Ladies ndani ya ndoa piteni hapa

Ladies ndani ya ndoa piteni hapa

FirstLady1

JF-Expert Member
Joined
Jul 29, 2009
Posts
16,789
Reaction score
5,409
Poleni na majukumu ya kila leo mashostito pale tunapokuwa na jambo lazima kushare pamoja

Leo nina jambo kidogo la kushare kwa sisi ambao tunashikilia Gurudumu la ndoa mambo machache ya kukumbushana na kuelekezana,

Kumekuwa na kasumba ya kina mama wakiwa saloon au popote kwenye mikusanyiko ya kina mama ,kina dada wengi utamsikia mtu ooh mme wangu ni mwaminifu ooh mme wangu saa kumi na mbili tu yuko ndani , ananipenda na hacheat na mengineyo mengi wakati wenzio ukigeuza tu kisogo wanakucheka na kusema things happen.
Cha msingi kama unaona hilo na kujua hivyo piga goti na umshukuru mungu kwa hilo,wala usifungue mdomo kujisifia Mbele za watu .
Mifano hai,

1.Kuna dada mmewe akiwa nyumbani kwake anajali watoto ,anamjali mke,Kusoma neno la mungu na kuongoza misa ya family ni mtu ambae ukimuona utasema yes mme ninae hasa hata kumdolishia kwa watu,Lakini upande mwingine wa shilingi ambao mkewe hajui na ni mke ambae mambo ya outing ,socialization kwake hayapo ,michepuko kwa mmewe ile ya underground ni namba 1,so mkewe akiwa sehemu kwenye vikao vya kparty au walipo wanawake anajisifia watu wanasikiliza tu kwa vile walioko nje wanamjua huyu shemeji sema wanashindwa kumwambia na hawawezi kuhofia kuleta hitilafu kwenye ndoa .INATISHA

2. Jmos nikiwa Saloon kuna warembo fulani walikuwa wanapiga story zao eti ooh huyu dada akija hapa nikujisifia mme wangu mme wangu hajui kama mmewe tunakula nae sahani moja,Kumbe mmoja wa wale akina dada anatoka na huyo jamaa yuko Bank moja,na ili kuthibitisha hilo akamcall jamaa wakaahidiana akitoka saloon atapita pale amchukue waende wanapojua..VERY BAD

3.Kubwa kuliko hii niliikuta duka la nguo za kina mama kuna wadada wamepeana kazi ya kumtafuta mme wa dada mmoja kwa udi na uvumba wanasema lazima wampate hii wamepeana task kabisa mmoja akishindwa kumpata lazima mwingine ampate ,hivyo wameweka mbinu na mikakati ya kumpata huyo jamaa ,
Ni jamaa ambae eti wanadai lazima aende hapo dukani kumfanyia mkewe shopping ya nguo na sokoni sometimez anaenda yeye kufanya manunuzi ya ndani
wanadai pia mke wake ni mzuri lakini mshamba,
Pia wanadai jamaa ni Handsome na ana mshiko wa uhakika-lazima waende nae sambamba

Duh tunaenda wapi kumbe waume zetu wanatafutwa :A S 11:

Haya kina mama tunaopenda kusifia waume zetu mbele za mabinti /kinadadaa mara ooh nikiwa mjamzito ananipikia anapapasa kitumbo ananiogesha - wapo wanaowapigia speed huko

Kina mama mnaotoa siri za ndani hizo ndio silaha za kutumaliza :flame:

Mwisho kabisa wanasema sie wachoyo kwanini kula peke yetu - Tukumbuke kuziombea ndoa zetu majaribu ni meeeengi sana.

Muwe na Ijumaa njema:couch2:
 
kuna dada mmoja yake ndo haya owh mume wangu this mume that kumbe huyo mume ni mshenzi hakuna mfano sketi haimpiti ila dada anavyochorwaaaa hajijui, unaanzaje kujitapa una mume bora hua hatujui kama alikutongoza akakupata atashindwaje kwa wengine??

akiwa ndani ni wako akitoka nje wa wenzako.
 
Siwezi kujisifu nina mume bora au bf bora ... hawa viumbe hubadilika mara ... kama kama kuchanganya maji na rangi nyekundu acha kabisa....... akiwa mzuri tumia hiyo nafasi vizuri jua ubaya unakuja...
 
Mie kwa kwa kweli kelele za chura hazitanizuia kumsifia zombie, niibe nijifiche kusifia, mume naye niogope kumsifia kisa kuna pyschos wanataka kumkwiba kwa kunikomoa nisijisifie? Wamkwibe tu, tena akiwa zuzu wambebe mazima.

As long as mume anarudi home, am at peace na nitamsifia hadi nitakapoona otherwise.

Kuna workmate wangu pia alinishangaza, anaishi Sinza. Alinisimulia jinsi wanavyopanga kumwibia shost yao mume kisa anajisifia sana. Nikamuuliza, mkishamuiba mnapanga na kuivunja hiyo ndoa, wakasema hapana, tunamkomesha tu afunge mdogo. Kweli nilimuona ni pyscho tu. Kumkoa mke wa ndoa wa mtu mtu ni sawa na kuikomoa serikali, haikomoleki. Sema tu hili gonjwa ndio balaa.

