Laiti wananchi wangeisoma ripoti ya CAG mapema

Laiti wananchi wangeisoma ripoti ya CAG mapema

Akili ya kijinga ni kupinga ukweli pole sana

Kudhihirisha kwamba Zito ni mchochezi, kwenye Ripoti yake ya PAC iliyopo kwenye tovuti ya Bunge la Tanzania, ukurasa wa 21 inakiri kwamba fedha waliyolipwa PAP ni Sh. 203.1billioni na kwamba fedha iliyotakiwa kuwa kwenye Escrow Account ni Sh. 306,675,081,939/=

Kumbe inaelekea hiki ndicho Zito na wapinzani hata waliomo ndani ya CCM walichokuwa wakiogopa kisijulikane pale Rais alipoagiza Ripoti ya CAG iwekwe wazi wananchi tuisome. Pamoja na Rais kutolea ufafanuzi suala hilo bado Zito anaendelea na upotoshaji! Maadili tu ya kawaida ya ki-Afrika hayaruhusu hili kutokea. Hii inatia mashaka hata malezi na makuzi ya Zito.

Lakini kwa makusudi kabisa na kwa kuongozwa na nia ya uchochezi ukurasa wa 47 Maoni na Mapendekezo ya Kamati, Ripoti ya PAC umetumia maneno makali ya uchochezi tofauti na ukweli waliouandika wenyewe ukurasa wa 21, ninanukuu "Mfumo mzima wa Serikali ulipata ganzi au uliganzishwa ili kuwezesha zaidi ya shilingi bilioni 306 kuporwa kutoka Benki Kuu ya Tanzania na kutakatishwa kupitia benki mbili hapa nchini"

Kwa mtu yeyote mwenye akili ya kawaida tu, atagundua kwamba kubadilisha matumizi ya neno "iliyolipwa" ukurasa wa 21 kuwa "kuporwa" ukurasa wa 47 na kuamua kutumia kiasi cha fedha ambazo hazikuwemo kwenye Escrow Account, ni mbinu ya kufanya propaganda ya uchochezi.

Zito, alitumia wadhifa wake kama M/Kiti wa PAC vibaya na labda kwa kuhongwa au kuingia kwenye dili chafu ya Standard Chartered Bank iliyotaka kinyemela kuiba fedha za IPTL kwenye Escrow Account kwa kutumiwa na Mkono, Mengi na wanasiasa wanaotafuta u-Rais 2015.

PAC kutolea maamuzi ya uhalali wa SCB wakati kesi ziko mahakamani na kumuandama Mh. Masele, Naibu Waziri wa Nishati na Nadini kwa kumkemea Balozi wa Uingereza kutojiingiza kwenye mambo ya Wizara yake, ni ushahidi tosha kwamba Zito, alikuwa anaongozwa na dhamira ovu na maslahi binafsi, hakutumia hata chembe ya busara. PAC lini imekuwa juu ya Mahakama? Na je, Mh. Masele ni kosa lipi alilokuwa amelifanya kwa kumkumbusha Balozi wa Uingereza kuheshimu mipaka yake ya kazi?

Hapa ndipo Zito anadhihirisha kutumikia maslahi ya SCB. Yeye mwenyewe alikiri kuwa mwaka 2009 alifuatwa na Balozi wa Uingereza na ujumbe wa SCB akawakatalia. Lakini Zito anataka kutuaminisha kuwa miaka mitano baadaye alikuwa bado na msimamo uleule na kujinasibu kuwa ni mzalendo. Maazimio ya PAC kubeba azimio la kuitaifisha IPTL ambyo ni mbinu chafu ya SCB tangu mwaka 2009 waliyotaka kuifanya kupitia Bungeni kwa kukwepa njia ya Mahakama na jitihada ambazo PAC ilionekana kulinda maslahi ya SCB inadhihirisha kuwa Zito na kundi zima la PAC walitumiwa kwa maslahi yao. Kwa hiyo Zito hana hata chembe ya uzalendo.

