Lazaro Nyalandu, kinyongo cha Uwaziri kitakuponza

Haya umemsema Lazaro Nyalandu kwakuwa tu hivi majuzi ameenda kumtembelea Tundu Lissu Hospitalini kuwa ana hasira ya kukosa Cheo katika Serikali ya Rais Magufuli na je vipi kwa Jaji Mstaafu Mzee Chande Othman ambaye na yeye juzi pia alimtembelea Tundu Lissu Hospitali?

Wewe ndiyo mmoja wa wale wana CCM ' Wapumbavu ' na wenye roho mbaya iliyojaa ' Ukatili ' hata wa kumzidi Muasisi wa ' Ukatili ' duniani ' Gaidi ' Osama Bin Laden. Na kama CCM yetu itaendelea kuwa na Watu ' makatili ' kama Wewe mwaka 2020 Kazi tunayo kwani nyie ndiyo mtakuwa ' alama ' Kuu ya chukizo la Wananchi Kwetu ( namaanisha CCM )

Halafu nikuonye tu kwamba wakati ' ukiwashwawashwa ' kumsema Lazaro Nyalandu kuwa ni mmoja wa ' Mafisadi ' au Watu walioiibia hii nchi jitahidi uwe na kumbukumbu nzuri kwani kuna Viongozi wako hapo tena wanatoka katika hiki hiki Chama chetu Tawala cha CCM ambao ni ' Mafisadi ' wakubwa na ndiyo hao hao wameifilisi nchi hii vibaya mno tokea miaka ya 90 hadi 2000 hapo mbona nao hujawasema? au huwajui? au unawaogopa?

Mimi ni Mwana CCM mwenzio na ' nakuchana ' mubashara / live kuwa acha kuwa na roho ya Kimasikini kama hiyo uliyonayo. Lililomtokea Tundu Lissu laweza kumtokea Mwanasiasa yoyote hata aliye Kwetu huku CCM? Pumbavu kweli Wewe tena ndiyo umenipandisha hasira na umeshaniharibia asubuhi yangu.

Mbona wanapougua Viongozi wetu wa CCM hawa hawa Watu wa CHADEMA huwa wanaenda kuwajulia hali huko Mahospitalini? Hivi leo Tanzania tumefikia hatua kwamba hadi Mtanzania mwenzetu wa Chama fulani akiugua basi Wewe wa Chama fulani hutakiwi kwenda na kama ukienda unaambiwa ' Msaliti ' au unaambiwa una ' Kisirani ' cha kukosa wadhifa / madaraka fulani?

Hakuna Member aliyenitibua ' akili ' zangu leo kama Wewe na nitaomba wana CHADEMA wasipoteze muda wao kukujibu ila waniachie Mimi mwana CCM mwenzako nikunyooshe vizuri humu ili siku zingine ujifunze kujua kwamba katika shida au tatizo lolote Watanzani huwa tunaungana na kuwa Mtu mmoja.

Najua utarudi tu sasa nakusubiri ili nikushushie rasmi ICBM langu la kisawasawa. Umenikera kunakotukuka asubuhi hii.
Heshima yako mkuu
 
Kama kumtembelea mgonjwa ni kinyongo, kama kuwahudumia watoto wa Lucky Vincent ni kinyongo na kama kusema ukweli ni kinyongo, basi acha aendelee nacho kinaonekana ni kinyongo kizuri kinachompendeza Mungu, kuliko kinyongo cha Sizonje na Bashite cha kutumia risasi na kuwaweka mahabusu wale (Manji) walio na kinyongo nao.
Mkuu yaani hawa watu wana roho mbaya kuliko wachawi. Sababu ya yote haya ni kitendo chake cha kwenda kumuona mbunge mwenzie wa Singida hapo Nairobi. Wanajaa chuki kiasi cha kupasuka, kama alivyo sema bwana wao kuwa anahesabu kuwa huo ni usaliti. Nina hakika kabisa wakimchunguza vizuri lazima hana asili ya Tanzania yule! kwa asili wa TZ wamezaliwa na kaupendo Fulani hivi.
 
Hamad Tundu Lissu akapata matatizo ya kupigwa Risasi,
Ghafla Nyarandu akaibukia Nairobi kumtembelea Tundu Lissu na kutoa kauli tata akiwa na Wabunge wa CHADEMA.

Kashifa zoooote hizi kwa Lazaro Nyalandu zinasababishwa na roho yake nzuri isiyo na mawaa ya udikteta, ukanda, ukada wa ccm na ukabila ndiyo maana akaenda kushughulika kuokoa maisha ya watoto wa Lucky Vincent na sasa ameenda kwa Tundu Lissu.

Mpaka wale watoto wanarudi na kupokelewa Kwa Sherehe pale KIA hakuna Pongezi toka Kwa waziri yeyote , Waziri mkuu, CCM wala Rais Magufuli Kwenda Lazaro Nyarandu. Walijua janja yake.

Pole sana wewe na hao uliowataja wenye kujaa chuki, roho mbaya na choyo. Wenye kumuabudu na kumuogopa dikteta uchwara utadhani mungu wao.
 
Wewe ni lijinga sana,ulitaka ajipendekeze kwa huyo baba yako?siku hizi ukifanya kitu kivyako eti una kinyongo na serikali.
 
Kwenda kumpa pole Lissu ni kinyongo cha uwaziri?
Ama kweli ccm ni wanafiki.
Yaani figisu zimeanza...
 
si useme ty hamruhusiw kwenda kumuona lissu sio unazunguka tu mbuyu
 
Lazaro Nyarandu mbunge wa Singida ametajwa kuwa na kinyongo cha kupitiliza Kutokana na kutoswa Kwenye Uwaziri Kwenye serikali ya awamu ya tano imebainika. Kati ya mawaziri wa Kikwete wanaoumia huyu bwana anashika nafasi ya kwanza. Baada ya serikali ya awamu ya tano kuingia madarakani na Nyarandu kutoingizwa Kwenye Baraza la mawaziri lá Magufuli, huyu bwana alisuka mkakati kuwashawishi Maseneta 7 wa Marekani kuja Tanzania kuonana na Rais Magufuli kuzungumza masuala yanayotajwa ya Kimaendeleo na kumshawishi Rais amteue Nyarandu Kwenye Wizara ya Maliasili ili Marekani iendelee kushirikiana na Tanzania Kwa kutoa misaada ya vifaa vya kudhibiti ujangili nchini. Mtakumbuka Rais Magufuli aligundua janja hiyo anakataa kuonana na hao wazungu wa Marekani badala yake alielekeza wakaonane na Spika Ndugai Waeleze mambo yao. Kitendo chá Maseneta hao waliokuja na Ndege binafsi kutomuona Rais kiliwakatisha tamaa sana Kwakuwa Ndugai hakuwa mlengwa.
Hata Wakati wa kikwete kumpandisha Nyarandu kuwa Waziri baada ya kujiuzulu Kagasheki ilikuwa ni Shinikizo la Western power, hii iliwahi kuripotiwa na Gazeti Jamhuri mara kadhaa.

Marekani wanamtaka Nyarandu Kwa sababu za maslahi ya Vitalu vya uwindaji na masuala yote yanayohusiana na bidhaa za wanyama Pori . Huyu ni mtu Pekee aliyeweza kucheza fitina zote kuwaridhisha Matajiri wa kimarekani Kwa kukana maslahi ya taifa lake.

Mdogo wake Nyarandu nimesoma Naye sheria tukiwa darasa moja na hadi leo tuko karibu sana, Pamoja na kutomkubali Kaka yake Kwa madai kwamba hana msaada kwa ndugu zake, Anaeleza jinsi Nyarandu alivyokuwa na matumaini ya kurejea Kwenye uwaziri baada ya uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 akiamini ana nguvu kubwa nyuma yake. Kwahiyo kitendo chá kuachwa mazima kimjengea kinyongo kupita maelezo na amenukuliwa akimnanga Rais Magufuli na Rc Makonda kwamba sio Viongozi wenye maono.

Hamad ikatokea ile Ajali ya watoto wa Lucky Visent, Wazungu waliokuwa safari Kwenda Karatu wakakutana na Ajali mbaya ya gari lá wanafunzi iliwabidi washuke na kuokoa wale Majeruhi na kuwakimbiza Hospitali Arusha, wale wazungu Kwa kushuhudia Ajali ile mbaya waliingiwa na huruma na kujitolea kuwapeleka wale watoto Marekani kutibiwa, Nyarandu alichomoka kusikojulikana akaingia kati na kujifanya Msemaji wa wa jambo lile Kwakuwa alikuwa anafahamiana na Wazungu wale. Akajipatia sifa kwamba yeye ndiyo kawapeleka Wale watoto Marekani. Mpaka wale watoto wanarudi na kupokelewa Kwa Sherehe pale KIA hakuna Pongezi toka Kwa waziri yeyote , Waziri mkuu, CCM wala Rais Magufuli Kwenda Lazaro Nyarandu. Walijua janja yake.

Ni katika mlolongo huo huo wa kinyongo cha bwana huyu, Mwezi Julay Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli Alikuwa na Ziara mkoani Singida kuzindua barabara ya Itigi -Tabora, Wabunge wote wa CCM mkoani Singida walihudhuria Ziara hiyo isipokuwa Nyarandu hakwenda Kwenye Ziara ya Rais Ndani ya mkoa wake na alikuwepo Arusha amechil tu.

Hamad Tundu Lissu akapata matatizo ya kupigwa Risasi, Mbunge wa wa CCM Turky akasaidia Kwa malikauli Ndege iende Dodoma kumbeba Lissu na kumpeleka Nairobi, yule mbunge amepongezwa na Spika wa Bunge na CCM makao makuu walimpongeza Kwa maandishi Kwa kitendo chá Uungwana kusaidia Ndege ya kumbeba Tundu Lissu.

Ghafla Nyarandu akaibukia Nairobi kumtembelea Tundu Lissu na kutoa kauli tata akiwa na Wabunge wa CHADEMA. "Muelekeo ni mhimu kuliko kasi, wengi hawajui waendako lakini wana kwenda kwa kasi! Ndio maana ni bora inchi moja kwenda kwenye muelekeo sahihi kuliko maili moja kwenda kwenye muelekeo usio sahihi" alisema Nyarandu.

kabla hajaruhusiwa kuingia ndani ya Hospital kumuona Tundu Lissu Nyarandu alipiga picha Kwenye kibao chá Hospitali na kupost mitandaoni haraka hata Kabla hujamuona mgonjwa. Hii inaashiria Lengo lake ni kuonekana ameenda huko ila sio dhamira ya dhati kumuona mgonjwa, wabongo wanaita kutafuta kiki. Na ameipata kiki aliyokuwa anaitafuta. Ila maneno aliyotoa huko Nairobi na Mengine nayahifadhi ni ishara ileile ya kinyongo chake.

MUDA WA KUMJUA WAZIRI JANGILI UMEFIKA?

Gazeti Raia mwema na Jamhuri walitoa ripoti Maalum ya kurasa 7 kuelezea Ujangili unaofanywa na waziri asiyefahamika katika awamu ya nne, ujangili wa waziri huyo Ulikuwa wa waziwazi na Ushahidi uliwekwa. Waziri huyo aliyetajwa kutumia Helicopter kubeba meno ya Tembo maeneo ya Manyoni na kuyapeleka kusikojulikana. Rais Magufuli baada ya kumulika sekta ya madini hamia na Kwenye Maliasili tuwajue wanaohujumu taifa letu.