Kwanza ukiona wanawake wanafuata mumeo, jua ulichagua aliyenona, na inafanya ndoa kuwa more exciting.
 
kizuri kula na wenzio ati! hahaha.... joking!

wengine husimulia na kusifia mambo ya chumbani kabisa kwa mashosti wao.

unadhani watakuachia ufaidi peke yako?

the liberation of your mind will liberate you from any enslavement

napita kimyaa kabisa kwenye huu uzi.
 
Sijaolewa ila nachangia from experience lol. Wanawake bana wakati wengine Mungu atusaidie tu. Unadhani hao wanaume wote wanaotafutwa waibwe, ni kwa sababu wake zao wanawasifia sana mbele za watu?
Wengine wameumbwa tu na roho za kwa nini, wivu wa kipumbavu tu. Usione mke na mume wamepita wamecheka, wewe. roho inakutukuta kwa kijiba chako, yani kosa lao kubwa ni " kwa nini mna furaha"? Watu wanapenda tu kuona mwenzao katoka na minundu ndani ndo roho zao kwatuuuu.

Sasa hao wanaomvizia baba wa watu hapo dukani sijui kisa tu anaendaga kumfanyia shopping mama watoto wake, mkewe amejisifu kwa watu? Unapovunja ndoa ya mwenzako unajisikiaje kwanza, roho haikusuti kuona familia ya mwanamke mwenzio inayumba kisa wewe?? Karma has no menu, u get served what u deserve, utalipwa tu siku moja kwa kazi yako njema ya kijiba cha roho, kama hutolipwa wewe basi kitalipa hata kizazi chako. Tuoneane huruma jamani
 
Mie kwa kwa kweli kelele za chura hazitanizuia kumsifia zombie, niibe nijifiche kusifia, mume naye niogope kumsifia kisa kuna pyschos wanataka kumkwiba kwa kunikomoa nisijisifie? Wamkwibe tu, tena akiwa zuzu wambebe mazima.

As long as mume anarudi home, am at peace na nitamsifia hadi nitakapoona otherwise.

Kuna workmate wangu pia alinishangaza, anaishi Sinza. Alinisimulia jinsi wanavyopanga kumwibia shost yao mume kisa anajisifia sana. Nikamuuliza, mkishamuiba mnapanga na kuivunja hiyo ndoa, wakasema hapana, tunamkomesha tu afunge mdogo. Kweli nilimuona ni pyscho tu. Kumkoa mke wa ndoa wa mtu mtu ni sawa na kuikomoa serikali, haikomoleki. Sema tu hili gonjwa ndio balaa.

Kwanza ukiona wanawake wanafuata mumeo, jua ulichagua aliyenona, na inafanya ndoa kuwa more exciting.

Kongosho mie nadhani pale inapostahiri kusifia maybe

Pengine unasifia watu wanakuchora ooh mme wangu nikikata nyanya anakata kitunguu,kisha anaongezea mnalalamika wee wakati wangu hana hayo matabia kuna mmoja alikuwa anaongea haya maneno wakati kwenye hilo Kundi kuna dada anatoka na mmewe na watu wanajua kila mtu alibakia kimya na kuumia rohoni kumwambia wanashindwa
Mama mmoja akamwambia we mwana wee jitahidi kuwa unatoka out na mmewe usimwache aende peke yake,
 
Ni kweli, si kila jambo la kusema hadharani, lakini mi naona nyumba ndogo tumezipa umuhimu kuliko zilizo nao.

Huyo dada kama anamsifia mumewe kutoka rohoni ni haki yake, sasa aogope kisa mwizi wake yuko pale, tena wala hamjui? Bora hata mume angekuwa ameitambulisha nyumba ndogo yake kwa mkewe, ningesema ana uzito fulani kwa muwe.

Anyway, ni mtizamo tu(he he he, japo huwa si mtu wa kujisifia iwe ninacho ama sina), but ningekuwa mtu wa matangazo na masifa, ningesifia hata kama najua ni kit.ombi. Binadamu anaweza kuwa na baya 1, akawa na mazuri 9, ya nini niyazike mazuri 9 kwa baya 1?

Labda kweli huyo dada mumewe anamsaidia kukata vitunguu, wangapi hapa tunasaidiwa vitunguu? Akiingia jikoni ni aidha kwa maelekezo ya mganga ama mke uko kwenye ambulensi. Sometimes if you have it, brag it, kama haikusumbui.

Kongosho mie nadhani pale inapostahiri kusifia maybe

Pengine unasifia watu wanakuchora ooh mme wangu nikikata nyanya anakata kitunguu,kisha anaongezea mnalalamika wee wakati wangu hana hayo matabia kuna mmoja alikuwa anaongea haya maneno wakati kwenye hilo Kundi kuna dada anatoka na mmewe na watu wanajua kila mtu alibakia kimya na kuumia rohoni kumwambia wanashindwa
Mama mmoja akamwambia we mwana wee jitahidi kuwa unatoka out na mmewe usimwache aende peke yake,
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom