Daimler
JF-Expert Member
- Sep 11, 2018
- 556
- 973
Kada wa CHADEMA, Lazaro Nyalandu akiwa pamoja na Viongozi wenzake wilayani Tarime, ametumia maandiko matakatifu kujipambanua kurudi upya kisiasa baada ya kukaa kwa muda bila kusikika tangu ahamie CHADEMA. Nyalandu alijifananisha na Batholomeo (kipofu), ambaye aliposikia Yesu akipita alipiga kelele akitaka aponywe.
"Mara baada ya mwaka mmoja, maana watu waliuliza Nyalandu yuko wapi, maana alikuja na halafu akapotea. Nikawaambia watu kulikuwa na saa ambayo ni lazima ifike na hiyo saa ilikuwa jana. Ilikuwa ni mara ya kwanza kuvaa gwanda, kukaa ngangari na kuwa tayari kwa ajili ya hili zoezi."
Nyalandu aliendelea: "Alichokifanya akasikia mkubwa anakuja kama hivi Mbowe. Akakaa barabarani akimsubiri yeye alikuwa kipofu, ukiwa kipofu huoni lakini unaweza kusikia, alikuwa anasikia mambo yanakuja, mageuzi yanakuja akakaa barabarani."
Nyalandu aliisifia CHADEMA ya zamani baada ya kusema kuwa, enzi zake akiwa CCM, walikuwa wakiwaogopa CHADEMA na kupanga mengi ya kupambana nao. "Tukisikia CHADEMA, BAVICHA wanakuja hatulali tunajipanga. Tulikuwa tunawaogopa, tunasema hawa jamaa wanakuja na wanajielewa."
Nyalandu aliwaponda CHADEMA kwa kudai kuwa, kwa sasa wamekuwa waoga tofauti na zamani. "CHADEMA wameanza kuwa waoga tofauti na zamani wakiogopa hata kuvaa sare."