omarilyas
JF-Expert Member
- Jan 24, 2007
- 2,130
- 145
Mambo ya ndani ya ndoa ya Masha hatuyajui, kama yeye na mkewe wana makubalinao flani hatujui, lakini ninawajua wananchi wengi hapa Darsalama, wanaoishi maisha ya open ndoa, na kuishi pamoja kwa ajili tu ya watoto wao, kuna wengine mashoiga na wana wake na watoto,
Masha ni mtu mzima na mwenye akili timamu na msomi pia aliyebobea na ni mwanasheria mzuri sana kati ya wachache sana tulio nao bongo, eti at this time and moment of his life tunaweza kumfundisha what is right na what is wrong? Tena waziri wa mambo ya ndani? Eti wewe mkuu unamjua vizuri mkewe?
Eti ni makosa kwa M-Tanzania kwenda Rosegarden kwa sababu tu ya kazi yake? Kwa sababu amesema nani? Kama hizi habari ni za ukweli na ni njema sana mbona waliozileta hawakuzileta kwa majina yao hasa wanayoheshimika nayo humu forum? Hivi kwa nini mnapenda kujifanya wajanja wakati ni wajinga? Hivi ni kwa nini mnapenda kuwafanya watu hapa forum kuwa ni wajinga sana na ninyi tu ndio wenye akili? Wewe unaamini kuwa una hoja hapa kwa nini unatuzunguka na majina kwa nini usisimame na jina lako hasa unalotumia hapa? Wanaleta udaku hapa halafu wanakimbia na kuangalia kwa pembeni huo ndio ujanja?
Wakuu again ninaomba mtuambie Masha ametumia hela ngapi za serikali kuhudumia huyu kimada? Msitupotezee muda hapa, kama kuwa na kimada ni vibaya sana basi tubadili katiba badala ya kujaribu kuharibu majina ya viongozi humu kwa sababu za wivu na chuki zisizokwisha!
Kaka maswala mengine haina haja ya kujiingiza. Hili la Masha unalijua kabisa na hata hali yake kindoa unaitambua na nini sababu na hata athari za hali hyo unazijua. Sasa ukiwa kama mtanzania unaoumizwa na uozo wa viongozi wetu na kama rafiki wa karibu wa Masha ni bora ukajinyamazia ukainua simu na kumwambia kwa upole tu....Kaka hii sio jitahidi kubadilika.....lakini sio kujaribu kuhalalisha uozo huu wa kimaadili ambao unajua wazi hasara zake kitaifa na kifamilia pia.
Kumbuka tukiwa kama vijana tunapaswa kusimamia Tanzania tuitakayo na sio hii tunayorithishwa na wazee wetu iliyojaa uozo kiasi hiki ambapo tunalzimika kujidanya kuwa uozo wa kimaadili wa viongozi wetu hauna uhusiano na uozo wa kiuongozi kwa taifa letu.
Uongozi bila ya uthabiti wa maadili binafsi sio uongozi bora tunaopigia kelele hapa kila kukicha.....
Onyesha urafiki wa kweli kwa Masha kwa kumwambia wazi kuwa anaharibu kwake binafsi, kwa familia yake lakini zaidi kwa ndoto za watanzania walio wengi walizonazo juu ya viongozi wa kizazi kipya kama yeye.
Bila ya kushughulikia ufisadi wa kimaadili kamwe hatuwezi kushughulikia ufisadi wa kiutendaji, kifalsafa na zaidi ufisadi wa kiuchumi....
Kama kiongozi anaweza kutoithamini familia yake na kama anaweza kumsaliti anayelala naye kitanda kimoja hivi unategemea nini kwa mamilioni ya watanzania anaowapita huku kajifungia ndani ya AC ya gari la mamilioni? Kama anaweza kusaliti kiapo chake cha kuheshimu ndoa yake kwa mungu anayemwamini tangia utotoni mwake hivi atashindwa vipi kusaliti kiapo alicohotoa mbele ya Rais asiye na imani naye, Spika asiyekubaliana naye ama hata mamilioni ya watanzania asio wajua?
Tanzanianjema