Itaendelea..............
isije ikawa wivu wa kike unahusika
 
Lazaro Nyarandu mbunge wa Singida ametajwa kuwa na kinyongo cha kupitiliza Kutokana na kutoswa Kwenye Uwaziri Kwenye serikali ya awamu ya tano imebainika. Kati ya mawaziri wa Kikwete wanaoumia huyu bwana anashika nafasi ya kwanza. Baada ya serikali ya awamu ya tano kuingia madarakani na Nyarandu kutoingizwa Kwenye Baraza la mawaziri lá Magufuli, huyu bwana alisuka mkakati kuwashawishi Maseneta 7 wa Marekani kuja Tanzania kuonana na Rais Magufuli kuzungumza masuala yanayotajwa ya Kimaendeleo na kumshawishi Rais amteue Nyarandu Kwenye Wizara ya Maliasili ili Marekani iendelee kushirikiana na Tanzania Kwa kutoa misaada ya vifaa vya kudhibiti ujangili nchini. Mtakumbuka Rais Magufuli aligundua janja hiyo anakataa kuonana na hao wazungu wa Marekani badala yake alielekeza wakaonane na Spika Ndugai Waeleze mambo yao. Kitendo chá Maseneta hao waliokuja na Ndege binafsi kutomuona Rais kiliwakatisha tamaa sana Kwakuwa Ndugai hakuwa mlengwa.
Hata Wakati wa kikwete kumpandisha Nyarandu kuwa Waziri baada ya kujiuzulu Kagasheki ilikuwa ni Shinikizo la Western power, hii iliwahi kuripotiwa na Gazeti Jamhuri mara kadhaa.

Marekani wanamtaka Nyarandu Kwa sababu za maslahi ya Vitalu vya uwindaji na masuala yote yanayohusiana na bidhaa za wanyama Pori . Huyu ni mtu Pekee aliyeweza kucheza fitina zote kuwaridhisha Matajiri wa kimarekani Kwa kukana maslahi ya taifa lake.

Mdogo wake Nyarandu nimesoma Naye sheria tukiwa darasa moja na hadi leo tuko karibu sana, Pamoja na kutomkubali Kaka yake Kwa madai kwamba hana msaada kwa ndugu zake, Anaeleza jinsi Nyarandu alivyokuwa na matumaini ya kurejea Kwenye uwaziri baada ya uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 akiamini ana nguvu kubwa nyuma yake. Kwahiyo kitendo chá kuachwa mazima kimjengea kinyongo kupita maelezo na amenukuliwa akimnanga Rais Magufuli na Rc Makonda kwamba sio Viongozi wenye maono.

Hamad ikatokea ile Ajali ya watoto wa Lucky Visent, Wazungu waliokuwa safari Kwenda Karatu wakakutana na Ajali mbaya ya gari lá wanafunzi iliwabidi washuke na kuokoa wale Majeruhi na kuwakimbiza Hospitali Arusha, wale wazungu Kwa kushuhudia Ajali ile mbaya waliingiwa na huruma na kujitolea kuwapeleka wale watoto Marekani kutibiwa, Nyarandu alichomoka kusikojulikana akaingia kati na kujifanya Msemaji wa wa jambo lile Kwakuwa alikuwa anafahamiana na Wazungu wale. Akajipatia sifa kwamba yeye ndiyo kawapeleka Wale watoto Marekani. Mpaka wale watoto wanarudi na kupokelewa Kwa Sherehe pale KIA hakuna Pongezi toka Kwa waziri yeyote , Waziri mkuu, CCM wala Rais Magufuli Kwenda Lazaro Nyarandu. Walijua janja yake.

Ni katika mlolongo huo huo wa kinyongo cha bwana huyu, Mwezi Julay Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli Alikuwa na Ziara mkoani Singida kuzindua barabara ya Itigi -Tabora, Wabunge wote wa CCM mkoani Singida walihudhuria Ziara hiyo isipokuwa Nyarandu hakwenda Kwenye Ziara ya Rais Ndani ya mkoa wake na alikuwepo Arusha amechil tu.

