Huu mjadala mwingine umeanza, hakuna hata mmoja hapa atakayefafanua wizi huo ila ni mhemuko wa kufutata mkombo kwamba pesa ni zawili. Fafanueni wizi ulitokeaje tuwaunge mkono, lakini kuhemuka kwa kufuata mkumbo siko tayari.
Ukimsoma vyema CAG utaielewa vyema ripoti nzima,hasa kwa wale wenye TAALUMA yao kwa maana ya WAKAGUZI na WAHASIBU.
Pesa ni ya wizi sababu zangu kuu zaweza kuwa tatu au nne.:
1.Pesa ile ilikuwa bado iko kwenye mgogoro wa pande mbili na ulikuwa unasubiri suluhisho toka MAHAKAMA ya kimataifa kuhusu uchakachuaji wa bei ya umeme iliyokuwa inalipwa na TANESCO kwa IPTL,kwa kuwa walalamikaji waliona wanalipa toza kubwa kuliko ilivyotakiwa,hivyo walifungua kesi na bahati nzuri walishinda,lakini hakuna mchanganuo uliokwihsa fanyika wakuweza kujua pesa za IPTL ni ngapi na za TANESCO ni ngapi,hivyo kwa mantiki hii pesa za UMMA hapa zimepigwa na wajanja.
2.Hakimu hakutoa maamuzi pesa hizi zilipwe kwa PAP kwa maana bado kesi ilikuwa ipo mahakamani kuhusu TOZO na mchanganuo wa pesa hizi haujafanywa hivyo kusema MAHAKAMA imeamua hata zile pesa zilizokuwepo kwenye account yenye pesa za wahusika wengi ni za PAP siyo sahihi,basi hapa wale wachache wanaojua kutumia ELIMU yao waliyoipata kwa KODI ya mtanzania vibaya wakaamua kuchota kisichohalali kutumia ELIMU yao hii kwa maana ya AG wetu,hakuwa na sababu ya kutoa idhini pesa zilipwe wakati anajua wazi si sahihi,lakini kwa sababu zake mwenyewe na wahusika aliamua kupindisha HUKUMU kwa maslahi yao wachache.
3.Kuna kodi hapo haikulipwa na ilitakiwa kulipwa kabla malipo hayajafanyika,hivyo basi hata hili nalo halikuonekana kuwa ni baya kwa viongozi wetu wakatumia vibaya mwanya wa elimu na nafasi waliyonayo kufanya maamuzi mabaya na kuhujumu mali ya umma.
4.Pesa ni ya IPTL si ya PAP kwa nini walipwe PAP na si IPTL?Na hapa hata leo JR akienda mahakamani kuishtaki serikali kuhusiana na pesa yake iliyokuwemo kwenye hii account anashinda tena kwa kishindo,sababu ana haki juu ya FAIDA iliyotokana na mauzo ya umeme baada ya kukokotoa TOZO halali,na kila muhusika kuchukua cha kwake kulingana na mahesabu.
5.Hivi serikali ilishindwa nini kufuatilia uhalali wa huyu singasinga kununua hisa za MERCHMAR?Na siyo kweli kwamba walikuwa hawamjui huyu kuwa ni TAPELI la kutupwa,amefilisika wanajua vyema sana kila kitu,lakini waliamua kufanya sababu walikuwa wanajinufaisha wao na familia zao!
Leo tuna mtu aliyepewa ZABUNI ya kuendeleza reli ya kati,na wanajua mtu huyu amefilisika na sheria za kufilisiwa wenzetu wanasheria wanazijua na hasa Mwakyembe iweje leo tumkumbatie mtu aliyefilisika,tunatafuta nini kwake zaidi ya kuliumiza TAIFA kiuchumi?
6.Jiulize ni kwa nini MASWI mpaka dakika za mwisho alikataa kuidhinisha pesa hizi kutoka,ila ni baada tu ya WAKUU wa nchi kuidhinisha pesa zitoke ndipo alipokubali kutoa,hebu tufikirie alilipwa ngapi?Je alitishwa ili akubali?Alifanywa nini huyu mtu,mpaka alidiriki kusema wakimwaga MBOGA atamwaga UGALI
Haya ndiyo mambo makuu ambayo ukiyaangalia vyema si MUHONGO,WEREMA,MASWI wala RAIS angediriki kuuchekea wizi huu.Ila sababu wote hawa wamekosa uhalali wa kuwa viongozi,wamelewa madaraka,si wazalendo hata kidogo,ni sawa na mwizi aliyeshindwa kumuibia jirani akaamua kujiibia mwenyewe.
Tujitahidi kuwa WAZALENDO tuwe tayari kulinda maslahi ya TAIFA letu,tuwe wamoja,tuwe TAIFA kwanza VYAMA baadaye.Tuchague viongozi wenye WELEDI,WAOGA wa MUNGU,WANYENYEKEVU,WAZALENDO,WATAKAO KUWA TAYARI KULIFIA TAIFA LAO.
Haya ndiyo maoni yangu,kwa TAALUMA yangu hizi pesa zipo za TANESCO,za TRA na za IPTL,hivyo kilichofanywa na viongozi wetu ni kuliibia TAIFA lao mchana kweupe,wakishirikiana na wanaowaita wawekezaji,ambao ni MATAPELI.
Na leo Sethi kanunua visima vya mafuta,hakuja na pesa zaidi ya ile $300,000,tumempa mamilioni ya dollar,hivi kweli VIONGOZI wetu wanafikiri kutumia nini?Hivi kwenye vichwa vyao kuna maji au ubongo?Hivi ni kweli walipoenda shule wameelimika au wameenda kuja kusoma na kuandika tu?
Candid Scope haya ni mawazo yangu kulingana na TAALUMA yangu,sijahongwa wala sitegemei kuhongwa sababu UTU wangu hauna bei.