Laana ya mwanamke

Nimekumbuka mbali sana Mungu nisaidie...nakumbuka jamaa alinichumbia na ujauzito juu...nililia sana aliponiambia sikupendi nimepata mwungine hapo kwake anitaki nyumban naambiwa nenda kwa aliekupa ujauzito...hakuna kipindi kugumu nilichopitia katika maisha yangu kama kile asante Mungu kwakua kila jaribu ulipa mlango wa kutokea sasa hv ukimuona du mwacheni Mungu aitwe Mungu
 
Hizi laana zitaendelea sana kutupata kwani wanawake bila kudanganywa aisee hupati kitu, ukisema ukweli utazungushwa balaa kama kwenda ofisi ya uma kupata huduma bila kuwa hata na hela ya rushwa kidogo.
 
Yalinikuta kwa hiyo siwezi kubisha chochote. Kuna huyu mwanamke nilimzalisha na sikuwa tayari kuishi naye, alilalamika sana. Balaa nilililopata baada ya siku chache tu, itachukua years to recover.

Pamoja na ubishi wangu nilijipeleka kanisani mwenyewe na ndio kwa mbaaali mambo yakaanza kuwa easy na sasaivi naongea na yule mwanamke na ikiwezekana ntaenda kumchukua tuishi wote japo saivi mtoto ni mkubwa tu
 
Hii thread naondoka nayo, Huyu mama nanihii kumbe nisimuache eeh, maana toka niko nae sijawahi kupata shida duh, noma sana!
 
Ni kweli usemayo,hakuna kitu kinauma kama kupotezewa muda jamani, umejitunza na kuwakataa wengine wenye nia afu mtu anakuacha hewani gafla,uwiii.... Mungu niepushie isinitokee tena
Vale inaonyesha uliumizwa sana coz umerudia tena kauli hii, pole sana
 
Dah! Sijui huyu mwanamke wangu nimuache vipi maana kiukweli anamapenzi makubwa sana juu yangu ila sina hata future naye maskini!
 
Hakuna kitu kinauma kama kupotezewa Muda, Ex wangu hadi leo pamoja na kuwa na kazi nzuri maisha yake hayaeleweki, kwenye mahusiano ndo usiseme, nabado napiga goti kwa Mungu siku atakayorudi kuomba msamaha kwakunikosea ndo amwachilie.
wewe ni kabila gani?
 
usipomuaminisha haupati Free papuchi,sasa nani anataka kugharamia?
 
Hakuna kitu kinauma kama kupotezewa Muda, Ex wangu hadi leo pamoja na kuwa na kazi nzuri maisha yake hayaeleweki, kwenye mahusiano ndo usiseme, nabado napiga goti kwa Mungu siku atakayorudi kuomba msamaha kwakunikosea ndo amwachilie.

Toa msamaha, utakuwa huru pia.
 
Nasikia wakwe wamekuambia ulipe faini ya kukulelea mwanao kwa miaka hyo tisa..polee sana
 
Vale inaonyesha uliumizwa sana coz umerudia tena kauli hii, pole sana
Ndio maisha ndugu yangu, tunapata wasiotambua thamani zetu hili ni pande zote... Kikubwa ni kusonga mbele na tunajifunza kutokana na makosa ili ikitokea anaekuthamini usimuache zaidi ya kumtendea vema...
 
Ndio maisha ndugu yangu, tunapata wasiotambua thamani zetu hili ni pande zote... Kikubwa ni kusonga mbele na tunajifunza kutokana na makosa ili ikitokea anaekuthamini usimuache zaidi ya kumtendea vema...
Wanaume kiujumla tumeumiza wengi, hili ni tatizo sana kwani limeleta madhara makubwa, ninapoona mabinti wanajiuza naumia sana coz wengi waliumizwa sana then wakakosa imani na wanaume wote wakijua na kuamini hakuna waoaji au wanaume waaminifu na ndipo wakajirahisisha japo sio wote.
Wanaume baadhi wamesababisha machokoraa kwa kuwatelekeza wanawake na kushindwa kulea watoto hatimaye wako mitaani kuokota vitu vya kuuza, sio hivyo wamesababisha vifo kwa wadada kwani waliwapa ujauzito na kuwakana na wakaamua kutoa ndipo kifo kikawapata. Wanaume wenzangu tubadilike tumeumiza wengi, na wengi wanalia kwa ajili yetu kwanini mabaya yasitupate?
Tuwe wakweli mbona dada zetu ni waelewa tu?
Mwambie aina ya urafiki uutakao kwake naye atakuelewa. Mtusamehe sana dada zetu
 
Ndio maisha ndugu yangu, tunapata wasiotambua thamani zetu hili ni pande zote... Kikubwa ni kusonga mbele na tunajifunza kutokana na makosa ili ikitokea anaekuthamini usimuache zaidi ya kumtendea vema...
Usife moyo utapata atakayekufanya usahau magumu yoote
 
Kusamehe napo ni mtihani,sio rahisi kama mkosaji anavyofikiria tena makosa ya makusudi yanaumaga balaa ni basi tu We love God so kupenda watu wake (wema kwa wabaya) ni amri otherwise walioniumiza wote acid zingewahusu,kama sio sumu,au kuchoma nyumba zao,achilia mbali kuwatengenezea ajali au hata kuwakodia majamaa wawageuza nyuma na picha juu kubandika mji mzima angalau tujumuike pamoja ktk maumivu.





Tuwatendee wenzetu tunayopenda kutendewa,tuwe wakweli ili mwenzio ajue atajiweka position ipi kwako,au aamue kuliwa kwa kupenda ye mwenyewe na sio kwa uwongo wako....
 
nimesoma huu uzi na comments. nimeona wanaoathirika sana ni wanaume kutokana na kuacha wenza wao. pia kuna wanawake ni wagumu kusamehe

mimi nimeachwa zaidi ya mara tatu na wanawake ila wanadunda tu na maisha yao.

Hisia sio kitu cha kuchezea kabisa. Hebu tujiepushe na haya mambo ya kuendekeza tamaa za mwili wakati huku unajua unaumiza wengine.

Heshima na upendo vituongoze sisi sote
 
Hii kitu ni atar sana kwaafya na mustakabali wa maisha kwa ujumla tujiepushe jaman me yashanikuta lakin nashukuru mungu nilichomoka salama
 
yani kama mimi usinisogelee kabisa sinaga presha ukiwa umejipanga kunichezea utajichezea mwenyewe.....wanarudi wanalialia ila cha moto wamekiona
 
Mleta mada, mimi siamini kuwa machozi yake(yao) yatanipa laana, kwa sababu;
1. Mbele za M/Mungu tulifanya dhambi ya uzinzi, ngono na uchafu ambao Mungu hapendi.
2. Tulitenda dhambi ya uongo wote (mimi nilimdanganya, nae kadanganya kwa Mungu)
Hayo yaliyokupata ni sehemu ya maisha tu (ups and downs) na wala haihusiani na kumdanganya au kuchezea mwili na hisia zake. Mwanamke wa kweli hachezewi mwili coz anaitambua thamani ya mwili wake, the worst you can do ni kuchezea hisia. Mwanamke/mwanaume anayechezewa mwili ni mjinga mjinga tu..
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…