Ni vyema kabisa Serikali ikamuangalia vizuri Zito na kudhibiti hila zake chafu ambazo ziko dhahiri kabisa. Bunge linapaswa kuiangalia kwa makini Kamati ya PAC kwa ilichokifanya kuleta taharuki isiyokuwa na sababu ambazo madhara yake ni makubwa kwa wananchi kuondoa Imani kwa Serikali yao, wahisani wakasitisha fedha za misaada ya bajeti na maendeleo hayo yote kutokana na uzushi wa Zito. Huyu ni mtu hatari kama Hitla. Asipodhibitiwa anaweza kuliangamiza taifa.

Tufikirie kwa makini na tuache mzaha, Zito na Kafulila hawafai katika jamii ya watu Wastaarabu ni wazushi, wachochezi na wasaliti wakubwa. Ni hatari sana kuamini kila wakisemacho katika kipindi hiki kuelekea uchaguzi mkuu. Inaelekea wanahofu kwa hatma na maisha yao ya kisiasa, kwa hiyo muda huu ni wajasiliamali wa kisiasa na hilo ndilo lililoko mbele yao bila kujali madhara yake.
 
Tatizo mlilo nalo wengi wenu ni uvivu wa kusoma. Lakini pia inasikitisha kushindwa hata kusikiliza mkaelewa! Kuwepo kwa kodi ni jambo tofauti ambalo halileti maana ya fedha kuibiwa. Utaratibu wa kulipa kodi ni jambo tofauti kabisa na ni jambo endelevu. TRA wanapaswa kudai hiyo kodi. Tatizo la uongo na uzushi wa PAC lipo wazi kwani wao walidai pesa iliyoibiwa ni ile ambayo haikuwemo kwenye Escrow Account lakini wameliaminisha taifa kwa kutumia tarakimu kubwa za uongo. IPTL/PAP hawawezi kuiba fedha zao. Licha ya hivyo, tofauti kati ya fedha ya kodi na ile pesa waliyoisamehe TANESCO ni kubwa mno. Inaelekea wengi mlioaminishwa uzushi wa PAC hata hesabu ya kujumlisha na kutoa, hamuijui.


Acha kujitoa ufahamu mkuuTanesco ni mali ya UMA, wamelipa pesa kwa mdeni wao ila mdeni wao hajapata hiyo hela ipo katika taasisi nyingine ya Serikali, yaani suruali moja mifuko tu ndo imeamishwa. Sasa katika hatua hiyo bado unataka kunishawishi ile pesa si ya serikali?

Na kama si ya serikali basi ni ya nani? Ama ndo ya Kirumo Charo?
 
Iwapo wananchi wangepata fursa ya kuisoma ripoti ya CAG kuhusu uchunguzi wa Akaunti ya Escrow ya Tegeta kabla ya kumsikiliza Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) alipowasilisha taarifa yake bungeni bila shaka wangegundua uongo wa wazi uliotolewa na kamati hiyo. Rais Kikwete alitambua udhaifu wa taarifa ya PAC ndio maana aliagiza ripoti ya CAG isambazwe na kusomwa, kabla hata yeye hajafikia maamuzi. Na kwa hakika maamuzi na ufafanuzi wa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwamba fedha iliyokuwa kwenye Akaunti ya Escrow ya Tegeta ni ya IPTL yamezingatia ripoti ya CAG.

Natumia fursa hii kuipongeza PAC kwa kwenda extra mile kuhusu suala la escrow.
 
Iwapo wananchi wangepata fursa ya kuisoma ripoti ya CAG kuhusu uchunguzi wa Akaunti ya Escrow ya Tegeta kabla ya kumsikiliza Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) alipowasilisha taarifa yake bungeni bila shaka wangegundua uongo wa wazi uliotolewa na kamati hiyo. Rais Kikwete alitambua udhaifu wa taarifa ya PAC ndio maana aliagiza ripoti ya CAG isambazwe na kusomwa, kabla hata yeye hajafikia maamuzi. Na kwa hakika maamuzi na ufafanuzi wa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwamba fedha iliyokuwa kwenye Akaunti ya Escrow ya Tegeta ni ya IPTL yamezingatia ripoti ya CAG.

