Laaana ya Mzize haitawaacha Yanga mwakani

Laaana ya Mzize haitawaacha Yanga mwakani

Pdidy

JF-Expert Member
Joined
Nov 22, 2007
Posts
61,023
Reaction score
36,892
Kinachoendelea Dili ya Clement Mzize Kuelekea ESPERANCE SPORTIVE DE TUNIS ni Masikitiko Makubwa.👀👀

Dili ya Clement Mzize Kwenda Esperance Sportive de Tunis Linakaribia Kabisa Kuota Mbawa

Yanga Africa walitaka USD Milioni Moja Kama Kuna timu Inataka huduma ya Mzize,Esperance wakaleta hii OFA chapu kwa haraka.

Yanga Africa Wakaomba waandae Mkataba wa Mauziano ya Mchezaji,Esperance wakasema hakuna neno

Yanga Africa wakatuma Esperance huo Mkataba wa Mauziano.

Esperance wakawajibu Yanga Africa Agosti 12,2025 Lakini wakaomba baadhi ya vipengele viwili Kubadilishwa

Yanga Africa wakukubali Lakini wakawaambia Esperance wasubiri Kwasababu siku hiyo walikuwa bize na Harambee ya CCM.

Yanga Africa wamebaki Kimya tangu Agosti 12,2025 Mpaka Leo Agosti 19,2025.

Rais wa Esperance,Hamdi Meddeb amekasirishwa na Hali hiyo na tayari wanatazama Machaguo Mengine ili Kukimbizana na Kufungwa Dirisha la Usajili

Kumbuka Mchezaji ameshakubaliana Maslahi Binafsi na Esperance Sportive de Tunis.

Clement Mzize anakufa moyoni,anataka Kwenda Kucheza timu namba 3 Kwa Ubora kwa Viwango vya CAF. Na Mabingwa wa Champions League Mara 4.

Mshahara wa Mwaka wa Kwanza ni USD350k (🇹🇿Milioni Mia tisa,Laki Saba na hamsini)

Mshahara Mwaka wa Pili wa Mkataba ni USD450 ( 🇹🇿BILIONI moja ,Milioni Mia moja Sitini na Sita laki tisa na tisini)

Kuna Bonasi Clementinho akifunga Goli 10 au Assits 10 ni USD25k (🇹🇿 Milioni Sitini na tano )

Clementinho akicheza 60% ya Mechi za Esperance Kuna bonus ya USD20k ( 🇹🇿Milioni hamsini na moja ,Lakini nane na Sitini na tisa na ushee)

Yanga Africa inaonekana hawataki tena Kumuuza Clement Mzize baada ya Kukataa Kwenda ile Ligi ya Wakulima Qatar na wameanza Kumshawishi na Mshahara wa Milioni Arobaini kwa Mwezi unatajwa.

Esperance Mshahara wao Kwa Mwezi ni Milioni Sabini na Nane Kwa Mwaka wa Kwanza na Milioni Tisini na Saba Mwaka wa Pili .

Jaribu Kuwa Clement Mzize Kwa hivi sasa,Viatu vyake vinakutosha?

Hapa naona Kabisa Kuna Dalili ya Sakata la Alexander Isak na Newcastle United au Ademola Lookman na Atalanta.

-

Toa maoni yako
 
Mwandiko wako tunaujua sio huu

Kuna uwezakano mkubwa sana ukawa umeandikiwa na binti zako

Yote kwa yote maisha ni magumu sana mzize aachwe akatafute maisha mengine huko mbele kwa mbele
 
Mwandiko wako tunaujua sio huu

Kuna uwezakano mkubwa sana ukawa umeandikiwa na binti zako

Yote kwa yote maisha ni magumu sana mzize aachwe akatafute maisha mengine huko mbele kwa mbele
Au mamayakooo nishukuru
 
Yanga haijawahi kutaka kuona mchezaji mzawa akitoka nje ya nchi kujitafutia maslahi manono. Edibily Lunyamila na Mrisho Ngassa wangeweka rekodi za watanzania kucheza Ulaya kabla hata ya Samatta lakini kutokana na kuwa kwenye timu iliyojaa wachawi hawakufanikiwa. Nonda Shabani kama sio ubishi wake binafsi angeishia jangwani.
 
