Law School ni jipu

salimkabora

JF-Expert Member
Nov 10, 2012
2,441
651
Nimesoma malalamiko ya wanafunzi wa Law School katika gazeti moja linalotoka mara moja kwa wiki siku ya jumanne na kustushwa sana na habari zile. Kati ya maombi 5,000 au sita ya kujiunga na shule ni maombi 500 tu yanayoweza kujiunga na chuo na kati ya hao ni 70 pekee wanaoweza kupata cheti kwa mwaka.

Kwa maoni yangu kati ya fani nyingi wanazosomea vijana hii ndio fani nyepesi kujiajiri lakini inapowekewa vikwazo vya jinsi hii inafaa tujiulize ni nini hasa lengo kuhusu mustakabali wa serikali na ajira za vijana iwapo utawapiga pini hata wale ambao hawatasumbua kupigia kelele ajira za serikalini na mashirika yake.

Pia fani ya sheria inahitajika sana katika kusaidia haki itendeke katikati ya jamii kwa wenye tuhuma au uhitaji mwingine kupata uhudumu wa mawakili na vilevile kuongeza na kuimarisha taasisis za utoaji haki kama vile mahakama, nk. sasa wachache wanapoamua kuibana fani ili wanufaika wawe wachache sidhani kama hiyo ni nia ya kufikia lengo jema.

Vyuo vya elimu ya juu vimeruhusiwa kisheria kuwa vingi, wahitimu ni wengi pia hivyo kuwabana warande mitaani kwa zaidi ya miaka saba au nane wakisubiri kujiunga Law school na miaka mingine kama hiyo kupa cheti cha uwakili ni jambo la kusikitisha na kushangaza sana.

Hebu serikali ilipatie ufumbuzi hili kwa kupanua Law School na/ama kuruhusu watu binafsi kusajili shule kama hiyo kuondoa tatizo hili na pia iwadhibiti hao wanaotaka kuhodhi fani ya sheria na kuifanya ya wateule; mbona hapo mwanzo haikuwa hivyo na mawakili wote wazoefu walioko sokoni na majaji ni bora sana na hawakuwa wakipitia Law School? Hii shule ni mzengwe wa kubana na kukomoa vijana wetu waliosomeshwa kwa gharama kubwa? hivi Taifa letu limeendelea kiasi hiki kuweza kupuuza nguvu kazi ya maana kama hii?
 
Mkuu tumia akili uwezo wa Chuo ni wanafunzi 500 ulitaka ichukue wangapi? Pili ufaulu ndio kigezo sio kubebana hata akifaulu mmoja in sawa.Kumbuka wahitimu wa hapo taifa linawategemea kuwa mahakimu Na mawakili .We we mwenyewe utakuwa wa kwanza kusema Law School wanabebana.Mkuu kama huna akili usiende Law School inaonekana umetoka Shule za kata ambako mnabebwa ili CCM ionekane imeziboresha zinafaulisha.
 
Nimesoma malalamiko ya wanafunzi wa Law School katika gazeti moja linalotoka mara moja kwa wiki siku ya jumanne na kustushwa sana na habari zile. Kati ya maombi 5,000 au sita ya kujiunga na shule ni maombi 500 tu yanayoweza kujiunga na chuo na kati ya hao ni 70 pekee wanaoweza kupata cheti kwa mwaka. Kwa maoni yangu kati ya fani nyingi wanazosomea vijana hii ndio fani nyepesi kujiajiri lakini inapowekewa vikwazo vya jinsi hii inafaa tujiulize ni nini hasa lengo kuhusu mustakabali wa serikali na ajira za vijana iwapo utawapiga pini hata wale ambao hawatasumbua kupigia kelele ajira za serikalini na mashirika yake. Pia fani ya sheria inahitajika sana katika kusaidia haki itendeke katikati ya jamii kwa wenye tuhuma au uhitaji mwingine kupata uhudumu wa mawakili na vilevile kuongeza na kuimarisha taasisis za utoaji haki kama vile mahakama, nk. sasa wachache wanapoamua kuibana fani ili wanufaika wawe wachache sidhani kama hiyo ni nia ya kufikia lengo jema. Vyuo vya elimu ya juu vimeruhusiwa kisheria kuwa vingi, wahitimu ni wengi pia hivyo kuwabana warande mitaani kwa zaidi ya miaka saba au nane wakisubiri kujiunga Law school na miaka mingine kama hiyo kupa cheti cha uwakili ni jambo la kusikitisha na kushangaza sana. Hebu serikali ilipatie ufumbuzi hili kwa kupanua Law School na/ama kuruhusu watu binafsi kusajili shule kama hiyo kuondoa tatizo hili na pia iwadhibiti hao wanaotaka kuhodhi fani ya sheria na kuifanya ya wateule; mbona hapo mwanzo haikuwa hivyo na mawakili wote wazoefu walioko sokoni na majaji ni bora sana na hawakuwa wakipitia Law School? Hii shule ni mzengwe wa kubana na kukomoa vijana wetu waliosomeshwa kwa gharama kubwa? hivi Taifa letu limeendelea kiasi hiki kuweza kupuuza nguvu kazi ya maana kama hii?

