mangaukawa
Senior Member
- Dec 5, 2014
- 153
- 63
Iwapo wananchi wangepata fursa ya kuisoma ripoti ya CAG kuhusu uchunguzi wa Akaunti ya Escrow ya Tegeta kabla ya kumsikiliza Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) alipowasilisha taarifa yake bungeni bila shaka wangegundua uongo wa wazi uliotolewa na kamati hiyo.
Rais Kikwete alitambua udhaifu wa taarifa ya PAC ndio maana aliagiza ripoti ya CAG isambazwe na kusomwa, kabla hata yeye hajafikia maamuzi. Na kwa hakika maamuzi na ufafanuzi wa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwamba fedha iliyokuwa kwenye Akaunti ya Escrow ya Tegeta ni ya IPTL yamezingatia ripoti ya CAG.
Rais Kikwete alitambua udhaifu wa taarifa ya PAC ndio maana aliagiza ripoti ya CAG isambazwe na kusomwa, kabla hata yeye hajafikia maamuzi. Na kwa hakika maamuzi na ufafanuzi wa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwamba fedha iliyokuwa kwenye Akaunti ya Escrow ya Tegeta ni ya IPTL yamezingatia ripoti ya CAG.