Hamad Tundu Lissu akapata matatizo ya kupigwa Risasi, Mbunge wa wa CCM Turky akasaidia Kwa malikauli Ndege iende Dodoma kumbeba Lissu na kumpeleka Nairobi, yule mbunge amepongezwa na Spika wa Bunge na CCM makao makuu walimpongeza Kwa maandishi Kwa kitendo chá Uungwana kusaidia Ndege ya kumbeba Tundu Lissu.

Ghafla Nyarandu akaibukia Nairobi kumtembelea Tundu Lissu na kutoa kauli tata akiwa na Wabunge wa CHADEMA. "Muelekeo ni mhimu kuliko kasi, wengi hawajui waendako lakini wana kwenda kwa kasi! Ndio maana ni bora inchi moja kwenda kwenye muelekeo sahihi kuliko maili moja kwenda kwenye muelekeo usio sahihi" alisema Nyarandu.

kabla hajaruhusiwa kuingia ndani ya Hospital kumuona Tundu Lissu Nyarandu alipiga picha Kwenye kibao chá Hospitali na kupost mitandaoni haraka hata Kabla hujamuona mgonjwa. Hii inaashiria Lengo lake ni kuonekana ameenda huko ila sio dhamira ya dhati kumuona mgonjwa, wabongo wanaita kutafuta kiki. Na ameipata kiki aliyokuwa anaitafuta. Ila maneno aliyotoa huko Nairobi na Mengine nayahifadhi ni ishara ileile ya kinyongo chake.

MUDA WA KUMJUA WAZIRI JANGILI UMEFIKA?

Gazeti Raia mwema na Jamhuri walitoa ripoti Maalum ya kurasa 7 kuelezea Ujangili unaofanywa na waziri asiyefahamika katika awamu ya nne, ujangili wa waziri huyo Ulikuwa wa waziwazi na Ushahidi uliwekwa. Waziri huyo aliyetajwa kutumia Helicopter kubeba meno ya Tembo maeneo ya Manyoni na kuyapeleka kusikojulikana. Rais Magufuli baada ya kumulika sekta ya madini hamia na Kwenye Maliasili tuwajue wanaohujumu taifa letu.

Itaendelea..............
Kadri muda unavyokwenda mtamuona kila mmojawenu ni mbaya wenu. Hata wewe itafika wakati utajiona ni mbaya miingoni mwenu wenyewe.

Sijui kama ni matokeo ya albadir au maombi ila najua huu ni ufalme uliofitinika. Hauta dumu. Mtamlamu kila mtu hadi abaki mmoja wa mwisho ambaye naye atajilaumu. Damu ya mtu asiye na hatia haijawahi kumuacha mtu salama
 
Haya umemsema Lazaro Nyalandu kwakuwa tu hivi majuzi ameenda kumtembelea Tundu Lissu Hospitalini kuwa ana hasira ya kukosa Cheo katika Serikali ya Rais Magufuli na je vipi kwa Jaji Mstaafu Mzee Chande Othman ambaye na yeye juzi pia alimtembelea Tundu Lissu Hospitali?

Wewe ndiyo mmoja wa wale wana CCM ' Wapumbavu ' na wenye roho mbaya iliyojaa ' Ukatili ' hata wa kumzidi Muasisi wa ' Ukatili ' duniani ' Gaidi ' Osama Bin Laden. Na kama CCM yetu itaendelea kuwa na Watu ' makatili ' kama Wewe mwaka 2020 Kazi tunayo kwani nyie ndiyo mtakuwa ' alama ' Kuu ya chukizo la Wananchi Kwetu ( namaanisha CCM )

Halafu nikuonye tu kwamba wakati ' ukiwashwawashwa ' kumsema Lazaro Nyalandu kuwa ni mmoja wa ' Mafisadi ' au Watu walioiibia hii nchi jitahidi uwe na kumbukumbu nzuri kwani kuna Viongozi wako hapo tena wanatoka katika hiki hiki Chama chetu Tawala cha CCM ambao ni ' Mafisadi ' wakubwa na ndiyo hao hao wameifilisi nchi hii vibaya mno tokea miaka ya 90 hadi 2000 hapo mbona nao hujawasema? au huwajui? au unawaogopa?