Umejuaje kama wananchi hawakuisoma?
 
Acha kujitoa ufahamu mkuuTanesco ni mali ya UMA, wamelipa pesa kwa mdeni wao ila mdeni wao hajapata hiyo hela ipo katika taasisi nyingine ya Serikali, yaani suruali moja mifuko tu ndo imeamishwa. Sasa katika hatua hiyo bado unataka kunishawishi ile pesa si ya serikali?

Na kama si ya serikali basi ni ya nani? Ama ndo ya Kirumo Charo?

Soma Ripoti ya CAG kama alivyokushauri Mh. Rais. Hayo mambo ya mifuko ya suruali hayatakusaidia kuelewa. Maarifa hupatikana kwenye maandishi. Pesa zilikuwa ni za IPTL na ndio hao waliolipwa. Mh. Rais alitoa ufafanuzi ukaeleweka ndiyo maana na Wafadhili wameridhika na kuamua kurejesha misaada. Tujitahidi sana kuwa tunayaangalia mambo kwa uwigo mpana. Kina Zito wanafahamu kuwa jamii yetu inapenda kulishwa habari za udaku ndiyo maana walifanikiwa kuihadaa kwa maslahi yao.
 
Mbona anawaweka watu viporo? Mtoa mada kasome vizuri mwenyewe na nakusaidia kidogo alicho sema kikwete

Kikwete: "Pesa za Escrow Account hazikuwa za umma"
Halafu baadaye akasema "kulikuwa na kodi ya serikali ambayo haikulipwa na akasema tayari mamlaka ya mapato wameanza kufuatilia kodi zile na kuwa IPTL wameshakubali kulipa".
Sasa je! Kama hakukuwa na pesa ya umma, TRA wanadai hela ya nini na kwa ajili ya nani?:llama::llama:

Achana Naye Huyo Hajui Kitu Mkuu, Inawezekana Ni Mh Chambi Huyu.
 
Soma Ripoti ya CAG kama alivyokushauri Mh. Rais. Hayo mambo ya mifuko ya suruali hayatakusaidia kuelewa. Maarifa hupatikana kwenye maandishi. Pesa zilikuwa ni za IPTL na ndio hao waliolipwa. Mh. Rais alitoa ufafanuzi ukaeleweka ndiyo maana na Wafadhili wameridhika na kuamua kurejesha misaada. Tujitahidi sana kuwa tunayaangalia mambo kwa uwigo mpana. Kina Zito wanafahamu kuwa jamii yetu inapenda kulishwa habari za udaku ndiyo maana walifanikiwa kuihadaa kwa maslahi yao.

Una uthibitisho gani kuwa wafadhili wamelegeza msimamo na kuanza kutoa fedha mkuu?
 
Umejuaje kama wananchi hawakuisoma?

Wengi mnaochangia kwa jazba, wengine hata kwa matusi, inadhihirisha hamkuisoma! Kusoma vichwa vya habari vya magazeti kwenye meza ya muuza magazeti na kusoma Ripoti yenyewe ni vitu viwili tofauti. Ukiisoma hata wewe utauona ukweli. Kwa kuwa una smart phone, ingia kwenye tovuti ya CAG utaipata na pia ingia kwenye tovuti ya Bunge la Tanzania utakuta Ripoti ya PAC, zisome, usiwe mvivu na zote zimeandikwa kwa Kiswahili kwa bahati nzuri. Utazielewa. Hapo ndipo unaweza kuchangia hapa kwa kujiamini kwa kuwa utakuwa unatumia hoja na kutoa rejea kwa kutaja vifungu.
 
Una uthibitisho gani kuwa wafadhili wamelegeza msimamo na kuanza kutoa fedha mkuu?

