Laigwanani Ole Kisongo ashindwa kumfanyia mila Lowassa

Laigwanani Ole Kisongo ashindwa kumfanyia mila Lowassa

Awali alieleza kuwa sokoine alipakwa mafuta alikuwa mkatoliki ila lowasa hawata mpaka kwakuwa ni mrutheli hizo hekaya mnazitoa wapi? Mbona alieleza jana. Huwa mnafaidika nini kwa kuandika uongo
Wewe hukumsikia vizuri...
Alisema kwa mujibu wa kabila la wamasai laigwanani akifariki kondoo huchinjwa na
Kutolewa mafuta kisha wajukuu kuupaka mwili huo mafuta ya kondoo huyo.

Dakika ya Mwisho Jana Ole Kisongo baada ya maombi ya kiimaasai kwenye kaburi la Lowassa.

Alitamka hawatamfanyia hiyo mila kwa kuwa familia imesema waheshimu imani ya hayati ya Kilutherii.

Uongo uko wapi hapo?
 
Sawa kwani unajua maana ya kisongo mkuu? Je majina hayo kwani huwa hayapewi watu?

Majina ya mahali huwa ni either ya watu, vitu au matukio so kisongo yawezekana kabla hapakuitwa hivyo mpaka alipoishi hapo mtu alitwae Ole Kisongo.
Nakupa elimu. Kisongo si jina la ukoo, ni jina la mahali. Na nilichosema mimi, hapakuitwa Kisongo kwa sababu ya ukoo wao.

Kuna Wamasai wa aina nyingi. Wamasai (Og) kutoka Manyara (Kiteto, Simanjiro, Babati, nk), Arusha (Longido, Monduli, Arumeru, Arusha), Kilimanjaro (Siha, Hai, nk) wanaitwa Irkisongo. Kwa tafsiri nyepesi ni watu wa Kisongo (sehemu).

Historia ya hilo jina ni ndefu.
 
Kivipi mazingira yanaharibika?? Yaan majeneza yanaharibu mazingira?? Wakati hapo Una shelves za mbao sofa seti za mbao...
Kukata mti utengeneze jeneza tu ushaharibu mazingira.

Hata land use tu ni uharibifu wa mazingira. Ukishazikwa wewe ndiyo umeziba eneo hilo lisitumike tena.

Tumetaka kuunganisha barabara ya Maliki Upanga chini na juu, imekuwa kazi sana kwa sababu hapo katikati kulikuwa na makaburi ya Tambaza.

Ikabidi watu wafukue makaburi na kuyahamisha kwa tabu sana. Ndipo kile kipande cha kutoka United Nations Road, hapa Muhimbili Primary School, kuja hapa juu Mindu Stree kikawekwa.

Ingekuwa hatujajifunga kwenye kuzika, tusingekuwa na matatizo kama hayo.

Kuna siku nilikuwa napiga mahesabu, kama watu wakiwa wanakufa kwa rate hii ya leo na wanazikwa tu, in 100 years tutatumia eneo kama la nchi nzima ya Gambia kwa makaburi tu.

Sasa watu wenye kufikiri mbele sana wanafikiria, what about in a thousand years? What will the economic cost be?

Even worse, zamani watu walikuwa wanazika ina biodegradable way, hawajengei. Siku hizi watu wanajengea mausoleum, wanaweka concrete kabisa. Nilikuwa natania nikasema jinsi watu wanavyosilibiwa simenti, ikiwa siku ya parapanda watu watafufuka kutoka makaburini, wengine watashindwa kufufuka kwa sababu ya makaburi yalivyosilibiwa simenti.

Najua mengine ni mambo ya utamaduni na kila mtu ana haki ya kuzika kivyake, lakini, kadiri tunavyoongezeka na ku face matatizo ya mazingira, land use etc, inaonekana ni vizuri zaidi kutafuta alternative.
 
Nakumbuka Nelson Mandela alizikwa kimila kwa mujibu wa kabila la kizulu
Mandela attained enlightenment, I have the guts to urgue so.

Ninaweza kumlinganisha na Mahatma Ghandi.

Ni kati ya binadamu waliofanikiwa kufikia upeo wa juu kabisa wa kufikiri, na ndio maana aliweza kupumzishwa kimila.
 
  • Thanks
Reactions: Tui
Mandela attained enlightenment, I have the guts to urgue so.

Ninaweza kumlinganisha na Mahatma Ghandi.

Ni kati ya binadamu waliofanikiwa kufikia upeo wa juu kabisa wa kufikiri, na ndio maana aliweza kupumzishwa kimila.
Ni tofauti sana na wanasiasa wetu.Alifungwa Robbin Island na makaburu na kazi ngumu na bado akasemehe.Hawa wa kwetu na visasi na ujinga na upeo mdogo wa kufikiri.Wengine wanamuita nabii.
 
Ole Kisongo. Nafikiri pale Kisongo panatokana na jina lake.
Si kweli. Huyo Mzee ni chawa-tapeli! Sijui kafikwa na nini tu anababuka ngozi
20240828_213902.jpg
 

Attachments

  • images (29).jpeg
    images (29).jpeg
    59.3 KB · Views: 11
Siku hizi watu wanajengea mausoleum, wanaweka concrete kabisa.
Sielewi wanajaribu ku prove au kuzuia kitu gani, ila hili swala la kuchimba kaburi halafu waanza kujengea matofali sijui zege na cement linanikera sana.
Labda wanajaribu kugomea kauli ya dust to dust
 
Sielewi wanajaribu ku prove au kuzuia kitu gani, ila hili swala la kuchimba kaburi halafu waanza kujengea matofali sijui zege na cement linanikera sana.
Labda wanajaribu kugomea kauli ya dust to dust
Hujasikia Kinondoni kuna watu wanazikwa kwenye makaburi ya zamani yanayochinbwa upya?

Watu wanajaribu kujimilikisha ardhi milele asizikwe mtu mwingine hapo.
 
Back
Top Bottom