Mimi ni Mwana CCM mwenzio na ' nakuchana ' mubashara / live kuwa acha kuwa na roho ya Kimasikini kama hiyo uliyonayo. Lililomtokea Tundu Lissu laweza kumtokea Mwanasiasa yoyote hata aliye Kwetu huku CCM? Pumbavu kweli Wewe tena ndiyo umenipandisha hasira na umeshaniharibia asubuhi yangu.

Mbona wanapougua Viongozi wetu wa CCM hawa hawa Watu wa CHADEMA huwa wanaenda kuwajulia hali huko Mahospitalini? Hivi leo Tanzania tumefikia hatua kwamba hadi Mtanzania mwenzetu wa Chama fulani akiugua basi Wewe wa Chama fulani hutakiwi kwenda na kama ukienda unaambiwa ' Msaliti ' au unaambiwa una ' Kisirani ' cha kukosa wadhifa / madaraka fulani?

Hakuna Member aliyenitibua ' akili ' zangu leo kama Wewe na nitaomba wana CHADEMA wasipoteze muda wao kukujibu ila waniachie Mimi mwana CCM mwenzako nikunyooshe vizuri humu ili siku zingine ujifunze kujua kwamba katika shida au tatizo lolote Watanzani huwa tunaungana na kuwa Mtu mmoja.

Najua utarudi tu sasa nakusubiri ili nikushushie rasmi ICBM langu la kisawasawa. Umenikera kunakotukuka asubuhi hii.
Khaaa! GENTAMYCINE kunywa maji mwanangu! mbona umemchana hivyo huyo mwanaccm wa Chato? nasema wa Chato kwa sababu nyie wanaccm asili hamna tabia za chuki kama hizo mpya zilizoletwa kutoka huko. Nauhakika Enzi ya JK pengine hata hiyo hela ya kumpeleka Lissu Marekani usingekuwa unapitishwa mchango kama sasa bali angesema tuu apelekwe.
 
Faili lake lifunguliwe? Hana uadilifu wowote, alizikwiba zitamtokea mdomoni au njia yeyote iliyo wazi

Mkiambiwa mko nyuma ya watu waliomshambulia Lissu mnagoma. Nyie ndio kila siku mnaimba mapambio kwamba ccm imebadilika na eti mnatetea mali za umma. Mmeanzisha mpaka mahakama za nafisadi kwa mbwembwe kisha mkasema eti haina wateja. Saa hii ww mzandiki unakuja na uzi mrefu wa kusema faili chafu la Nyalandu mnalo.

Halafu kwa tabia hii ya huko ccm kuwa kichaka cha kufichia wezi hatuoni yoyote akipigwa risasi bali Lissu anayesema ukweli. Hiyo tabia ya viongozi wa ccm toka juu mpaka chini kujificha ndani ya ccm kama kichaka cha kujifichia waovu tutahakisha tunapambana mpaka kieleweke. Halafu ndio mnasema mpeleke bungeni mswaada wa rais kuongezewa muda wa kukaa madarakani. Kwa hali hii ya kutishana nani anatarajia wabunge wa ccm wenye maovu wawe na maoni huru?

Ulidhani unamtisha Nyalandu kumbe ndio mmejiweka wazi kwenye uovu wenu. Watanzania wote kuanzia viongozi wa dini, wakulima na wafanyakazi someni andiko la huyu bwana muone jinsi ccm ilivyojiunga na kukaa kimya huku wakijua umoja wao ni wa watu wachafu. Halafu tuko kimya watu waovu wanataja kujiongezea muda wa kukaa madarakani.
 
Back
Top Bottom