Pengine jana haukusoma magazeti lakini habari hizo hata hapa JF ziliwekwa tangu jana zikimnukuu Mh. Mwigulu Mchemba.
 
Wengi mnaochangia kwa jazba, wengine hata kwa matusi, inadhihirisha hamkuisoma! Kusoma vichwa vya habari vya magazeti kwenye meza ya muuza magazeti na kusoma Ripoti yenyewe ni vitu viwili tofauti. Ukiisoma hata wewe utauona ukweli. Kwa kuwa una smart phone, ingia kwenye tovuti ya CAG utaipata na pia ingia kwenye tovuti ya Bunge la Tanzania utakuta Ripoti ya PAC, zisome, usiwe mvivu na zote zimeandikwa kwa Kiswahili kwa bahati nzuri. Utazielewa. Hapo ndipo unaweza kuchangia hapa kwa kujiamini kwa kuwa utakuwa unatumia hoja na kutoa rejea kwa kutaja vifungu.

Mimi sijachangia zaidi ya kuuliza mbinu uliyotumia kujua kuwa hawajasoma, sasa unaniunganisha vipi na hao waliokosoa hoja yako? Mbona wewew hujafanya kama unavyoshauri? Nani kakwambia au umejuaje kama Kiingereza kina nipa shida?!!
 
Iwapo wananchi wangepata fursa ya kuisoma ripoti ya CAG kuhusu uchunguzi wa Akaunti ya Escrow ya Tegeta kabla ya kumsikiliza Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) alipowasilisha taarifa yake bungeni bila shaka wangegundua uongo wa wazi uliotolewa na kamati hiyo. Rais Kikwete alitambua udhaifu wa taarifa ya PAC ndio maana aliagiza ripoti ya CAG isambazwe na kusomwa, kabla hata yeye hajafikia maamuzi. Na kwa hakika maamuzi na ufafanuzi wa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwamba fedha iliyokuwa kwenye Akaunti ya Escrow ya Tegeta ni ya IPTL yamezingatia ripoti ya CAG.

Tumelijadili hili katika mada mojawapo inayohusu Rugemalila kuingiza pesa kwenye account ya Askofu msaidizi Nzingirwa wa jimbo kuu la Dar es Salaam. Kwa kufuatilia taarifa mbalimbali na hiyo ya mkaguzi na mthibiti wa pesa za serikali nimekuja kuelewa kwamba pesa ni halali ya wabia wa kuiuzia Tanesco umeme, kama malipo yalikuwa juu mno ni uzembe wa waliomwaga wino kwenye mkataba, la sivyo wasingelipa hizo pesa kama wabia hao hawakutekeleza matakwa ya mkataba.

Biashara yo yote hulka yake ni kutengeneza faida hata ya ziada, mteja jukumu lake kutolipa zidada kubwa mno, lakini akizubaa na kukubali malipo hayo kimkataba basi imekula kwake, hakuna ujanja.

Matokeo ya msimamo wangu huo nimetukwanwa na kusimangwa ukatoliki wangu kwamba namtetea Askofu. Nikawauliza walete hoja za utetezi kwa kufafanua wizi uliofanyika, matokeo wanazidi kutoa povu jingi tu kwamba pesa ni za wizi, nikaona hali kama hii ni mhemuko wa kufuata mkombo tu.

Ukweli ile kamati ya zito wamechukulia jambo kwa kiherehere bila kufafanua wizi ni upi isipokuwa Mwugulu pekee ndiye aliyofafanua kuhusu kodi katika pesa hizo.

Jambo hili ukilisoma kwa makini limekaa kwa mashinikizo ya kisiasa zaidi na baadhi kujitafutaia umaarafu kupitia weak point ya ESCROW.
 