Club zenye hela kama esperence huwa hazibembelezi mchezaji. Yanga wakichelewa tu haya mabilioni anaenda sajiliwa mwingine
 
Hii nchi ni ngumu sana kupata maendeleo kwasababu raia wake kama huyu mtoa mada wana vigumu sana ambavyo ni ngumu kufikiria zaidi ya hicho alichoandika. Mzize ni mali ya Yanga na wana mkataba. Kama Mzize anahitaji kuondoka ni yeye ndo anaetakiwa kudeal na hiyo issue kisheria na taratibu zipo za kufuata ikiwapo kununua mkataba wake mwenyewe. Kama Yanga hawataki kumuuza hiyo ni juu yao, kama ni faida au hasara watapata wao. Nchi yetu imeingia kwenye mfumo mbaya sana wa maisha ya uchawa. Wazazi wametumia rasilimali na pesa nyingi kupeleka watoto shule ili waje kua na tija kwenye jamii na taifa kwa ujumla lakini mwisho wa siku tumetengeneza taifa la watu kujikomba komba kwa watu wakijifanya kupigania haki ya muhusika. Sheria na taratibu zipo ila wapumbavu wachache wanajifanya kupigania haki. Yani mtu aingie mkataba yeye mwenyewe kisheria halafu wewe utoke maporoni huko unakuja kumpambania kweli?! Nchi zilizoendelea huwezi kukuta huu ujinga.
 
Hii nchi ni ngumu sana kupata maendeleo kwasababu raia wake kama huyu mtoa mada wana vigumu sana ambavyo ni ngumu kufikiria zaidi ya hicho alichoandika. Mzize ni mali ya Yanga na wana mkataba. Kama Mzize anahitaji kuondoka ni yeye ndo anaetakiwa kudeal na hiyo issue kisheria na taratibu zipo za kufuata ikiwapo kununua mkataba wake mwenyewe. Kama Yanga hawataki kumuuza hiyo ni juu yao, kama ni faida au hasara watapata wao. Nchi yetu imeingia kwenye mfumo mbaya sana wa maisha ya uchawa. Wazazi wametumia rasilimali na pesa nyingi kupeleka watoto shule ili waje kua na tija kwenye jamii na taifa kwa ujumla lakini mwisho wa siku tumetengeneza taifa la watu kujikomba komba kwa watu wakijifanya kupigania haki ya muhusika. Sheria na taratibu zipo ila wapumbavu wachache wanajifanya kupigania haki. Yani mtu aingie mkataba yeye mwenyewe kisheria halafu wewe utoke maporoni huko unakuja kumpambania kweli?! Nchi zilizoendelea huwezi kukuta huu ujinga.
Wabongo wengi wana shida vichwani. Wao suala la sheria, kanuni na taratibu kwao haliwaingiagi wanapenda ushabiki tu na kukurupuka
 
Hivi mnaelewa maana ya mkataba au mnaropoka tu kama mmepandwa majini? Kwamba Yanga hawataki hela wanataka kumkomoa Mzize? CCM itatawala milele hii nchi
 
Kila siku nasema hapa wakulaumiwa kwanza ni mameneja wa wachezaji wetu wandani na wachezaji wenyewe. Tunajua wachezaji wetu sio rahisi kujua mambo ya sheria na mikataba inakuwaje lakini utakuta wanafanya kosa la kiufundi kuweka mameneja wababaishaji. Ikifika wakati wa kusaini mikataba wao wanaangalia sehemu ya mshahara kwa mwezi na "signing fee" vikiwa poa wanaanguka saini haraka haraka. Vipengele vya muhimu kama akitaka kuvunja mkataba hawaanagalii. Baadae huko mbele ya safari anashangaa akitaka kuvunja mkataba anakuta mkataba unasema ailipe klabu yake bilioni moja halafu klabu ya ikitaka kumvunjia yeye mkatba inatakiwa imlipe milioni hamsini.

Nyie wachezaji na mameneja wenu uchwara hakikisheni kabla ya kusaini mkataba ombeni mpewe walau wiki moja ya kuupitia. Na mkipewa huo mkataba acheni ubahili nendeni kwa wanasheria mahiri lipeni pesa kaeni naye chini awatafsirie na kuwasaidia nini cha kuondolewa au kuongezwa kwenye huo mkataba.

Kwenye suala la Mzize wa kualaumiwa ni huyo Jasmine. Kwa sababu huwa anajinasibu kuwa anajua sheria sasa kinachomkwamisha nini wakati ni juzi tu hapa Mzize kasaini mkataba mpya. Je alishindwa kuweka "clause" inayomlinda Mzize akipata timu yenye malahi makubwa?

Kwa nini wachezaji wetu wa ndani kila SIKU kulia kulia tu? Kwa nini wasijifunze kwa wenzano wa nje kwenye ishu ya mikataba?

Ni mtizamo tu.
 
Hivi mnaelewa maana ya mkataba au mnaropoka tu kama mmepandwa majini? Kwamba Yanga hawataki hela wanataka kumkomoa Mzize? CCM itatawala milele hii nchi
Yanga ikisema tunataka dola 1m ipo sahihi kukataa ofa chini ya hapo, ikisema hatumuuzi mchezaji pia ipo sahihi. Ila ikisema tunamuuza, tunataka dola 1m, ikaja dola 1m halafu isirespond kama mleta mada anavyosema hapo sasa kuna dalili ya kukomoana, unless kuna ofa nzuri zaidi inategemewa. Wachezaji wawe makini sana na mikataba wanayosaini esp vipengele vya kuvunja mkataba.
 
Back
Top Bottom