kikuu cha St.Thomas Minnesota Father Dennis Dease pia ni mtu wa karibu na Hon.Nyalandu,ikumbukwe kuwa Rais Kikwete 2009 alikwenda St.Thomas kutunukiwa shahada juhudi hizo na nyingine zinatokana na watu kama Nyalandu.Kwa maana hiyo si taabu kwa Mh.Nyalandu kupata viza au kwenda Ubalozi wa Marekani Tanzania kwa ajili ya kupata information mbalimbali kutoka USA.
Umaarufu wa Nyalandu unaongezwa na kumuoa Faraja Kota (Former Miss Tanzania).Mzazi wa Faraja (Baba) ambaye ni marehemu amewahi kuwa mtumishi aliyetukuka katika Jeshi la wananchi wa Tanzania (Brigedia Jenerali mstaafu William Kota).Wazazi wote wawili wa Faraja ni marehemu.
Nyalandu alikuwa mmoja kati ya Wabunge wachache waliokataa kwa nguvu zote kuujadili mjadala wa mahakama ya Kadhi Bungeni,pia mwaka jana alisimamia kidete kutokuiruhusu serikali kuiruhusu Zanzibar kuingia ktk Jumuiya ya Nchi za kiislamu (OIC).Pamoja na mambo mengine ya udhaifu wa kibinadamu wa kupenda sifa na kupenda mabinti,bado Lazaro namchukulia kuwa ni kiongozi mzuri kuliko viongozi wengi katika Cabinet tuliyonayo.Tumjadili kwa utendaji kazi wake,na punde akivuruga tuseme madhambi yake kama ilivyokuwa kwa Masha.
Hana cha uchapakazi ni kwamba hakuamini kupata uwaziri. amekuwa akisubiri uwaziri miaka yote hivyo anajitahidi kumu impress Mkwere. Anajitia mlokole lakini hakuna kitu ni malaya kwanza alimdanganya mtoto wa mchungaji Haule wa Arusha kwamba atamuoa lakini wapi. Binti alikuwa anafanya kazi Zain Arusha. Currently ni board member wa TANAPA na AICC. Anapenda sana pesa huyu kijana.
Ni kweli kabisa, jamaa alimuahidi pia kumuoa mtoto wa Brig. Jen. Kisinda ambaye sasa hivi ni hakimu wakati huo mtoto wa watu alikuwa anasoma sheria Tumaini Iringa lakini akamtosa mbayaa baada ya kumpata Faraja Kota. Ila kwa uchapa kazi jamaa ni noma, anapiga sana mzigo hapo lazima tuseme. Ufisadi mmmhhhhhh inawezekana, uongozi inadaiwa anajiandalia mazingira ya uwaziri mkuu 2015, Pesa anayo ya nguvu wala si ya kitoto.
Duh jamani, na mimi nipo tena hapa...kwa CHE NKAPA...too paranoic, my brothers and sisters...
Ukisoma kwa makini utaona mengi ya yaliyoandikwa ni majungu tu.Mwingine anasema Nyalandu ana mawasiliano ya moja kwa moja na ma senators wengi wa Marekani,mpaka wabunge wenzake wanamshangaaa,maana si kawaida.Na tena anaweza kwenda ubalozi wa Marekani muda wowote anaoutaka.Eti ni mtu wamarekani,anayetumikia maslahi ya Marekani.
Wakati wengine wanasema,Nyalandu ni wanted huko Marekani,na hawezi kutia mguu wake.Sasa which is which?Halafu unajiita msomi wa Masters wakati ni mpika mijungu tuu,no wonder mnapewa contacts famba
Tuache wivu wabongo,Tujitume
Ni kiongozi wa serikali ambaye haruhusiwi kuingia US. Vyombo vya habari mna wajibu wa kuielimisha jamii, ni kwa nini kazuiwa kuingia US? ahhaha hahaha ana RB ya US. Vyombo vya habari, muulizeni kwa nini hatakiwi kukanyaga kwa Obama?
....hahaaaa....nilikuwa naye darasa moja kibaha school.....tulikuwa tu streams tofauti, yeye alikuwa stream B...alikuwa anakaa Kibo House...Umesahau kitu, alikua anapenda sana ngoma,kwaya na kua karubu na walimu, uwezo wake darasani aukua mzuri, social activities alikua mzuri.Nilikua kibaha o level na A level darasa moja nyuma yake.Jamaa angefit sana wizara ya utamaduni