FirstLady1
JF-Expert Member
- Jul 29, 2009
- 16,789
- 5,409
Poleni dear may they rest in peace.... Enways FL1 una bahati huna hizo mshike mshie ....
Kumbe zipo mshike mshike eeeh mungu awatie nguvu wote wenye mama mkwe wa namna hii ,
wapate kubadilika
Poleni dear may they rest in peace.... Enways FL1 una bahati huna hizo mshike mshie ....
Hahaha!!! Diary inakaribia kujaaI know.... ndo mana nakuambia always carry that big diary of yours....
Kumbe zipo mshike mshike eeeh mungu awatie nguvu wote wenye mama mkwe wa namna hii ,
wapate kubadilika
Mimi nina bahati sina mawifi nina mama mkwe tu maana nasikia mawifi nao ni issue sometimes. Mama mkwe wangu nampenda na so far hatujawahi kugombana. Labda kwa kuwa yuko mbali na si wa kijijini kwa hiyo ni muelewa. Pili huwa sijajaribu hata siku moja kuwa kiwingu kati yake na mwanae kwani mume wangu ni last born. Akiniomba kitu basi niko tayari kukopa kama sina ela nimpatie. Sometimes huwa nawaza am I caring too much than the way am treating my own mother? Well ukipenda boga lazima upende na ua lake!
Na kwa kumtreat mama mkwe wangu vizuri nadhani kunamfanya mume wangu anipende sana na kutonificha chochote kuhusu familia yao hata wanachoongea na mama yake on my absence. Hata mashemeji zangu wananipenda pia.
Hakuna atakaye kupenda ukimchukia mzazi wake!
Hakuna watu watamu kama mama wakwe jamani. Ujue kama huna UHUSIANO na mama yako mzazi hakuna jinsi utampenda au kuwa na uhusiiano mzuri na mama mkwe.Mtaandika yote na kufunua hadi vitabu vya saikolojia end of the day utagundua kwamba BIBLIA/MSAHAFU ndiyo ufunuo wako kwenye maisha yako ya kila siku. Wanawake ndiyo leaders wa nyumba, mama mkwe hana tofauti na mama yako mzazi kwa nini umchukie? Unampendaje mtoto ukamchukia mamake? wanawake wengi wanapoolewa wanakuwa WACHOYO mtu na mamake walishazoea kutumiana hela 300,000 kila mwezi kusaidia shughuli za nyumbani kwa mama yake wewe KIGUGUMIZI umeingia tu inaanza kutoka laki 1, badala ya kuongeza iwe 4 weew unakuja na ugumu wako. Unategemea utapendwa hapo zaidi ya chuki? Sometimes kweli mama wakwe wanaweza kuwa nje ya msitari but chanzo kikawa ni mumeo au wewe muolewaji. Acheni viburi, majidai, kujisifu, kujikweza, kujiona hakuna kama wewe, mwambie mungu akutunze wewe na familia yako siyo kukakamalia uchoyo na kiburi visivyo na sababu.
Mimi nina bahati sina mawifi nina mama mkwe tu maana nasikia mawifi nao ni issue sometimes. Mama mkwe wangu nampenda na so far hatujawahi kugombana. Labda kwa kuwa yuko mbali na si wa kijijini kwa hiyo ni muelewa. Pili huwa sijajaribu hata siku moja kuwa kiwingu kati yake na mwanae kwani mume wangu ni last born. Akiniomba kitu basi niko tayari kukopa kama sina ela nimpatie. Sometimes huwa nawaza am I caring too much than the way am treating my own mother? Well ukipenda boga lazima upende na ua lake!
Na kwa kumtreat mama mkwe wangu vizuri nadhani kunamfanya mume wangu anipende sana na kutonificha chochote kuhusu familia yao hata wanachoongea na mama yake on my absence. Hata mashemeji zangu wananipenda pia.
Hakuna atakaye kupenda ukimchukia mzazi wake!
Kitu ninachokiangalia sana kwa mama mkwe wangu ni kum-treat kama mama yangu. na huwa najitahidi sana, hata akifanya kitu kinachonikwaza huwa namwambia kuwa mama hapa umenikwaza. mwanzo alikuwa hanielewi lakini sasa ananipenda sana, huwa nasikia tu kwa watu kuwa mama mkwe ananiongelea vizuri kwa wenzake.
Mi si mkareee we unanisareeee!!Nimechoka kukuambia kua we mkareee.....
FP Hongera kwa kushinda mtihani ambao wadada wengi hutushinda... Bravo!!... Keep on keeping on....
Mi si mkareee we unanisareeee!!
Hheheh we zaidi mpendwa ndo maana umeleta hii yuziful nyuzi!!!
Nani kama mama mkwe!
Asante my dear.
Unajua wadada wengi wanashindwa sababu ya ku-pretend. anapoingia anataka kumfanyia mama mkwe heaven on earth, at the end anashindwa. yaani hata mama mkwe akikosea anajitahidi kumwonyesha yupo vizuri ingawa analalamika pembeni. hawa mama wakwe ni binadamu tu kama sisi, na wanapaswa walijue hilo. kwa hiyo anauwezo wa kukukwaza na pia kukufanyia jema. akikufanyia jema, unamshukuru na kumwambia kuwa hili jambo ni jema, na akikosea unatakiwa kumwambia kuwa umekwazika, kiaina, siyo kwa kugombana. kama unakwazika na mamako sembuse mama wa mwingine?
Ni kweli unayosema na nakubaliana nayo... Mimi ndo maana huona kama mwanaume anataka akae/aishi kwa amani nyumbani kwake asipende kumleta mamake aishi nae labda in speacial cases kama labda ni mzee saana na anahitaji assistance au ni mgonjwa... Otherwise its better awe ankuja kusalimia tu hata kama weeks au mwezi.... what ever the case but sio awe permanently hapo kama inawezekana...
Kwenye ile project ndio maana i made a request of a Lawyer lol!!Itabidi nikusindikize ukachukue course ya short hand uache kunakili ma sentence marefu....... lol
Hili pia ni jambo la maana sana, na ukiona mama mkwe anang'ang'ania kukaa kwenu bila sababu (uzee, ugonjwa) ujue huyo ni mshari. kwa nini asikae kwake? huwa nampenda sana mamangu, yaani mpaka aje kwako ujue kuna sababu maalumu, tena ni nyie ndo mnashida, akiwa na shida yeye anasema anapenda nyie ndo mkienda kwake, siyo yeye kuja kwenu. yaani ukijifungua, kuja kuona mjukuu atakuja kwa siku chache na ataondoka, kila mara huwa anatutafutia ndugu zetu ndo waje kutusaidia tukijifungua..................... kwa kweli wifi yetu atakuwa na amani sana kwa ndoa yake, hatapata shida kabisa na mawifi wala mama mkwe
Nilisikitika mama mkwe alipokufa kama binadamu. ila niliutua mzigo mkubwa sana maana tulikuwa tunakaa nae. Nyumba ilikuwa haikaliki ila sasa amani tele.Miaka 2 ya ndoa ilikuwa kama 20 kuishi nae zizi moja.