Nendeni shule msome achani hoja za kitoto. Mwenyewe nilipita hapo na nilitoka vizuri. Kikubwa mtangulize Mungu afu komaa. Tatizo ni kuna wanafunzi waliosoma vyuo kijanjajanja na wengine wengi wanatokea vyuo vya kiaina kutoka India wanakuwa weupe sana kichwani. Maksi za dezo zilishaisha. Ukifuatilia matokeo ya law schools hata za nchi jirani utagundua ya kwetu iko poa sana
 
Hivi hizi Shule za sheria zina umuhimu gani kama kila siku wezi kama kina Mhando wanaachiwa, Mikataba mibovu inaingiwa, rushwa zinazidi....
 
Nendeni shule msome achani hoja za kitoto. Mwenyewe nilipita hapo na nilitoka vizuri. Kikubwa mtangulize Mungu afu komaa. Tatizo ni kuna wanafunzi waliosoma vyuo kijanjajanja na wengine wengi wanatokea vyuo vya kiaina kutoka India wanakuwa weupe sana kichwani. Maksi za dezo zilishaisha. Ukifuatilia matokeo ya law schools hata za nchi jirani utagundua ya kwetu iko poa sana
Mbona kwenye nyanja za kimataifa hatuwasikii au nyie mpo vizuri kitaifa tu.
 
Mkuu tumia akili uwezo wa Chuo ni wanafunzi 500 ulitaka ichukue wangapi? Pili ufaulu ndio kigezo sio kubebana hata akifaulu mmoja in sawa.Kumbuka wahitimu wa hapo taifa linawategemea kuwa mahakimu Na mawakili .We we mwenyewe utakuwa wa kwanza kusema Law School wanabebana.Mkuu kama huna akili usiende Law School inaonekana umetoka Shule za kata ambako mnabebwa ili CCM ionekane imeziboresha zinafaulisha.
Mtu mwenye akili hatoi mapovu kama haya; hao majaji na mawakili wazoefu waliopo sasa walipita Law School? mapovu yako haya yanatoa solution ya hoja iliyotolewa au ni hoja mpya? Leta ufumbuzi wa tatizo kama unao; watu wasome miaka minne watoke na first class vyuoni chini ya uangalizi wa professor ndio unaona wanalilia kubebwa? maelfu yote hayo ya first class ni feki? jibu hoja acha kuongea pumba
 
Mtu mwenye akili hatoi mapovu kama haya; hao majaji na mawakili wazoefu waliopo sasa walipita Law School? mapovu yako haya yanatoa solution ya hoja iliyotolewa au ni hoja mpya? Leta ufumbuzi wa tatizo kama unao; watu wasome miaka minne watoke na first class vyuoni chini ya uangalizi wa professor ndio unaona wanalilia kubebwa? maelfu yote hayo ya first class ni feki? jibu hoja acha kuongea pumba

First class ya mwisho Udsm ilikuwa around 94 ya Prof .Majamba hizo za kwenu zinagawiwa wapi mkuu?
 
Kazi wanazifanya wanasheria hujulikana kwa kusomwa na siyo kwa kusikia unavyotaka wewe.
mimi nilidhani kazi ya mwanasheria inajulikana kwa namba ya kesi anazoshinda na aina ya wateja wake. Hadi leo sijasikia law firm Tanzania inawakilisha multinational corporation yoyote lakini kama zipo ningependa kujua.
 
mimi nilidhani kazi ya mwanasheria inajulikana kwa namba ya kesi anazoshinda na aina ya wateja wake. Hadi leo sijasikia law firm Tanzania inawakilisha international firm yoyote lakini kama zipo ningependa kujua.

Mkuu acha utani, hivi IMMA Advocates, Mkono and Company advocates, Rex Attorneys etc zipo nyingi mkui
 
Hao waliofungua kesi hawakujua kuwa hawana ushahidi? Ile kesi hata kama wakili angekuwa mwanafunzi wa beekeeping mwaka wa kwanza angemtetea Mhando, angeshinda

Bila ya kuzungumzia sana nature ya ushahidi lengo la shule ya sheria ni kufanya watu wawe competent vizuri kuepuka hayo. Ingawaje kuna kesi zinafunguliwa bila ushahidi kutokana na msukumo wa kisiasa
 
Wanatakiwa kuingeza wigo wa kudahuki wanafunzi wawe na Vyuo walau kila kanda..
kuhusu suala la kufaulu hata akifaulu mmoja ni poa wasipanue goli wakati kipa ni mmoja..Mfano mwaka 1992 kati ya May au Novemba NBAA ilikosa hata mtu mmoja aliyefayefaulu matokeo ya CPA..
 
Sikutanii mkuu naomba kujua at least clients wao wawili tu ambao ni multinational corporation.


Siyo taratibu za kimaadili kutaja clients wa watu ila nenda kwenye websites zao au tafuta CV za baadhi ya hao mawakili utapata majibu unayohitaji
 
Hong
First class ya mwisho Udsm ilikuwa around 94 ya Prof .Majamba hizo za kwenu zinagawiwa wapi mkuu?
Hongera kwa kuwa na data kiboko kama hiyo; '94 mimi mwenyewe nilikuwa pale Udsm lakini sikuweza kuipata kwa kuwa nilikuwa bize zaidi kule FOE. Tuletee basi na data za vyuo vingine vya nje hasa ulaya na marekani kwa maana hata waliotoka Havard wanatakiwa kujiunga Law School
 
Siyo taratibu za kimaadili kutaja clients wa watu ila nenda kwenye websites zao au tafuta CV za baadhi ya hao mawakili utapata majibu unayohitaji
Hamna tatizo nitafanya ka uchunguzi kangu. Asante, na hongera kwa kuwa ethical kwa kutotaja majina ya clients.
 
Mtoa mada una mhenuko.Law School ni regulatory board ambayo Wanafunzi toka vyuo vyote mnapitia pale.Pili,Lst Haiwezi kuanzishwa kila chuo na ndio maana tunataka wanasheria wenye same standard,-Tatu,Wanafunzi 500 ni wengi na pia wanatosha .Nne,Fani ya sheria siyo rahisi kujiajiri kama unavyofikiri,najua wewe ni llb graduate ambaye ukiona wakili unawaza wateja wanamfuata hapo matakoni .Uwakili ni zaidi ya muhuri n a law firm,ni kujitolea ,kutolala na kufanya tafiti sana.Nakushauri ukasome ustawi wa jamii kama hutaki kupitia lst.Nbaa ,kwa wahasibu mbona hawalii lii namna hii?Procurement nao wana bodi yao,Nini maana ya profession?Isikute mpo llb na mnason madesa ya kida Kadeghe ndo maana reasoning capacity yenu ipo chini.Jaji Ndika kuwa makini na hawa wanafunzi wa 17- 29th Cohort,Kumbuka hawa ndo wale waliobebwa na serikali matokeo ya form 4 na 6 ili isiabike dhidi ya shule binafsi.Ndika ,Majamba,Chuwa,Madam molel ,Lukumay ,Dr Swai Kamata hao vijana supp za kutosha,Waachieni kama 20 tu ili wajue uwakili si matako!
 
Mtoa mada una mhenuko.Law School ni regulatory board ambayo Wanafunzi toka vyuo vyote mnapitia pale.Pili,Lst Haiwezi kuanzishwa kila chuo na ndio maana tunataka wanasheria wenye same standard,-Tatu,Wanafunzi 500 ni wengi na pia wanatosha .Nne,Fani ya sheria siyo rahisi kujiajiri kama unavyofikiri,najua wewe ni llb graduate ambaye ukiona wakili unawaza wateja wanamfuata hapo matakoni .Uwakili ni zaidi ya muhuri n a law firm,ni kujitolea ,kutolala na kufanya tafiti sana.Nakushauri ukasome ustawi wa jamii kama hutaki kupitia lst.Nbaa ,kwa wahasibu mbona hawalii lii namna hii?Procurement nao wana bodi yao,Nini maana ya profession?Isikute mpo llb na mnason madesa ya kida Kadeghe ndo maana reasoning capacity yenu ipo chini.Jaji Ndika kuwa makini na hawa wanafunzi wa 17- 29th Cohort,Kumbuka hawa ndo wale waliobebwa na serikali matokeo ya form 4 na 6 ili isiabike dhidi ya shule binafsi.Ndika ,Majamba,Chuwa,Madam molel ,Lukumay ,Dr Swai Kamata hao vijana supp za kutosha,Waachieni kama 20 tu ili wajue uwakili si matako!
Hii nayo ni mada mpya wala haina uhusiano na hoja; after all mimi sihusiki na hicho unachokisema wala sijasoma llb, miaka ya '94 nilikuwa pale Faculty of Engineering sihusiki kabisa na hayo uyasemayo na nimetamka sourse ya habari zangu mwanzoni kabisa mwa post yangu; lengo ni kutafuta solution. Hizo bodi unazoziongelea wewe hazihodhi shule bali zinasanifu mitihani; nadhani hayo ni mambo mawili tofauti na pia msingi mkuu hapa ni kujua kwanini uruhusu vyuo vikupatie graduates elfu tano kila mwaka wakati kule mbele hakuna shule ya kuwapokea; NBAA/NBMM hawana viini macho hivyo; yoyote anayejiona ana ubavu wa kufanya mtihani anakaribishwa; suala la kwamba kajiandaa vipi, kafanya,review au kuna kashule kanampiga msasa ni juu yake na akibunda ni juu yake
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom