Eli Cohen
JF-Expert Member
- Jun 19, 2023
- 1,309
- 4,017
Ndugu zangu naelewa kila mmoja anapitia ya kwake kimaisha na kila mmoja anafahamu historia ya safari ya mapito ya ukoo wake.
Tambueni kuwa kuna kero na karaha nyingi za kujirudia zinazotesa koo nyingi. Na inafikia wakati hadi matatizo haya yamekuwa ni ya kuzoereka kutokana na kuchukulia poa au kutokuwa na umoja wa kujaribu wa kuyatatua madhira hayo.
Kinachofatia ni kuhangaika kwa waganga, wachungaji feki, mashehe watoa majini, kurushiana lawama za kulogana baina ya ndugu, etc.
Laana inarithika katika vizazi, laana inasaka wapi pa kutua ili ijitukuze, kwa maana bado inalilia damu ndani yenu kutokana na uchungu uliofanyika na mababu au mabibi zenu kwa watu wengine.
Madhabahu yaliyowekwa na mababu yalijitengeneza kiroho ndani ya ukoo na sasa yakaangaza na kukaa enzi na enzi. Madhabahu hayo yalifanyika katika matambiko ya kishirikina au kuenzi mizimu. Kuumaanisha walikaribisha roho hizo ziweze kuangaza ndani ya damu na vizazi vya ukoo.
■Kuna koo ambazo unakuta wanawake karibia wote wanapitia mateso ya ndoa. Hii unakuta kuna bibi aliwahi kufanya kitu kibaya na wakamlaani yeye na kizazi chake.
■kuna koo unakuta mabinti wanasumbulia na mizimu ya kuagua na uganga eti kisa bibi zao walifanya hivi.
■kuna koo unakuta kuna roho ya visasi na kufanya mauaji inatembea ndani yao. Yani hawakuachi hivi hivi lazima wakufanyie damage ndio walidhike hata kama ni mwanae amemkosea pakubwa.
■kuna koo unakuta majina flani wakipewa watu wanakuwa wafuska sana kwa sababu mtu huyo nae alikuwa mfuska.
■Kuna koo unakuta watu wengi hawana vibali vya kukubalika, anapiga kazi sana, anaona vimatunda lakini ghafla mambo yanasambaratika tena anaanza upya kwa kujitafuta. Hii unakuta kuna watu babu zao waliwafanyia ubaya na wakawanenea maneno ya laana kwa uchungu.
■kuna koo unakuta umoja hakuna. Ni fitna, kufanyiana uchawi, husda na vinyongo vibaya.
Mtu wa kawaida anaweza kusema haya ni mambo ya kawaida kutokana na mapito ya maisha, lakini ni kwa sababu hajapitia tabu hizi na hajashuhudia kiuhalisia jinsi gani kuna jamii ambazo matatizo yao ni sugu na ya kujirudia.
Na matatizo haya sio mapitio ya kila siku ya maisha bali ni mapitio ya uzamani ulioharibika na kurithiwa ndani yao. Tatizo ni kuwa hakuna wa kusaidia kwa maana kila mtu unakuta na yeye ana miroho ndani yake, yani unakuta moto unakutana na moto. Ila kuna wale mnaopata mwanga kidogo, mjifunze kukemea hizi roho kwa imani yenu binafsi na kwa usaidizi wa watumishi wa Mungu wa wazuri na huku ukitanguliza sadaka ya kuikomboa familia yako.
Tambueni kuwa kuna kero na karaha nyingi za kujirudia zinazotesa koo nyingi. Na inafikia wakati hadi matatizo haya yamekuwa ni ya kuzoereka kutokana na kuchukulia poa au kutokuwa na umoja wa kujaribu wa kuyatatua madhira hayo.
Kinachofatia ni kuhangaika kwa waganga, wachungaji feki, mashehe watoa majini, kurushiana lawama za kulogana baina ya ndugu, etc.
Laana inarithika katika vizazi, laana inasaka wapi pa kutua ili ijitukuze, kwa maana bado inalilia damu ndani yenu kutokana na uchungu uliofanyika na mababu au mabibi zenu kwa watu wengine.
Madhabahu yaliyowekwa na mababu yalijitengeneza kiroho ndani ya ukoo na sasa yakaangaza na kukaa enzi na enzi. Madhabahu hayo yalifanyika katika matambiko ya kishirikina au kuenzi mizimu. Kuumaanisha walikaribisha roho hizo ziweze kuangaza ndani ya damu na vizazi vya ukoo.
■Kuna koo ambazo unakuta wanawake karibia wote wanapitia mateso ya ndoa. Hii unakuta kuna bibi aliwahi kufanya kitu kibaya na wakamlaani yeye na kizazi chake.
■kuna koo unakuta mabinti wanasumbulia na mizimu ya kuagua na uganga eti kisa bibi zao walifanya hivi.
■kuna koo unakuta kuna roho ya visasi na kufanya mauaji inatembea ndani yao. Yani hawakuachi hivi hivi lazima wakufanyie damage ndio walidhike hata kama ni mwanae amemkosea pakubwa.
■kuna koo unakuta majina flani wakipewa watu wanakuwa wafuska sana kwa sababu mtu huyo nae alikuwa mfuska.
■Kuna koo unakuta watu wengi hawana vibali vya kukubalika, anapiga kazi sana, anaona vimatunda lakini ghafla mambo yanasambaratika tena anaanza upya kwa kujitafuta. Hii unakuta kuna watu babu zao waliwafanyia ubaya na wakawanenea maneno ya laana kwa uchungu.
■kuna koo unakuta umoja hakuna. Ni fitna, kufanyiana uchawi, husda na vinyongo vibaya.
Mtu wa kawaida anaweza kusema haya ni mambo ya kawaida kutokana na mapito ya maisha, lakini ni kwa sababu hajapitia tabu hizi na hajashuhudia kiuhalisia jinsi gani kuna jamii ambazo matatizo yao ni sugu na ya kujirudia.
Na matatizo haya sio mapitio ya kila siku ya maisha bali ni mapitio ya uzamani ulioharibika na kurithiwa ndani yao. Tatizo ni kuwa hakuna wa kusaidia kwa maana kila mtu unakuta na yeye ana miroho ndani yake, yani unakuta moto unakutana na moto. Ila kuna wale mnaopata mwanga kidogo, mjifunze kukemea hizi roho kwa imani yenu binafsi na kwa usaidizi wa watumishi wa Mungu wa wazuri na huku ukitanguliza sadaka ya kuikomboa familia yako.