Iwapo wananchi wangepata fursa ya kuisoma ripoti ya CAG kuhusu uchunguzi wa Akaunti ya Escrow ya Tegeta kabla ya kumsikiliza Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) alipowasilisha taarifa yake bungeni bila shaka wangegundua uongo wa wazi uliotolewa na kamati hiyo. Rais Kikwete alitambua udhaifu wa taarifa ya PAC ndio maana aliagiza ripoti ya CAG isambazwe na kusomwa, kabla hata yeye hajafikia maamuzi. Na kwa hakika maamuzi na ufafanuzi wa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwamba fedha iliyokuwa kwenye Akaunti ya Escrow ya Tegeta ni ya IPTL yamezingatia ripoti ya CAG.

Naona mko wengi sana mliojiunga kutetea ufisadi
 
Naona mko wengi sana mliojiunga kutetea ufisadi

Huu mjadala mwingine umeanza, hakuna hata mmoja hapa atakayefafanua wizi huo ila ni mhemuko wa kufutata mkombo kwamba pesa ni zawili. Fafanueni wizi ulitokeaje tuwaunge mkono, lakini kuhemuka kwa kufuata mkumbo siko tayari.
 
Tumelijadili hili katika mada mojawapo inayohusu Rugemalila kuingiza pesa kwenye account ya Askofu msaidizi Nzingirwa wa jimbo kuu la Dar es Salaam. Kwa kufuatilia taarifa mbalimbali na hiyo ya mkaguzi na mthibiti wa pesa za serikali nimekuja kuelewa kwamba pesa ni halali ya wabia wa kuiuzia Tanesco umeme, kama malipo yalikuwa juu mno ni uzembe wa waliomwaga wino kwenye mkataba, la sivyo wasingelipa hizo pesa kama wabia hao hawakutekeleza matakwa ya mkataba.

Biashara yo yote hulka yake ni kutengeneza faida hata ya ziada, mteja jukumu lake kutolipa zidada kubwa mno, lakini akizubaa na kukubali malipo hayo kimkataba basi imekula kwake, hakuna ujanja.

Matokeo ya msimamo wangu huo nimetukwanwa na kusimangwa ukatoliki wangu kwamba namtetea Askofu. Nikawauliza walete hoja za utetezi kwa kufafanua wizi uliofanyika, matokeo wanazidi kutoa povu jingi tu kwamba pesa ni za wizi, nikaona hali kama hii ni mhemuko wa kufuata mkombo tu.

Ukweli ile kamati ya zito wamechukulia jambo kwa kiherehere bila kufafanua wizi ni upi isipokuwa Mwugulu pekee ndiye aliyofafanua kuhusu kodi katika pesa hizo.

Jambo hili ukilisoma kwa makini limekaa kwa mashinikizo ya kisiasa zaidi na baadhi kujitafutaia umaarafu kupitia weak point ya ESCROW.

Zito, Kafulila a.k.a Tumbili, Filikunjombe na Timu yao yote walikuwa kazini. Hao ni wajasiliamali wa ki siasa. Habari ndiyo hiyo.
 
Zito, Kafulila a.k.a Tumbili, Filikunjombe na Timu yao yote walikuwa kazini. Hao ni wajasiliamali wa ki siasa. Habari ndiyo hiyo.

Povu lote walilotoa bungeni hakuna sehemu waliyofafanua wizi ulivyotokea katika pesa hizo, ni Mwigulu pekee aliyethubutu kuanikwa wazi kuwa kodi ilitakiwa kukatwa katika pesa hizo jambo ambalo Banki ya Mkombozi walitekeleza. Wizi ni upi? Ni kutafuta umaarufu wa kisiasa tu.
 
Mimi sijachangia zaidi ya kuuliza mbinu uliyotumia kujua kuwa hawajasoma, sasa unaniunganisha vipi na hao waliokosoa hoja yako? Mbona wewew hujafanya kama unavyoshauri? Nani kakwambia au umejuaje kama Kiingereza kina nipa shida?!!

Watanzania wengi wetu Kiingereza chetu ni cha matatizo. Kwa hiyo Ripoti kuwa imeandikwa kwa Kiswahili nililiona ni zuri tu kwamba mimi na wewe hatutabishana kwa sababu ya kutoelewa lugha.
 
Back
Top Bottom